Kama RC Mnyeti anatuhumiwa kwa rushwa basi Mhe. Mbowe na Kamati Kuu ya CHADEMA nao wana kesi ya kujibu

kipande

JF-Expert Member
Dec 29, 2010
2,136
1,317
Wasalaam Wana Jamii,

Nimefuatilia mijadala mingi kwenye hii forum na kuona watu wengi wakilaumu juu ya Uteuzi wa Mhe. Mnyeti kuwa RC - Manyara kwasababu eti anatuhumiwa (haijathibitika) kutoa rushwa kwa madiwani wa CDM ili wakihame chao na hivyo hakustahili kuteuliwa.Dhana hii imejengwa juu ya ushahidi uliowasilishwa TAKUKURU na Mhe. Nassari.

Baada ya kutafakari kwa kina, nimeona kimsingi walichofanya kina nassari dhidi ya mnyeti ni siasa na lengo lilikua ni kurudisha imani ya wananchi kwa chama chao ionekane madiwani hawakuhama kwa hiari yao au kwasababu walizotoa bali ni kwa kununuliwa/tamaa ya fedha. Well, hata kama ilifanyika hivyo nijuavyo mimi siasa ni maslahi (cheo, fedha n.k) hakuna mwanasiasa (hasa walio kwenye uongozi au wenye ushawishi mkubwa katika jamii) ambae ameshawahi kuhama chama chake kwenda kingine bila kufuata maslahi niliyoyataja na kabla ya kuhama ni lazima mazungumzo yafanyike kwenye chama anachohamia ili kujihakikishia kwamba maslahi yake yanazingatiwa.

Kuthibitisha haya, nitolee mfano kwa kujikumbusha wakati Bw.Lowassa anahamia CDM kutoka CCM. Kabla ya kuhama, yalifanyika mazungumzo ambayo mengine yalikua ya siri na mengine yalifanyika wazi ingawa hayakua public (yale yaliyofanyika bahari beach) lengo la mazungumzo yale pamoja na mambo mengine ilikua ni kumhakikishia Bw. Lowassa kwamba atakapohamia CDM basi atapewa nafasi ya kuwa mgombea urais na ikawa hivyo, japokua CDM ilikua tayari imeshakamilisha mchakato wa kumchagua mgombea urais wake na ilikua imebakia kuafikiana na UKAWA na kisha kumtangaza (rejea maelezo ya Dk.Slaa wakati anang'atuka CDM na ujio wa Lowassa).

Sasa tunapozungumzia rushwa kwa tafsiri isiyo rasmi ni kitu chochote mtu anachotoa kwa lengo la kupata kitu fulani kwa njia isiyo halali. Sasa swali la kujiuliza hapa ni ipi 'njia isiyo halali' hususan kwenye siasa. Je, kumpa ahadi mwanasiasa kwa kuzingatia maslahi yake ya kisiasa (fedha, cheo n.k) ili ahamie kwenye chama chako ni njia isiyo halali? kama tunakubaliana kwamba njia hii siyo halali basi tukubaliane pia kwamba hata Lowassa alihamia CDM kwa njia isiyo halali kwasababu alihama kwa lengo la kupata cheo/ nafasi ya kugombea u Rais aliyoahidiwa (vinginevyo asingehama). halikadhalika, kama tunaamini kwamba DC Mnyeti (sasa RC) kitendo chake cha kufanya mazungumzo na madiwani waliohama CDM na kutoa ahadi ili wahame chama chao ni kosa ambalo linahusiana na rushwa basi hata Kamati Kuu ya CDM, Mhe.Mbowe na washirika wao waliofanikisha lowassa kuhama CCM basi inabidi na wao washitakiwe kwa kosa hilo hilo la rushwa ya kumshawishi Lowassa ahamie kwenye chama chao ili apewe nafasi ya kugombea rais. Otherwise, kama tunasema njia iliyotumika kumshawishi Lowassa kuhamia CDM ilikua halali basi tuseme pia njia iliyotumika kuwashawishi madiwani ni halali.

Hivyo, Mhe. Mnyeti hakufanya kosa lolote na wala hatupaswi kuwashurutisha TAKUKURU kuchukua hatua dhidi yake kwa sababu ile haikua RUSHWA bali ni USHAWISHI uliozingatia maslahi ya kisiasa. Na kwa maana hiyo Mhe.Rais hakukosea kumteua kada mtiifu aliefanya kazi yake kwa uadilifu na werevu Mhe. Alexander Mnyeti kuwa RC mpya - Mkoa Manyara.

Naomba kuwasilisha.
 
