Synthesizer
JF-Expert Member
- Feb 15, 2010
- 11,023
- 18,563
Nasikia uchungu sana kwa nchi yangu Tanzania.
Imefikia mahali hata kama hujihusushi na mambo ya siasa, utaudhiwa na hujuma za wazi wazi zinazofanywa na serikali dhidi ya vyama vya upinzani nchini, nikiamini hujuma hizi zikiwa ni kwa shinikizo la CCM na hata kuchochewa na Raisi Magufuli mwenyewe.
Raisi Magufuli, kama alivyodai yeye mwenyewe, hawezi kukwepa kuwa raisi wa Watanzania wote, walio CCM, walio upinzani na hata wale wasio jihusisha na siasa. Kila mtu anajua kwamba kuna wakati Raisi Magufuli amefikia kutoa kauli zinaonyesha kwamba anaona mtu yeyote aliye kwenye chama cha upinzani kuwa adui.
Watanzania tunashuhudia kila siku hali ya "mpambano" ambao uko nje kabisa ya hali ya kawaida ya upinzani wa kisiasa, kati ya CCM na vyama vya upinzani. Kwa kuwa CCM ndio chama kilichoko madarakani, ni wazi kabisa mara nyingi "mpambano" huu huzaa hali ya kuonewa na kunyanyaswa kwa wale walio vyama vya upinzani. Hili hutokea ndani na nje ya Bunge, na hata katika nyanja za Majiji, Halmashauri na serikali za mitaa kwa ujumla. Na mbaya zaidi, vyombo vyetu vya usalama, pamoja na TISS na Polisi, wamekuwa wakiingizwa katika mpambano huu na kuharibu kabisa uhusiano wao na raia. Wakati fulani hata kumekuwa na jitihada za kujaribu kuwaingiza JWTZ.
Hali hii haipendezi kabisa kwa nchi yetu, na inatia aibu na kinyaa kuona watu wa uongozi wa juu hata ngazi ya raisi wakifanya kila wawezalo kuhujumu vyama vya upinzani.
Na tuseme wazi basi, kama Raisi Magufuli na CCM kwa ujumla wanaona kwamba kwa sasa hali ya vyama vingi vya siasa haifai kwa nchi yetu, basi waliweke hili wazi, ili tuamue na ikibidi kufanya referandum kuamua kuondoa mfumo wa vyama vingi na kurudi kwenye mfumo wa chama kimoja au la.
Tupo wengi ambao ukweli ni kwamba tungependa kuona nguvu za viongozi shupavu na makini walioko CCM na vyama vya upinzani kama CHADEMA, CUF, ACT, NCCR nk zikiunganishwa ili kuendeleza nchi yetu. Sasa kama hili haliwezekani chini ya mfumo wa vyama vingi, basi ni bora tutafakari upya kama ni bora kurudi kwenye mfumo wa chama kimoja na kuwa nguvu moja.
Imefikia mahali hata kama hujihusushi na mambo ya siasa, utaudhiwa na hujuma za wazi wazi zinazofanywa na serikali dhidi ya vyama vya upinzani nchini, nikiamini hujuma hizi zikiwa ni kwa shinikizo la CCM na hata kuchochewa na Raisi Magufuli mwenyewe.
Raisi Magufuli, kama alivyodai yeye mwenyewe, hawezi kukwepa kuwa raisi wa Watanzania wote, walio CCM, walio upinzani na hata wale wasio jihusisha na siasa. Kila mtu anajua kwamba kuna wakati Raisi Magufuli amefikia kutoa kauli zinaonyesha kwamba anaona mtu yeyote aliye kwenye chama cha upinzani kuwa adui.
Watanzania tunashuhudia kila siku hali ya "mpambano" ambao uko nje kabisa ya hali ya kawaida ya upinzani wa kisiasa, kati ya CCM na vyama vya upinzani. Kwa kuwa CCM ndio chama kilichoko madarakani, ni wazi kabisa mara nyingi "mpambano" huu huzaa hali ya kuonewa na kunyanyaswa kwa wale walio vyama vya upinzani. Hili hutokea ndani na nje ya Bunge, na hata katika nyanja za Majiji, Halmashauri na serikali za mitaa kwa ujumla. Na mbaya zaidi, vyombo vyetu vya usalama, pamoja na TISS na Polisi, wamekuwa wakiingizwa katika mpambano huu na kuharibu kabisa uhusiano wao na raia. Wakati fulani hata kumekuwa na jitihada za kujaribu kuwaingiza JWTZ.
Hali hii haipendezi kabisa kwa nchi yetu, na inatia aibu na kinyaa kuona watu wa uongozi wa juu hata ngazi ya raisi wakifanya kila wawezalo kuhujumu vyama vya upinzani.
Na tuseme wazi basi, kama Raisi Magufuli na CCM kwa ujumla wanaona kwamba kwa sasa hali ya vyama vingi vya siasa haifai kwa nchi yetu, basi waliweke hili wazi, ili tuamue na ikibidi kufanya referandum kuamua kuondoa mfumo wa vyama vingi na kurudi kwenye mfumo wa chama kimoja au la.
Tupo wengi ambao ukweli ni kwamba tungependa kuona nguvu za viongozi shupavu na makini walioko CCM na vyama vya upinzani kama CHADEMA, CUF, ACT, NCCR nk zikiunganishwa ili kuendeleza nchi yetu. Sasa kama hili haliwezekani chini ya mfumo wa vyama vingi, basi ni bora tutafakari upya kama ni bora kurudi kwenye mfumo wa chama kimoja na kuwa nguvu moja.