MINOCYCLINE
JF-Expert Member
- Apr 2, 2015
- 8,011
- 16,748
Binafsi hivi majuzi tu tena nikiwa Sokoni nimekutana na Wamachinga na Wanyonge ( Masikini ) wakiwa wanasema hauna Upendo Kwao kama aliokuwa nao Mwendazake.
Nilijitahidi kukutetea kwa Nguvu zote mpaka pale nilipoona naanza Kuzungukwa nao ( kuwekwa Mtu kati ) huku Nyuso zao zikiwa na Jazba na kutumia Akili ya ziada nikawazuga kidogo na kuondoka kwani nilihisi kilichokuwa kinafuata pale ni Mimi Krav Maga kupokea Kipondo.
Hali hii ikanipelekea Kujiuliza ni Kitu gani Mwendazake aliwapa hawa Wamachinga na Wanyonge ( Masikini ) wenzangu kiasi kwamba walimuamini na kumpenda 100%, ila Kwako Wewe ni tofauti japo mara kwa mara unarejea Kauli Mbiu yako ya Kazi Iendelee na utafanya yale yale aliyokuwa akiyafanya?
Na hakuna Kitu kinachowauma kama siyo Kuwakera kwa sasa pale wakikuona kila mara upo Juu Angani kama Popo kwa Kusafiri na Ndege huku Gari ukiwa huzitaki kabisa wakati Kero zao zilizoanza Kujitokeza kama ile ya pale Stendi Mpya Mbezi Lois na hii ya Juzi ya hapo Ilala ukiwa umezinyamazia wakati Mwendazake angekuwepo angeshazitatua mara moja.
Wakati nabishana nao Sokoni nikiwa nakutetea kuna Mmoja nilimsikia akisema Tanzania sasa imempata Rais Mrembo na Mpaka Mafuta ya Kuuongeza tu Weupe wake Usoni na muonyesha Mitindo ya Mavazi. Nilitaka Kumjibu ila nilipomuangalia vizuri Mkononi nikaona ameshika Kisu cha Kuchinjia Kuku na Kuogopa kuwa huenda ningethubutu kunyanyua Mdomo wangu leo hii ama ningekuwa ICU Muhimbili au naendelea tu Kuganda na Friji za Mochwari ya Mwananyamala Hospitali.
Mama lifanyie sana Kazi hili Uaminike.
Nilijitahidi kukutetea kwa Nguvu zote mpaka pale nilipoona naanza Kuzungukwa nao ( kuwekwa Mtu kati ) huku Nyuso zao zikiwa na Jazba na kutumia Akili ya ziada nikawazuga kidogo na kuondoka kwani nilihisi kilichokuwa kinafuata pale ni Mimi Krav Maga kupokea Kipondo.
Hali hii ikanipelekea Kujiuliza ni Kitu gani Mwendazake aliwapa hawa Wamachinga na Wanyonge ( Masikini ) wenzangu kiasi kwamba walimuamini na kumpenda 100%, ila Kwako Wewe ni tofauti japo mara kwa mara unarejea Kauli Mbiu yako ya Kazi Iendelee na utafanya yale yale aliyokuwa akiyafanya?
Na hakuna Kitu kinachowauma kama siyo Kuwakera kwa sasa pale wakikuona kila mara upo Juu Angani kama Popo kwa Kusafiri na Ndege huku Gari ukiwa huzitaki kabisa wakati Kero zao zilizoanza Kujitokeza kama ile ya pale Stendi Mpya Mbezi Lois na hii ya Juzi ya hapo Ilala ukiwa umezinyamazia wakati Mwendazake angekuwepo angeshazitatua mara moja.
Wakati nabishana nao Sokoni nikiwa nakutetea kuna Mmoja nilimsikia akisema Tanzania sasa imempata Rais Mrembo na Mpaka Mafuta ya Kuuongeza tu Weupe wake Usoni na muonyesha Mitindo ya Mavazi. Nilitaka Kumjibu ila nilipomuangalia vizuri Mkononi nikaona ameshika Kisu cha Kuchinjia Kuku na Kuogopa kuwa huenda ningethubutu kunyanyua Mdomo wangu leo hii ama ningekuwa ICU Muhimbili au naendelea tu Kuganda na Friji za Mochwari ya Mwananyamala Hospitali.
Mama lifanyie sana Kazi hili Uaminike.