Kama Taifa ifikie nyongeza ya mshahara iwe inadaiwa mahakama kuu pale serikali inapowanyima wafanyakazi bila sababu za msingi

Chagu wa Malunde

JF-Expert Member
Jul 11, 2015
8,708
5,711
Kwanza kabisa watanzania wanatakiwa kutambua kuwa kila mtanzania anayo haki ya kupata mshahara unaostahili kukidhi mahitaji ya msingi. Ibara ya 23(2) imetamka wazi kuwa watanzania wanaofanya kazi wanatakiwa wapate just remuneration. Hivyo kupata mshahara unaostahili ni takwa la kikatiba na ni haki ya msingi.

Inapotokea mkuu wa nchi haongezi mshahara watumishi wa umma au sekta binafsi kwa muda wa miaka sita hili ni tatizo kubwa. Mbaya zaidi ni sababu zinazokuwa zinatolewa kuwa ni kuwekeza kwanza kwenye maendeleo ya taifa ili baadae wafanyakazi waongezwe mishahara.

Mbaya zaidi wakati mnajikita kuwekeza kwenye maendeleo gharama za maisha pia zinapanda juu hivyo ni wazi kuwa hata kama taifa linajenga miundo mbinu, shule na mahospital kwa miaka sita gharama za maisha pia zitakuwa zimepanda juu, maana miaka sita sio haba.

Achana na kujikita katika kuwekeza kwenye maendeleo. Mkuu wa nchi anaposema kuwa hawezi kuongeza mshahara sababu ya ugonjwa ambao haijulikani lini utaisha hili nalo ni tatizo. Kama Covid 19 ndio sababu ya kushusha uchumi na pato la taifa letu. Tunafahamu lini huu ugonjwa utaisha ili uchumi wetu upande na kupandisha mishahara?

Hivyo ni wazi kuwa kama Katiba ya JMT inatamka kuwa wafanyakazi wanatakiwa kulipwa mshahara unaokidhi mahitaji yao, basi serikali hainabudi kuwaongeza. Maana sababu zinazotolewa kutoongeza mishahara hazina mashiko. Gharama za maisha zimepanda na katiba inapaswa kuzingatiwa.

Hivyo kama ikitokea kuna namna serikali inakuwa inatoa sababu hazina mashiko juu ya kuongeza mishahara watumishi wafanyakazi wawe wanaenda mahakamani kudai haki hiyo ya kikatiba.
 
Kwa nini wafanyakaz huongezewa au huwa wanastahili kuongezewa mshahara?
 
Piganeni uzalishajai wenye ufanisi na uchumi upande, mpaka watu wawe na uwezo wa kuacha kazi zenye mishahara midogo serikalini, waende kufanya kazi zenye mishahara mikubwa au biashara sekta binafsi.

Karibu dunia nzima kazi za serikali ni kazi zenye mishahara midogo.Kuna siku nilikuwa naangalia kitu kinahusiana na kazi za wafanyakazi wa Ikulu ya Marekani. Uzuri wa Marekani vitu vingi vinawekwa wazi mitandaoni, hususan vitu vya serikali vinavyoenda kwa kodi za wananchi.

Nilivyoona mishahara yao (wafanyakazi wa White House) wengi sana ilikuwa kama wanafanya kazi za kujitolea, wengine mishahara yao niliwazidi kwa mara mbili, wengine karibia mara tatu.Hawa ni watu waliosoma mpaka graduate school wengi wao,wana formal education ya masters level au zaidi, na uzoefu mzuri tu.

Kazi za serikali ni kati ya kazi zenye mishahara midogo kabisa.

Ndiyo maana unaweza kukuta mtu kama Dr. Sanjay Gupta wa CNN aliombwa kuwa Surgeon General na rais Obama, akakataa.
Kazi kubwa, mshahara mdogo, lawama nyingi.

Akajikita private sector CNN huko tu.

