Kama tunaandaa Bajeti pasipo kuzingatia athari za Corona, sitashangaa siku moja tukalazimika kuwa na Bunge la dharua ku-review upya Bajeti yetu

Salary Slip

JF-Expert Member
Apr 3, 2012
47,013
144,371
Mbali na kusababisha madhara ya kijamii ni wazi corona itaathiri uchumi wetu kwani inagusu sekta muhimu kwa uchumi wa nchi yetu ambayo ni sekta ya utalii,sekta tunayoambiwa inachangia asilimia 25 ya mapato ya nchi yetu.

Vile vile ikitokea ugonjwa unasambaa na kutulazimisha kufikia hatua ya ku-restrict movement na shughuli za watu,sekta nyingi zaidi zitaathirika na hivyo kuongeza hatari ya kuporomoka kwa uchumi.

kwa maana hiyo, kama kweli Bajeti yetu haiangalii athari zinazoweza kujitokeza kutokana na ugonjwa huu kama Mhe.Mbowe alivyodai Bungeni,sitashangaa kuona siku moja tunalazimika kuwa na Bunge la dharura kupitia upya Bajeti yetu au kuwa na vikao vya Bunge vya kupitia upya Bajeti yetu katika mojawapo ya mikutano ya Bunge iliyopo katika ratiba za Bunge.

Japo kuna taarifa za mashirika na taasisi za kifedha kutoa mikopo kusaidia nchi zinazoendelea kukabiliana na athari za kiuchumi zinazotokana na corona pamoja na mapendekezo ya kutufutia madeni, sidhani kama hatua hizi zinaweza kutunusuru ukizingatia uwezekano wa ahadi hizi za mabeberu kutotimizwa kabisa au kutotimizwa kwa asilimia mia moja.

Hivyo,ushauri wa Mbowe na ule wa ACT uzingatiwe, vinginevyo ipo siku tunaweza kujikuta tunalazimika kutekeleza ushauri huo tukiwa tayari tumechelewa.
 
Siku hizi Tanzania hakuna bunge. Labda kama unaongelea nchi nyingine lakini kama ni bongi basi serikali inajifanyia chochote inachotaka.

Bajeti imebakia kuwa porojo za kwenye makaratasi tu ila kinachofanywa na serikali na taasisi zake kinaamuliwa na kikundi cha watu wachache waliopora mamlaka ya kila kitu.

Kwa sasa bunge limekuwa kama taasisi ya kutafuna pesa za wananchi bila kufanya kazi. Na awamu ya 5.2 ya bunge la kuteuliwa nayo sahau mambo ya bunge.

Tuzitafute barakoa (face mask) kabla hazijawa dili. Na pia tuvitumie vile viwanda vya cherehani kujitengenezea maski.
 
Mambo ya majanga na dharula si kwamba linakuwa fungu linalopangwa ndani bajeti ya waziri mkuu? Kwani bajeti ya waziri mkuu haipo? Kwa nini una mashaka? Nafikiri itakuwa imezingatiwa! Anyway so mbaya kutaka kujua, ingawa naamini viongozi wetu hawawezi kutozingatia hilo.
 
Kwa mwenendo wa taifa letu hata wataalamu wetu mbali wabunge lala salama hii japo corona hatari na tishio hawasubu kuipa corona uzito unaostahili kufuatia commet ya mkuu ...." tusitishane sana....mengine siyo yetu... litapita..."

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mambo ya majanga na dharula si kwamba linakuwa fungu linalopangwa ndani bajeti ya waziri mkuu? Kwani bajeti ya waziri mkuu haipo? Kwa nini una mashaka? Nafikiri itakuwa imezingatiwa! Anyway so mbaya kutaka kujua, ingawa naamini viongozi wetu hawawezi kutozingatia hilo.
Kwanini "udhani"?? Tuje na facts itatusaidia
 
Back
Top Bottom