Kama tunamsifu Nyerere kwenye mambo ya madini,je mgodi wa Almasi Mwadui mbona haujalisaidia taifa?

chiembe

JF-Expert Member
May 16, 2015
11,636
19,860
Watanzania turudi kwenye ukweli na tuache kulishwa propaganda ,tunaambiwa eti Mwalimu Nyerere (R.I.P) alikuwa makini sana kwenye mambo ya madini na maneno mengine meeengi!!

Sasa tujiulize,mgodi wa Almasi mwadui ulikuwepo tangu nchi unapata Uhuru mwaka 1961 mpaka Nyerere anaachia ngazi mwaka 1985,mbona hatuelezwi mgodi huu ulileta faida gani kwa taifa?

Mbona hatuelezwi mikataba yake ilikuwaje?

Tunataka tuujue uzalendo wa Mwalimu Nyerere katika mgodi huu wa Almasi mwadui ........na kwa nini hauguswi na tume zote za serikali,yaani tume zote ni Tanzanite na Dhahabu,almasi vipi? Hasa ya Mwadui?

Mikataba ya Serikali ya Nyerere na Mwadui ilikuwaje na ikoje?
 
Watanzania turudi kwenye ukweli na tuache kulishwa propaganda ,tunaambiwa eti Mwalimu Nyerere (R.I.P) alikuwa makini sana kwenye mambo ya madini na maneno mengine meeengi!!

Sasa tujiulize,mgodi wa Almasi mwadui ulikuwepo tangu nchi unapata Uhuru mwaka 1961 mpaka Nyerere anaachia ngazi mwaka 1985,mbona hatuelezwi mgodi huu ulileta faida gani kwa taifa?

Mbona hatuelezwi mikataba yake ilikuwaje?

Tunataka tuujue uzalendo wa Mwalimu Nyerere katika mgodi huu wa Almasi mwadui ........na kwa nini hauguswi na tume zote za serikali,yaani tume zote ni Tanzanite na Dhahabu,almasi vipi? Hasa ya Mwadui?

Mikataba ya Serikali ya Nyerere na Mwadui ilikuwaje na ikoje?
"Makini sana" maana yake nini?
 
sijaelewa unataka kuhalalisha nini!
kwamba, hata kama nyerere aliboronga ndo iwe nafuu ya Chenge, washirika wake na chama dada chote?
nadhani ulikusudia kuupeleka uzi huu kwenye jukwaa na UTANI
Sijui hujaelewa nini,labda wewe ni wale wanaojua kusoma na kuandika
 
Magufuli kashaharibu, huyu si ajabu alitarajia awe na Noah ndipo aine amenufaika. Mwadui tuna 30+% shares na faida tunapata.
 
Kama huwezi kutuambia maana unayoielewa wewe ya "makini sana" mjadala huu hauwezi kwenda popote.

"Makini sana" kwako inaweza kuwa "kukosa umakini sana" kwa mwingine.

Hata kama mnatumia kamusi moja.
Basi ondoa neno makini sana halafu endelea na mjadala
 
Maana yake ni hiyo uliyoiona hapo kwenye mada
Ipi? Hujaitaja.

Umetumia maneno ambayo hujaeleza unamaanisha nini na kwa hiyo mjadala wako unakosa maana.

"Makini sana" ni nini? Unapimaje huyu "makini sana" na huyu si "makini sana"?
 
3 Reactions
Reply
Back
Top Bottom