Shimba ya Buyenze
JF-Expert Member
- Dec 22, 2014
- 178,111
- 1,076,912
Si mlikuwa mmechoshwa na upole wa JK nyinyi? Mmeanza kumkumbuka hata mwezi haujaisha. Tena wengine mlisema rais ajaye awe dikteta. Sasa kilio chenu kimesikiwa makelele ya nini tena?
Wanabodi,
Tanzania ni nchi inayofuata utawala wa sheria, hivyo itaongozwa kwa mujibu wa sheria taratibu na kanuni!, no one is above the law!. Katika kufuata sheria hizo, taratibu na kanuni, pia kuna mamlaka ambayo katiba imempa rais wetu wa JMT kuyatekeleza at his pleasure, yaani vile rais atakavyoona inafaa, ikiwemo presidential appointments powers, and the power to hire and fire civil and public servants!.
Hata kama Dr. Magufuli ni rais wetu, haina maana ana inherent powers kuamua chochote na watendaji walio chini yake kazi yao ni kusema tuu 'YES!", "ndiyo mzee!". Ila kwa hali ninayoina sasa, jee kuna ubaya tukimshauri rais wetu, kamu huu Sio Udikiteta?!, then ni bora sana, Mhe. Rais aka "Futilia Mbali Utawala wa Sheria, kuamua kuongoza kwa kutumia Presidential Decrees!, yaani kina anachokotaka rais na kukisema kinaandikwa na kinakuwa sheria!, kiukweli atafanikiwa sana!.
Rais alipoamuru zile pesa "private money", zilizochangwa na private entities, zikiwemo public corporation, kama sehemu yao ya CSR kuwakiimu wabunge wapya kwa mlo wa usiku!, alitumia mamlaka gani?!. Yaani rais anaweza kuamuru private entities watumieje fedha zao?!, kwa sheria ipi, kanuni ipi na taratibu ipi?!. Huu kama sio udikiteta ni nini?!.
Alipoamua hayo, wengi wameishia tuu kupiga makofi, hakuna aliyejiuliza, agizo hilo amelitoa kwa mamlaka gani?!.
Njuavyo mimi mashirika na makampuni yanatenga fungu fulani za kufanya shughuli za CSR ili ku achieve specific objectives kwenye strategic plans zao!. Kama Bunge liliomba udhamini wa mlo wa usiku, na mashiika na makampuni wakaona zina fit kwenye zile CSR zao, wakatoa, rais alikuwa na mamlaka gani ya kuingilia na kuamuru diferent use ya private money?!.
Hata kama rais ameona matimizi yale yalikuwa ni anasa tuu, angeliamuu bunge likatae michango hiyo, na kuirudisha kwa wenyewe ili zipangiwe CSR nyingine, na rais kama alihitaji hizo fedha zipelekwe kuhudumia wagonjwa Muhimbili wenye uhitaji mkubwa zaidi wa vitanda kuliko mlo wa wabunge, angeomba kama waombaji wengine!.
Baada ya kufanikiwa kwenye hili na kupongezwa, leo rais wetu ameibuka na jinginekufuta parade ya uhuru!. Swali ninalojiuliza hivi kumbe parede ya uhuru ni miongoni mwa sherehe zinazoadhimishwa at the pleasure of the president?!. Nilifikiri hii ndio the no 1 state event na ipo kwa mujibu wa sheria, taratibu na kanuni?!, hivi ni kweli ais wa nchi anaweza tuu kuamka asubuhi na kuamuru maandimisho ya parade ya uhuru yafutwe just like that?!, mamlaka hayo rais wetu ameyatoa wapi?!.
Mbaonaje mkiungana na mimi, tumshauri rais wetu ili kuyanyoosha mambo yake vizuri, awe na mamlaka ya kufanya kila anachotaka, mnaonaje kama atasitisha utawala wa sheria kwa muda, badala yake aongoze kwa kutumia pesidential decrees pekee?!.
Kuna Jambo niliwahi kulizungumza hapa, sasa naona kama linakwenda kutokea!.
If You Can't Beat Them, Join Them!, He is a Worst Dictator!.
Mungu Ibariki Tanzania,
Mungu Mbariki Rais Wetu, Dr. John Pombe Joseph Magufuli.
Pasco.
Hata kama ni cost cutting sio kufuta kabisa ile fhifa ya kitaifa
Jamaa wa parade waende wapige kwata wale hakuna posho mshahara si wanalipwa
Kwangu hata akisema ku.tom.ba mara moja tu kwa wiki na goli moja tu na muda uliobaki tukafanye kazi ili tutoke hapa, sawa tu! Kama unataka mambo ya demokrasia, kuandamana na kuunda tume ya kila upuuzi hamia Kenya huko ndiyo kuna huwo upuuzi, ila hapa kwetu ni amri tu ktk juu kushuka chini na hakuna kupingwa!
mwezi umeisha bila baraza la mawaziri, mtu mbili tu zinaendesha nchi magufuli na ombeni tosha kabisa, pale bungeni walivyokuwa wanafanya fujo angelifuta bunge palepale ingekuwa bonge la big up.
umeongea vyema kabisaaaaa!!!u dictator pkus usanii alafu ukiwa unaongoza mapoyoyo basii utawala kunoga kweli!