Hapo sawa naanza kukuelewa.Umeongea jambo la msingi sana. Kuna vijiji vingi sana - na hata wilaya, ambazo zina vyanzo vizuri vya maji na kuwapa access ya maji wala isingekuwa tatizo, lakini hatufanyi hilo.
Juzi juzi hapa nilipewa taarifa za ngazi za wilaya ambazo watu wanashindwa kuelewa ni jinsi gani serikali imeshindwa kubororesha huduma za maji na ilionekana ni sababu ya uzembe tu wa kiuongozi. Ilitokea mradi mkubwa wa maji kanda ya ziwa uliofanikiwa kwa mabilioni ya fedha kulinganishwa na huduma ya naji wilaya ya Rungwe (Tukuyu). Engineer mmoja alita taarifa kwamba ni uzembe tu Rungwe hawana maji kwa kuwa ni wilaya mojawapo Tanzania ambazo unahitaji kuwekeza vitu viwili ili wapate maji - tanki na mambomba, na akasema hii ni kwa sababu vyazno vya maji viko mlimani kwa hiyo huhitaji pampu wala umeme kuwapatia maji. Angalia kwamba Rungwe ndiko alikotoka Prof Mwandosaya alikuwa Waziri wa Maji na ndiko anatoka Tulia naibu spika wa sasa - lakini bado wanachi wake wanapata shida ya maji hadi ngazi ya wilayani mjini. Sembuse huko kwingine!
Kuna sehemu nyingi Tanzania unaweza kusambaza maji kwa gravity na hii haitahitaji fedha nyingi, lakini hilo halifanyiki kwa ajili ya uzembe tu!