Kama si uswahiba basi ana kifundo chake maana hakuna Waziri mbovu kama Kamwelwe

mavumbi

JF-Expert Member
Feb 8, 2013
596
326
Ndio hivyo!

MV Nyerere - ajali iliyopoteza maisha ya Watz zaidi ya 100. Ni jambo la kusikitisha na ingawa lawama zikatupwa huku na kule, mwajibikaji mkuu akaachwa, akabaki kuwawajibisha wengine.

Daraja la barabara ya Dar - Dom pale wilayani Kilosa likabomoka na kusababisha adha kubwa kwa wiki nzima. Na Rais alimuuliza sema wewe Mhe Waziri tuanze na wewe, unsemaje? Ni wazi Mhe Rais alitegemea huyu bwana angeanza kuwajibika mwenyewe.

Lakini Mhe Waziri akaishia kusema hadaharani "Mhe Rais, nimekosa, naomba nisamehe!" Bila aibu wala chembe ya kutambua kuwa ana wajibu kwa tukio kama hilo na Dunia nzima ikamsikia.

Baada ya hapo akaonekana kwenye vyombo vya habari akijinadi ati hatasita kumchukulia hatua mtendaji yeyote atakaye onekana ana hitilafu - sawa.

Limekuja hili la barabara ya Lindi Mtwara, mbio kwenye vyombo vya habari 'Natengua huyu na huyu na huyu..."
Hoja ya msingi: kabala rais hajapita huko yeye hakujua hali ikoje?

Anangoja hadi yatokee ndio aonekane yupo?

Ubovu gani huu?

NB. Wallahi sina chuki binafsi!
 
Hata Mh. Mama Kairuki sijawahi kuona alichokifanya kwny hii miaka 5 yake ya uwaziri.

Naongelea Performance kazini.
 
Naam yawezekana ila Tukianza na uwezo wa ufafanuzi wa sera, usimamizi wa sera, usimamizi wa utendaji, na ufahamu wa sekta wanazoziongoza bado naona huyo bwana ana shika mkia
 
Back
Top Bottom