Unajua wakati mwingne inafikia wakati unasema UJINGA BHASI...kama ni kweli HAWA MADIWANI WAMEPEWA PESA KUHAMA CHADEMA kwa upande wangu nawaona wapo sahihi sana(huku ndio kunaitwa pambana na hali yako)..wamesoma mchezo wakagundua kabsa wao wanatumika kijinga sana na BAADHI YA VIONGOZI NDANI YA CHADEMA...kama mbowe na baadhi ya VIONGOZI WAANDAMIZI WA CHADEMA Waliweza kuhongwa pesa na EL Wamsimamie KIDETE awe mgombea URAIS kupitia CHADEMA na mbowe kufaidika kwenye hili na hao mazuzu wenzake kama kina MSIGWA sasa iweje hawa MADIWANI wao wakatae kuhongwa na CCM.....WANGEKUWA WAPUUZI wa KARNE....
Na hiki ni kithibitisho kingne JINSI hiki CHAMA kilivyo cha AJABU kweli....WATANZANIA tusijidanganye kabsa KUWAPA NCHI hawa....WATATUUZA ASUBUHI NA MAPEMA...wameonekana ni WATU RAHISI SANA KUDANGANYIKA
Ntashangaa baadhi ya WAPUUZI humu ndani MKATAE ETI VIONGOZI WAKUU NDANI YA CHADEMA hawakuvuta chochote kwa NYEUPE.....hii si kweli kabsa hata nafsi zetu lazima zitakuwa zinatusuta sana....hawa jamaa pesa walivuta kufunga midomo sasa acheni na hawa madiwani wafaidike kama ni kweli
 
Kuna mambo, ukimya unatosha kukuonyesha ulivyo mwerevu. Mwezetu kwakuwa ni kada wa CCM, unaweza kuandika chochote. Wengine hata tukijadili tu, tutaitwa wachochezi. Busara zinanituma kutoandika chochote katika kujadili jambo lako. Tuache tuendelee kufanya tafakuri kwa yote yaliyotokea na yanayoendelea kutokea.
 
Wasalaam Wana Jamii,

Nimefuatilia mijadala mingi kwenye hii forum na kuona watu wengi wakilaumu juu ya Uteuzi wa Mhe. Mnyeti kuwa RC - Manyara kwasababu eti anatuhumiwa (haijathibitika) kutoa rushwa kwa madiwani wa CDM ili wakihame chao na hivyo hakustahili kuteuliwa.Dhana hii imejengwa juu ya ushahidi uliowasilishwa TAKUKURU na Mhe. Nassari.

Baada ya kutafakari kwa kina, nimeona kimsingi walichofanya kina nassari dhidi ya mnyeti ni siasa na lengo lilikua ni kurudisha imani ya wananchi kwa chama chao ionekane madiwani hawakuhama kwa hiari yao au kwasababu walizotoa bali ni kwa kununuliwa/tamaa ya fedha. Well, hata kama ilifanyika hivyo nijuavyo mimi siasa ni maslahi (cheo, fedha n.k) hakuna mwanasiasa (hasa walio kwenye uongozi au wenye ushawishi mkubwa katika jamii) ambae ameshawahi kuhama chama chake kwenda kingine bila kufuata maslahi niliyoyataja na kabla ya kuhama ni lazima mazungumzo yafanyike kwenye chama anachohamia ili kujihakikishia kwamba maslahi yake yanazingatiwa.

Kuthibitisha haya, nitolee mfano kwa kujikumbusha wakati Bw.Lowassa anahamia CDM kutoka CCM. Kabla ya kuhama, yalifanyika mazungumzo ambayo mengine yalikua ya siri na mengine yalifanyika wazi ingawa hayakua public (yale yaliyofanyika bahari beach) lengo la mazungumzo yale pamoja na mambo mengine ilikua ni kumhakikishia Bw. Lowassa kwamba atakapohamia CDM basi atapewa nafasi ya kuwa mgombea urais na ikawa hivyo, japokua CDM ilikua tayari imeshakamilisha mchakato wa kumchagua mgombea urais wake na ilikua imebakia kuafikiana na UKAWA na kisha kumtangaza (rejea maelezo ya Dk.Slaa wakati anang'atuka CDM na ujio wa Lowassa).

