Kuelekea laini za simu zisizosajiliwa kuzimwa; Ushauri wa namna bora ya kufanya ili kutovunja sheria za nchi

idawa

JF-Expert Member
Jan 20, 2012
25,284
38,312
Binafsi nilijiandikisha tena mara mbili lakini nimefuatilia namba zangu NIDA kama naomba mkopo benki. Hakuna nilichoambulia. Uzembe wa NIDA usumbufu nabebeshwa mimi.

Matokeo yake naambiwa nijiandikishe upya, yaani nianze taratibu za kwenda kwa Mtendaji, Uhamiaji halafu NIDA.

---
Mambo ya msingi ya kufanya kabla ya laini kufungwa kama huna namba ya kitambulisho cha NIDA

Kuthibitisha kama laini yako ya simu imesajiliwa kwa alama za vidole piga *106# chagua 1


Kwanza niwape pole wale wote ambao wanashinda ofisi za NIDA bila kufanikiwa.

Ukweli process ya vitambulisho ni ndefu sana.

Kwa wale ambao hawana vitambulisho vya NIDA unaweza tafuta ndugu yako ukasajili kwa kutumia kitambulisho chake, kitambulisho kimoja kinaruhusiwa kusajili laini 10.

Kwa wale ambao hawajasajili hakikisha fedha zote umezitoa na kama umezoea kutumia mobile banking hakikisha kadi yako ya ATM ipo valid otherwise utapata usumbusu mkubwa sana kupanga foleni bank na kupata ATM mpya inachukua more than one week.

Kwa NIDA nashauri watume majina na namba za wananchi ambao wameshajaza form na hawajapata namba zao ili mitandao ya simu (MNO) wasiwafungie kwa sababu hawana hatia.

Nawatakia weekend njema.

------
Waziri Nditiye asema hekima itatumika usajili wa laini kwa wasio na vitambulisho vya Taifa


Serikali ya Tanzania imesema itatumia hekima kuwasaidia wananchi walioshindwa kusajili laini za simu kwa sababu ya kukosa kitambulisho cha Taifa na namba licha ya kuanza mchakato wa kupata kitambulisho hicho.

Imesema wananchi hao taarifa zao zipo katika Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa (Nida), huenda wamekosa kitambulisho au namba kwa sababu zilizo nje ya uwezo wao.

Hayo yameelezwa leo Jumapili Januari 19, 2020 na naibu Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Atashasta Nditiye katika mkutano wa ndani wa CCM mkoani Kigoma.

"Serikali itaona jinsi ya kutumia hekima kwa wananchi ambao taarifa zao zipo katika ofisi za Nida kuona namna ya kufanya lakini kwa wengine ambao hawajajaza fomu laini zao zitazimwa,” amesema Nditiye.

Amesema ambao laini zao zitazimwa ni wale waliosajili laini chache na kuacha nyingine licha ya kuwa na kitambulisho hicho.

Amebainisha kuwa usajili wa laini za simu ni endelevu licha ya baadhi ya wananchi kupuuza.

Chanzo: Mwananchi


---
Dakika chache kutoka sasa simcard zisizosajiliwa zitazimwa

Imebakia robo saa kutimia saa sita kamili ya tarehe 20. January. 2020.. Muda ambao ni kikomo cha mwisho kwa wasiosajiliwa kwa alama za vidole wafanye hivyo la sivyo kuanzia saa sita na dakika moja laini zote ambazo hazijafanya USAJILI WA vidole zitazimwa... Ina maana baada ya hapo laini kwenye simu husika haitafanya kazi tena...

Huu ni mtego wa hatari mno kwa serikali kama haijajipanga vema na tayari kuna baadhi ya wananchi wameshaanza kubeza hiyo hatua kama hili zoezi la kuzima lisipofanyika ama lisipofanikiwa

Kuna machache kwenye mengi ya kujadili hapa...
1. Je serikali imeshafanya upembuzi yakinifu kwenye hili, hasara na faida zake? Je hasara ni zipi na faida ni zipi?

2. Je muda huu mamlaka ya mawasiliano kupitia mitandao husika wako kazini wakisubiri dakika zilizobakia waminye kitufe cha kuzima laini? Je mamlaka kupitia mitandao husika ina uwezo na zana zenye nguvu za kuweza kuzima laini zaidi ya milioni 20 ambazo bado hazijapata usajili?

3. Je hili haliwezi kuchukuliwa kama uhujumu uchumi kutokana na serikali kukosa mapato makubwa ndani ya saa 24 zijazo? Kuanzia miamala ya pesa, manunuzi ya muda wa maongezi, vifurushi vya data nknk?

4. Je serikali haiwezi kushitakiwa kwa uzembe na usumbufu? kwakuwa kama wangetuma watu wao kwenye vituo vya usajili wangeona wananchi wanavyopatishwa tabu kwenye kupata vitambulisho vya taifa kwa ajili ya kupata usajili wa simcard?

5. Dhihaka ni jambo baya sana kwenye mambo muhimu ya KITAIFA.. Lakini mkuu wa mkoa wa DSM katoa dhihaka kwa wale watakaozimiwa simu zao usiku huu kama ni watu waliokuwa na michepuko... Je ana ushahidi na ithibati kwenye hili? Nini maana ya kuwa kiongozi?

Tayari ni saa sita na dakika tatu siku ya tar 21 January 2020... Nadhani muda huu tayari zoezi la kuzima limeshaanza... Likifanikiwa hili kuna madhara mengi yatatokea usiku huu.. Kuna dharura hazitafanyiwa kazi.. Kuna vifo vitatokea kwa kukosa mawasiliano... Kuna watu watakwama kusafiri, kutuma pesa ya dawa, chakula nk kwa kukosa kufanya miamala nknk...