Wafanyakazi wa serikali hata Marekani mishahara yao, chukua mfano wa White House chini ya Director level, ukiiangalia unaona kabisa hawa hawakwenda kufanya kazi kwa sababu ya mshahara. Ama wana nia ya kusaidia watu, ama wanataka kutengeneza connections na experience wazifanyie kazi baada ya kufanya kazi serikalini.

Kuna gavana mmoja wa state maarufu Marekani aliamua kutogombea tena u gavana, huku watu wanampenda bado. Aliulizwa na mtu wangu wa karibu kwa nini hagombei?Akajibu kwamba kazi za serikali zina maslahi madogo, anataka kwenda kufanya kazi kwenye private sector kwenye maslahi makubwa, kwani anaona kashachangia uongozi wa serikali, ni zamu ya watu wengine kuchangia. Yeye ana familia na ana mambo mengi ambayo mshahara wa serikali hautoshi, na hawezi kufanya biashara kubwa kwa sababu ya mambo ya masharti mengi ya kimaadili ya viongozi, bora arudi uraiani ataweza kufanya vizuri zaidi financially kuliko kazi za serikali.

Huyo gavana wa state kubwa tu Marekani, anaondoka kazi za serikali kwa sababu anaona kashachangia kwenye uongozi, anataka kutengeneza mambo yake financially kwenye private sector. Kufanya kazi serikalini aliona kama anajitolea kutimiza civic duty yake tu, lakini kiuhalisia kila mwaka anaofanya kazi serikalini alikuwa anapoteza mamilioni ya dola za Kimarekani ambayo angeweza kutengeneza private sector.

Sisi tatizo letu hatuna private sector ya kueleweka ku absorb watu, watu wanahemea kazi za serikali na wanataka ziwatoe. Granted, mishahara ikiwa chini sana inakuwa kama utumwa, hata kazi ya wito lazima iangalie basic needs.Lakini, bila kujenga private sector yenye ufanisi na uchumi mzuri, kutegemea mishahara ya serikali ipande ni mbio za sakafuni. Kwa sababu serikali yenyewe inaendeshwa kwa kodi za private sector.

Ukianza kupanga mshahara mkubwa na kuulazimisha serikalini, kama nchi ina uchumi mdogo, walipa kodi wachache, hata huo mshahara serikali ikipandisha itakuwa na matatizo kulipa watu.

Hizi ni kanuni za uchumi tu.
 
Tumia akili kdg, unaweza kupewa hiyo nyongeza ya kila mwaka ila PAYE ikawa kubwa sana. Hata hiyo nyongeza ikaoneka si kitu chochote
 
Piganeni uzalishji wenye ufanisi na uchumi upande, mpaka watu wawe na uwezo wa kuacha kazi zenye mishahara midogo serikalini, waende kufanya kazi zenye mishahara mikubwa au biashara sekta binafsi.

Karibu dunia nzima kazi za serikali ni kazi zenye mishahara midogo.Kuna siku nilikuwa naangalia kitu kinahusiana na kazi za Wafanyakazi wa Ikulu ya Marekani. Uzuri wa Marekani vitu vingi vinawekwa wazi mitandaoni, hususan vitu vya serikali vinavyoenda kwa kodi za wananchi.

Nilivyoona mishahara yao (wafanyakazi wa White House) wengi sana ilikuwa kama wanafanya kazi za kujitolea, wengine mishahara yao niliwazidi kwa mara mbili, karibia tatu.Hawa ni watu waliosoma mpaka graduate school wengi wao,wana masters au zaidi.

Lakini mishahara yao ukiiangalia unaona kabisa hawa hawakwenda kufanya kazi kwa sababu ya mshahara. Ama wana nia ya kusaidia watu, ama wanataka kutengeneza connections na experience wazifanyie kazi baada ya kufanya kazi serikalini.