Sasa tunapozungumzia rushwa kwa tafsiri isiyo rasmi ni kitu chochote mtu anachotoa kwa lengo la kupata kitu fulani kwa njia isiyo halali. Sasa swali la kujiuliza hapa ni ipi 'njia isiyo halali' hususan kwenye siasa. Je, kumpa ahadi mwanasiasa kwa kuzingatia maslahi yake ya kisiasa (fedha, cheo n.k) ili ahamie kwenye chama chako ni njia isiyo halali? kama tunakubaliana kwamba njia hii siyo halali basi tukubaliane pia kwamba hata Lowassa alihamia CDM kwa njia isiyo halali kwasababu alihama kwa lengo la kupata cheo/ nafasi ya kugombea u Rais aliyoahidiwa (vinginevyo asingehama). halikadhalika, kama tunaamini kwamba DC Mnyeti (sasa RC) kitendo chake cha kufanya mazungumzo na madiwani waliohama CDM na kutoa ahadi ili wahame chama chao ni kosa ambalo linahusiana na rushwa basi hata Kamati Kuu ya CDM, Mhe.Mbowe na washirika wao waliofanikisha lowassa kuhama CCM basi inabidi na wao washitakiwe kwa kosa hilo hilo la rushwa ya kumshawishi Lowassa ahamie kwenye chama chao ili apewe nafasi ya kugombea rais. Otherwise, kama tunasema njia iliyotumika kumshawishi Lowassa kuhamia CDM ilikua halali basi tuseme pia njia iliyotumika kuwashawishi madiwani ni halali.

Hivyo, Mhe. Mnyeti hakufanya kosa lolote na wala hatupaswi kuwashurutisha TAKUKURU kuchukua hatua dhidi yake kwa sababu ile haikua RUSHWA bali ni USHAWISHI uliozingatia maslahi ya kisiasa. Na kwa maana hiyo Mhe.Rais hakukosea kumteua kada mtiifu aliefanya kazi yake kwa uadilifu na werevu Mhe. Alexander Mnyeti kuwa RC mpya - Mkoa Manyara.

Naomba kuwasilisha.
in other words una maana wenyeviti wa taifa wa vyama vyote viwili (Chadema & CCM) wote ni watoa rushwa.

Watanzania hatuna shida.... tunaamini katika dhana ya "two wrongs don't make it right", kwa hiyo TAKUKURU iwashughulikie wote hawa wawili haraka sana!
 
Wasalaam Wana Jamii,

Nimefuatilia mijadala mingi kwenye hii forum na kuona watu wengi wakilaumu juu ya Uteuzi wa Mhe. Mnyeti kuwa RC - Manyara kwasababu eti anatuhumiwa (haijathibitika) kutoa rushwa kwa madiwani wa CDM ili wakihame chao na hivyo hakustahili kuteuliwa.Dhana hii imejengwa juu ya ushahidi uliowasilishwa TAKUKURU na Mhe. Nassari.

Baada ya kutafakari kwa kina, nimeona kimsingi walichofanya kina nassari dhidi ya mnyeti ni siasa na lengo lilikua ni kurudisha imani ya wananchi kwa chama chao ionekane madiwani hawakuhama kwa hiari yao au kwasababu walizotoa bali ni kwa kununuliwa/tamaa ya fedha. Well, hata kama ilifanyika hivyo nijuavyo mimi siasa ni maslahi (cheo, fedha n.k) hakuna mwanasiasa (hasa walio kwenye uongozi au wenye ushawishi mkubwa katika jamii) ambae ameshawahi kuhama chama chake kwenda kingine bila kufuata maslahi niliyoyataja na kabla ya kuhama ni lazima mazungumzo yafanyike kwenye chama anachohamia ili kujihakikishia kwamba maslahi yake yanazingatiwa.

Kuthibitisha haya, nitolee mfano kwa kujikumbusha wakati Bw.Lowassa anahamia CDM kutoka CCM. Kabla ya kuhama, yalifanyika mazungumzo ambayo mengine yalikua ya siri na mengine yalifanyika wazi ingawa hayakua public (yale yaliyofanyika bahari beach) lengo la mazungumzo yale pamoja na mambo mengine ilikua ni kumhakikishia Bw. Lowassa kwamba atakapohamia CDM basi atapewa nafasi ya kuwa mgombea urais na ikawa hivyo, japokua CDM ilikua tayari imeshakamilisha mchakato wa kumchagua mgombea urais wake na ilikua imebakia kuafikiana na UKAWA na kisha kumtangaza (rejea maelezo ya Dk.Slaa wakati anang'atuka CDM na ujio wa Lowassa).