Kuna nafasi bado ya kutafakari kwenye hili... Lakini je serikali iko tayari kujishusha na kukiri wazi kuwa haikutafari vema kwenye hili? Muda utasema kukipambazuka.. Lakini tayari kejeli zimeshaanza
View attachment 1329002

Jr


---UPDATE 21 January, 2020---
TCRA kufungia laini zisizosajiliwa kwa awamu


Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA), James Kilaba amesema uzimaji wa laini za simu ambazo hazijasajiliwa kwa alama za vidole unafanyika kwa awamu

Amesema zoezi hilo lililoanza jana Januari 20, 2020 linafanyika kwa awamu ili kuondoa usumbufu na hadi kufikia jana usiku saa nne walikuwa wamezima laini 975,041

Amesema kundi la kwanza waliozimiwa laini ni watu 656,091 ambao wana Vitambulisho vya Taifa au namba lakini hawajasajili laini zao

Amebainisha kuwa kundi la pili ni watu 318,950 waliosajili laini zao kwa Kitambulisho cha Taifa kabla ya kuanza mfumo wa kusajili kwa alama za kidole

Amesema, “Tunazima kidogo kwa sababu ya mambo ya kitaalamu, hauwezi ukazima laini milioni tano au 10 kwa mara moja kwa maana watajazana kwenye kusajili kitu kinachofanya mifumo ya Nida inaelemewa.”
 
Nilikuwa sina mpango wa kusajili line yangu ya simu ingawa sina sababu ya msingi kabisa NIDA ninayo ile ya mwanzo kabisa ya yule aliyeshitakiwa basi tuu sikuwa nataka usumbufu ila nadhani sasa naweza sajili
 
Nilikuwa sina mpango wa kusajili line yangu ya simu ingawa sina sababu ya msingi kabisa NIDA ninayo ile ya mwanzo kabisa ya yule aliyeshitakiwa basi tuu sikuwa nataka usumbufu ila nadhani sasa naweza sajili
Wewe unaweza kuwapigia wale wanaosajili line mtaani wakakusajilia hata Nyumbani kwako, hongera umeyapatia Maisha.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Wewe unaweza kuwapigia wale wanaosajili line mtaani wakakusajilia hata Nyumbani kwako, hongera umeyapatia Maisha.

Sent using Jamii Forums mobile app


Yaani nimecheka kwa sauti ya juu hapo kwenye kupatia maisha ... Mkuu bado sema mimi kipindi kile cha kujiandikisha NIDA sikuukataa wito nilifanya hivyo kwa siku tatu mfululizo mpk kuja kufikia sehemu ya kupiga picha nakumbuka nikaenda halafu nikachana na hiyo biashara nikaja kutumiwa msg sijui baada ya miezi zaidi ya minne nikafuata kitambulisho.


Mimi huwa sina tabia ya kupuuzia mambo huwa nasema ngoja nifanye ikae hapo huwezi jua....
 
NIDA kumekuwa na folen ya kufa mtu sio kwa kuwa watu wanataka vitambulisho vya Taifa bali kwa kuwa wanapigania namba zao za simu zisizimwe

Yaan watu hawana mpango na vitambulisho sema tu inabidi wawe nacho kukamilisha usajili

I.e line ya simu ni muhimu kuliko kitambulisho
ikitangazwa kuwa usajili wa line sio muhimu kitambulisho cha NIDA basi folen inaisha fasta
 
Poleni sana mtakaozimiwa line! Ni muhimu kufanya jambo kwa wakati sahihi na kwa muda sahihi si vizuri Sana kila Jambo ufanye dakika za mwisho/dakika za lala salama.

Usikate tamaa bado muda upo na usiruhusu hali ya kuupuza vitu, uvivu au uzembe ukutawale.
 
Binafsi nilijiandikisha tena mara mbili lakini nimefuatilia namba zangu NIDA kama naomba mkopo benki. Hakuna nilichoambulia. Uzembe wa NIDA usumbufu nabebeshwa mimi.

Matokeo yake naambiwa nijiandikishe upya, yaani nianze taratibu za kwenda kwa Mtendaji, Uhamiaji halafu NIDA.

Acha wafungie nimejiandaa kisaikolojia!

Sent using Jamii Forums mobile app
Kajiongeze kwa wale mawakala watakufanyia mchakato
 
Binafsi nilijiandikisha tena mara mbili lakini nimefuatilia namba zangu NIDA kama naomba mkopo benki. Hakuna nilichoambulia. Uzembe wa NIDA usumbufu nabebeshwa mimi.

Matokeo yake naambiwa nijiandikishe upya, yaani nianze taratibu za kwenda kwa Mtendaji, Uhamiaji halafu NIDA.

Acha wafungie nimejiandaa kisaikolojia!

Sent using Jamii Forums mobile app
Poleni third world dwellers yani mnatawaliwa na misomi uchwara yenye PhD uchwara
 
Kisaikolojia fanya haya. Kama una smartphone utaendelea na internet kwa wi fi ya mtu mwingine karib. Utaacha aina zote za mikopo ya mitandaon. Utafanya mawasiliano ya kupiga kwa internet tu bila line kwenye whasapp, viber etc. Utarudia mifumo ya kibenk kuhusu pesa hasa huduma ya cardless. Mwisho wa yote utaambulia usumbuf kias lakin kampun zitapoteza makato meng yanayokuhusu na serkali itapoteza mapato ya kodi.
 
Back
Top Bottom