Kuna gavana mmoja wa state maarufu Marekani aliamua kutogombea tena u gavana, huku watu wanampenda bado. Aliulizwa na mtu wangu wa karibu kwa nini hagombei?Akajibu kwamba kazi za serikali zina maslahi madogo, anataka kwenda kufanya kazi kwenye private sector kwenye maslahi makubwa, kwani anaona kashachangia uongozi wa serikali, ni zamu ya watu wengine kuchangia.

Sisi tatizo letu hatuna private sector ya kueleweka ku absorb watu, watu wanahemea kazi za serikali na wanataka ziwatoe. Granted, mishahara ikiwa chini sana inakuwa kama utumwa, hata kazi ya wito lazima iangalie basic needs.Lakini, bila kujenga private sector yenye ufanisi na uchumi mzuri, kutegemea mishahara ya serikali ipande ni mbio za sakafuni. Kwa sababu serikali yenyewe inaendeshwa kwa kodi za private sector.

Ukianza kupanga mshahara mkubwa na kuulazimisha serikalini, kama nchi ina uchumi mdogo, walipa kodi wachache, hata huo mshahara serikali ikipandisha itakuwa na matatizo kulipa watu.

Hizi ni kanuni za uchumi tu.
Hoja hapa ni kuongeza mishahara kwa mujibu wa katiba ya JMT. Hivyo iwe ni mshahara mdogo au mkubwa lakini lazima uwe just renumeration. Hakuna nchi isiyokuwa na sekta ya umma au binafsi. Kama ndio hivyo hata huko Usa watu wote wangefanya kazi sekta binafsi.
 
Tumia akili kdg, unaweza kupewa hiyo nyongeza ya kila mwaka ila PAYE ikawa kubwa sana. Hata hiyo nyongeza ikaoneka si kitu chochote
Nyongeza ya namna gani unayoizungumzia? Mimi nazungumzia nyongeza inayokidhi mahitaji ya mfanyakazi. Nakushauri wewe acha kukariri kuwa Paye ndogo ndio kupata mshahara mkubwa.
 
Wafanyakazi wa serikalini mnapenda sana kulialia,wenzenu wa binafsi hawajui mambo hayo mnayodai na wanaishi.Hawana mikopo wala nyongeza wanaishi tu na wamejipanga vizuri hadi ni wenye nyumba wenu.Nyie mnafeli wapi?
 
Wafanyakazi wa serikalini mnapenda sana kulialia,wenzenu wa binafsi hawajui mambo hayo mnayodai na wanaishi.Hawana mikopo wala nyongeza wanaishi tu na wamejipanga vizuri hadi ni wenye nyumba wenu.Nyie mnafeli wapi?
Hao wa sekta binafsi unaowazungumzia ni wa aina gani? 80% ya sekta binafsi wanafanya kazi kwa wachina na wahindi na mishahara yao ni midogo sana.
 
Hao wa sekta binafsi unaowazungumzia ni wa aina gani? 80% ya sekta binafsi wanafanya kazi kwa wachina na wahindi na mishahara yao ni midogo sana.
Kwa hiyo hawastahili nyongeza?Mbona wanakatwa kodi inaenda Serikalini kama ni kwa wahindi na wachina wasiachwe tu?Watu walipe kodi wanaofanya kazi kwa wachina wewe upewe nyongezza ya mshahara?Sasa sikiliza Chagu,Ili nyongeza iwepo lazima uchumi ukue.
 
Kwa hiyo hawastahili nyongeza?Mbona wanakatwa kodi inaenda Serikalini kama ni kwa wahindi na wachina wasiachwe tu?Watu walipe kodi wanaofanya kazi kwa wachina wewe upewe nyongezza ya mshahara?Sasa sikiliza Chagu,Ili nyongeza iwepo lazima uchumi ukue.
Mkuu kwani rais akitangaza nyongeza kima cha chini huwa anabagua sekta binafsi?
 
6 Reactions
Reply
Back
Top Bottom