Spy1983
Senior Member
- May 24, 2018
- 131
- 159
Yupo Studioni sasa EFM kwenda ' Kuzurula ' na ' Kuwadanganya ' wana Yanga SC na ameulizwa Swali dogo lenye Kuhitaji jibu fupi tu na Mtangazaji Tunu Hassan Shemkome na Majibu yake ( Injinia Hersi Said ) yakawa hivi ( haya ) ....
Swali Mtangazaji Tunu...
Je, bado Injinia Hersi anadhani Yanga SC inaenda kuwa Bingwa wa VPL kama alivyosema na Kuwaaminisha wana Yanga?
Jibu la Injinia Hersi wa GSM....
Yanga SC imetoka mbali sana ilikuwa na Njaa na uwezo wa Kipesa ulikuwa ni mdogo mno. Sasa hivi Yanga SC kuna Heshima na Wachezaji wengi wanaitwa Timu za Taifa kama Mukoko, Yacouba na Mwamnyeto. GSM tumeweza kuwa na Msaada mkubwa Yanga SC hadi kuwa ni Timu yenye Jezi nzuri kuliko Timu zote za VPL hapa nchini. GSM tunaendelea kuibadili Yanga SC hasa Kimfumo na kuwa na Idara mbalimbali ili kuleta Ufanisi wa Kiutawala na Kimasoko.
Asanteni sana EFM kwa kutuletea 'Mpuuzi' na 'Msanii' huyo hapo Studioni kwenu leo.
Na GENTAMYCINE nawatakia kila Ia kheti wale Wote mnaoendelea kusikia ' Ngonjera ' za Injinia Hersi Said wa GSM na Yanga SC.
Mwisho Wewe Mtangazaji wa Kipindi hicho cba Michezo Tunu Hassan Shemkome umeonyesha ' how unprofessional you're ' kwa Kukubali ' Source ' wako huyo Injinia Hersi Said ' akumeze ' Kimaongezi huku ukishindwa ' Kumbana ' ajibu Kwanza Swali la Msingi ulilomuuliza awali na sasa kumuacba ' akibwabwaja ' tu hapo Studioni.
Umeonyesha ' Udhaifu ' mkubwa kama Mtangazaji na Mwandishi wa Habari. Ndiyo maana hivi sasa Fani nzima ya Uandishi wa Habari nchini ' inadharaulika ' na Wewe ( Tunu Hassan Shemkome ) umeongeza ' Kudharauliwa ' kwa Tasnia hiyo nzima.
Tatizo watu wameanza kupenda timu badala ya mpira…. Na watu wanapenda kusikia propaganda badala ya uwalisia pia wanapenda story za vijiweni ulikuwa progress ya timu… GSM wamefanya makubwa sana kuliko hata kuchukua ubingwa… Yanga ina Kambi ya Kisasa kuliko hata Simba niwaambie