Kama Taifa, viongozi wetu wasituchukulie sisi kama watoto wadogo

brazaj

JF-Expert Member
Jul 26, 2016
27,824
35,827
Mabibi na mabwana sisi ni taifa na kama taifa cheo ni dhamana tu.

Kiongozi yeyote kwa uongozi wake ni muhimu akazingatia ukweli kuwa kwa dhamana aliyo nayo si kuwa sasa eti ndiyo anayo fursa kamili ya kufanya au hata kusema lolote kwa kuwa tu eti dhamira yake itakuwa imemtuma huko.

Rais wetu kutaka kutuaminisha kuwa chanjo ya corona inaweza kuwa na walakini kwa kuwa tu imetengenezwa na anaowaita mabeberu ni jambo lisilokubalika.

Kwani ni chanjo ipi au dawa ipi ambayo haitengenezwi na mabeberu? Kama ana mashaka hayo kwanini hajawahi kusema lolote kwenye chanjo za polio, Pepo punda, ndui, nk?

Ieleweke kuwa kutofautiana kwa mawazo ni jambo la kheri wala si uhaini.

"Kama watoto mapacha hufikia hatua ya kutokuelewana. Sembuse mimi na wewe Neema?"

Sisi: mmoja mmoja na kwa jumuiya mbali mbali zikiwamo wana harakati, madhehebu za dini, wasomi, nk kwa roho safi ni muda sasa wa kumhitaji mheshimiwa huyu kubadili uelekeo.

Kwa hakika, kuunyamazia uelekeo huu ni kuyaweka maisha yetu wenyewe hatarini pasipo na uhalali wowote.

Ninawasilisha.
 
Kwani umekatazwa kwenda kuchanja bwashee?

Maoni yenu msitake kutujumuisha na wengine.

Lengo lenu ni kutaka kukwepa wajibu wenu wa serikali wa kununua chanjo kwa ajili ya maisha ya watu ili tu kununua madege kwa cash?

Si mseme tu kuwa hela za kodi ambazo aghalabu hamlipi mnazitumia ndivyo sivyo na sasa hivi sasa ndiyo tuko hapa?
 
Huyu anatuchosha tu.

Mzungu hakwepeki hata yeye hajawagusa tu. Alitafutwa yule wa Iran kwa drone na wakamshughulikia sembuse huyu aliyepo Chato barabarani.

Sisi tunaagiza kila kitu nje. Wakitaka kutumaliza it is just a cake.

Asituchoshe.
 
Sawa muuza barakoa tumekuelewa

Barakoa siuzi ila navaa tena ya kanga. Napenda kuendelea kuishi.

Vaa barakoa jombi, jitahidi angalau 1.5m kwenye kadamnasi, bila kusahau maji tiririka na sabuni ya mche japo ile ya kufulia.

Inshallah hautajuta kwa jitihada hizo.

Usisahau kwingine wananunua chanjo. Kwetu wasiolipa hata kodi wananunua midege.
 
Mleta mada una akili sana..Nakumbuka wakati wa harakati za kuiangamiza Polio na Pepo Punda kuna watu walikataa kuwepeleka watoto wao kupata hizo chanjo na Serikali iliwachukulia hatua.Cha kujiuliza ni utafiti upi umefanyika apa Tz na kuonyesha kua hizo chanjo zina madhara au nikufuata tu mkumbo kisa kaongoea mwanaccm
 
We beba familia yako ukaipate hiyo chanjo tuone km hujarudi na mtindio wa akili.

Usinifokee Mburula wewe.

Unaujua hata huo utaratibu wa upatikanaji hiyo chanjo ulivyo?

Kwamba hela zimeenda kununua madege sasa ndiyo mmetumwa kusafisha hilo kwa kuwa hela za chanjo hazipo na mnatumai mtazuga.

Fumbo fumbieni wajinga.
 
Msamehe bure hawa ndo bado wanaendeshwa akili na wazungu.

Unaandika kwa uzi upi jombi?

Uzi huu haukubaliani na mawazo ya mh. rais Magufuli. Baridi kabisa kama binadamu mwenye akili timamu.

Kwa maana nyingine uzi huu unatambua kuwa katika jamii ambayo misukule kama wewe ipo na wenye akili zao pia wapo. Asijisahau kwa hilo.

Jiridhishe kuwa umeuelewa uzi
😂😂😂😂😂😂😂😂😂.
 
Maoni yenu msitake kutujumuisha na wengine.

Lengo lenu ni kutaka kukwepa wajibu wenu wa serikali wa kununua chanjo kwa ajili ya maisha ya watu ili tu kununua madege kwa cash?

Si mseme tu kuwa hela za kodi ambazo aghalabu hamlipi mnazitumia ndivyo sivyo na sasa hivi sasa ndiyo tuko hapa?
Wanathamini madege kuliko raia tena walipa kodi,sijui hayo madege watapanda kina nani
 
Unachelewa kuipata hiyo chanjo kimbia peke yako usitushawishi ujinga!
Km chanjo wanayo mbona bado wanaisha wewe ni Nani ukapone?
Kaz tunayo kumne tuna watu wapuuzi kias hiki
IMG_20201126_084846.jpg
 
Mabibi na mabwana sisi ni taifa na kama taifa cheo ni dhamana tu.

Kiongozi yeyote kwa uongozi wake ni muhimu akazingatia ukweli kuwa kwa dhamana aliyo nayo si kuwa sasa eti ndiyo anayo fursa kamili ya kufanya au hata kusema lolote kwa kuwa tu eti dhamira yake itakuwa imemtuma huko.

Rais wetu kutaka kutuaminisha kuwa chanjo ya corona inaweza kuwa na walakini kwa kuwa tu imetengenezwa na anaowaita mabeberu ni jambo lisilokubalika.

Kwani ni chanjo ipi au dawa ipi ambayo haitengenezwi na mabeberu? Kama ana mashaka hayo kwanini hajawahi kusema lolote kwenye chanjo za polio, Pepo punda, ndugu nk?

Ieleweke kuwa kutofautiana kwa mawazo ni jambo la kheri wala si uhaini.

"Kama watoto mapacha hufikia hatua ya kutokuelewana. Sembuse mimi na wewe Neema?"

Sisi: mmoja mmoja na kwa jumuiya mbali mbali zikiwamo wana harakati, madhehebu za dini, wasomi, na jumuiya mbali mbali kwa roho safi ni muda sasa wa kumhitaji mheshimiwa huyu kubadili uelekeo.

Kwa hakika, kuunyamazia uelekeo huu ni kuyaweka maisha yetu wenyewe hatarini pasipo na uhalali wowote.

Ninawasilisha.
Wewe jomba sijajua unalilia nini na uzi wako huu...Nani amekukataza kwenda kujidunga hizo dawa...umekatazwa...? Kila mtu ana maamuzi yake hujafungwa na lolote .fanya maamuzi sahihi yanayokufaa ..sisi wengine tupo na Rais wetu bega kwa bega mpk kieleweke
 
Back
Top Bottom