Sasa tunapozungumzia rushwa kwa tafsiri isiyo rasmi ni kitu chochote mtu anachotoa kwa lengo la kupata kitu fulani kwa njia isiyo halali. Sasa swali la kujiuliza hapa ni ipi 'njia isiyo halali' hususan kwenye siasa. Je, kumpa ahadi mwanasiasa kwa kuzingatia maslahi yake ya kisiasa (fedha, cheo n.k) ili ahamie kwenye chama chako ni njia isiyo halali? kama tunakubaliana kwamba njia hii siyo halali basi tukubaliane pia kwamba hata Lowassa alihamia CDM kwa njia isiyo halali kwasababu alihama kwa lengo la kupata cheo/ nafasi ya kugombea u Rais aliyoahidiwa (vinginevyo asingehama). halikadhalika, kama tunaamini kwamba DC Mnyeti (sasa RC) kitendo chake cha kufanya mazungumzo na madiwani waliohama CDM na kutoa ahadi ili wahame chama chao ni kosa ambalo linahusiana na rushwa basi hata Kamati Kuu ya CDM, Mhe.Mbowe na washirika wao waliofanikisha lowassa kuhama CCM basi inabidi na wao washitakiwe kwa kosa hilo hilo la rushwa ya kumshawishi Lowassa ahamie kwenye chama chao ili apewe nafasi ya kugombea rais. Otherwise, kama tunasema njia iliyotumika kumshawishi Lowassa kuhamia CDM ilikua halali basi tuseme pia njia iliyotumika kuwashawishi madiwani ni halali.

Hivyo, Mhe. Mnyeti hakufanya kosa lolote na wala hatupaswi kuwashurutisha TAKUKURU kuchukua hatua dhidi yake kwa sababu ile haikua RUSHWA bali ni USHAWISHI uliozingatia maslahi ya kisiasa. Na kwa maana hiyo Mhe.Rais hakukosea kumteua kada mtiifu aliefanya kazi yake kwa uadilifu na werevu Mhe. Alexander Mnyeti kuwa RC mpya - Mkoa Manyara.

Naomba kuwasilisha.

Unahitaji kupewa pole tu
 
  • Thanks
Reactions: BAK
in other words una maana wenyeviti wote wawili... wa Chadema na CCM wote ni watoa rushwa.

Watanzania hatuna shida.... tunaamini katika dhana ya "two wrongs don't make it right", kwa hiyo TAKUKURU iwashughulikie wote hawa wawili haraka sana!

Takukuru isiyo na meno itamshughulikia Mbowe na Kumuacha aliyesababisha hasara ya KIVUKO KIBOVU
 
Unajua wakati mwingne inafikia wakati unasema UJINGA BHASI...kama ni kweli HAWA MADIWANI WAPEWA PESA KUHAMA CHADEMA kwa upande wangu nawaona wapo sahihi sana

Kwa sababu kwako RUSHWA iko kwenye damu yako
 
Huna haja yakujibishana na wapuuzi
nikuwaacha waongee wata jidharau wenyewe,
Mnyeti watake wasitake ndio RC wao
nchi haiongozwi kwa matakwa yao
watu hawa hawana jema,Hawana Zuri wala Baya
Kila jambo kwao sio kutwa udaku na kushindwa kufanya kazi.
 
Tegemea Matusi,Kejeli na dharau kutoka kwa makamanda wadeki Lami na wazungusha mikono
mbowe.jpg
 
  • Thanks
Reactions: UCD
Yaani brainwashed ni ujinga na huu ujinga wa mtoa mada ni hatari sana.
Hebu mtoa mada leta sehemu yoyote ambayo pesa ya umma àmbayo mbowe au Lowassa waliyotumia ktk mipango yao.
Onyesha ni wapi mbowe na Lowassa walitumia ofisi za umma ktk hilo jambo
Onyesha ni wapi Lowassa na mbowe alitumia Mali ya umma ktk kufanikisha jambo hilo.
Jitu linatumia Mali, ofisi, na fedha za umma na bado majitu brainwashed, yasiyojielewa yanakuja na mada mfu kama hizi
 
Yani hapo ndo umefikira mpaka mwisho. Wana Lumumba lazima wajitoe ufahamu ndo waweze kuja na hoja nyepesi kama hizi
 
Mbona kama mnatumia nguvu nyingi sana kujustfy uteuzi wa huyu mtu! Kuna nini?
 
Yaani brainwashed ni ujinga na huu ujinga wa mtoa mada ni hatari sana.
Hebu mtoa mada leta sehemu yoyote ambayo pesa ya umma àmbayo mbowe au Lowassa waliyotumia ktk mipango yao.
Onyesha ni wapi mbowe na Lowassa walitumia ofisi za umma ktk hilo jambo
Onyesha ni wapi Lowassa na mbowe alitumia Mali ya umma ktk kufanikisha jambo hilo.
Jitu linatumia Mali, ofisi, na fedha za umma na bado majitu brainwashed, yasiyojielewa yanakuja na mada mfu kama hizi
kwa maana hiyo... kwa tafsiri yako rushwa ni ile inayotolewa kwa kutumia fedha ya umma. ila ukitumia fedha nyingine kutoa rushwa haiesabiki kma ni rushwa. sijui unauona huu ujinga ulioandika. inabidi uombeww
 
  • Thanks
Reactions: UCD
Back
Top Bottom