Kama Rais Samia ameweza kufanya kwa Wakuu wa Mkoa, kwanini hakufanya kwa Mawaziri?

MsemajiUkweli

JF-Expert Member
Jul 5, 2012
13,172
23,975
Nilishangaa kidogo kusoma Press Release ya Ikulu ambayo ilitangaza majina ya Wakuu wa Mikoa ''wapya'' ambao WAMETEULIWA na Rais Samia. Kilichonishangaza ni lugha iliyotumika lakini ''kiuhalisia'' kilichofanyika ni UHAMISHO TU wa Wakuu wa Mikoa na kuziba nafasi za wale wamestaafu.

Rais Samia alichofanya ni kuhamisha hao Wakuu wa Mikoa kitu ambacho ni kizuri kiutendaji lakini pia ni kibaya kwa matumizi ya fedha na muda. Hawa Wakuu wa Mikoa itabidi walipwe pesa za Uhamisho lakini pia itawachukua muda kuyazoea mazingira kikazi ya sehemu waliyohamishwa.

Sasa kama ameweza kufanya hivi kwa Wakuu wote wa Mikoa, Kwa nini hakufanya hivyo kwa Waziri Mkuu na Mawaziri ili ionekane hii ni serikali yake ya Awamu ya Sita na sio Serikali ya Awamu ya tano yenye Rais wa Sita!

Rais Samia alitakiwa apendekeze Jina la Waziri Mkuu hata kama ni yule yule (Majaliwa) na likapigiwe kura bungeni kama Katiba inavyosema, halafu baadaye aunde baraza lake la Mawaziri hata kama ni wale wale halafu awaapishe kama atakavyofanya kwa Wakuu wa Mikoa.

Kwa sasa kila mara serikali inapofanya makosa, lawama wanatupiwa mawaziri ambao wanadaiwa niwa ''Rais Magufuli'' na wanafanya kazi kwa kutumia ''mentality'' ya Rais Magufuli kwa sababu hawakuteuliwa na Rais Samia. Kama angefanya kama alivyofanya kwa Wakuu wa Mikoa, hizi lawama zisingeendelea kuwepo!

Je, Rais Samia aliogopa nini kufanya kama alivyofanya kwa Wakuu wa Mikoa ''wapya''?
 
Kipindi cha jiwe ulikuwa huulizi maswali critical namna hii, wewe ulikuwa ni mzee wa mapambio na kuunga mkono kila afanyalo jiwe. Nini kimekukumba?
Ninashukuru sana kuwa na watu wanaonifatilia kama wewe! Yaani unajua kila hoja niliyoweka wakati wa kipindi cha ''jiwe''! Yaani mpaka ninashtuka!

Kwangu haya sio maswali critical bali ni maswali ya kawaida sana labda kama uwezo wako ni mdogo ndio maana utaona ni critical!
 
Nilishangaa kidogo kusoma Press Release ya Ikulu ambayo ilitangaza majina ya Wakuu wa Mikoa ''wapya'' ambao WAMETEULIWA na Rais Samia. Kilichonishangaza ni lugha iliyotumika lakini ''kiuhalisia'' kilichofanyika ni UHAMISHO TU wa Wakuu wa Mikoa na kuziba nafasi za wale wamestaafu.

Rais Samia alichofanya ni kuhamisha hao Wakuu wa Mikoa kitu ambacho ni kizuri kiutendaji lakini pia ni kibaya kwa matumizi ya fedha na muda. Hawa Wakuu wa Mikoa itabidi walipwe pesa za Uhamisho lakini pia itawachukua muda kuyazoea mazingira kikazi ya sehemu waliyohamishwa.

Sasa kama ameweza kufanya hivi kwa Wakuu wote wa Mikoa, Kwa nini hakufanya hivyo kwa Waziri Mkuu na Mawaziri ili ionekane hii ni serikali yake ya Awamu ya Sita na sio Serikali ya Awamu ya tano yenye Rais wa Sita!

Rais Samia alitakiwa apendekeze Jina la Waziri Mkuu hata kama ni yule yule (Majaliwa) na likapigiwe kura bungeni kama Katiba inavyosema, halafu baadaye aunde baraza lake la Mawaziri hata kama ni wale wale halafu awaapishe kama atakavyofanya kwa Wakuu wa Mikoa.

Kwa sasa kila mara serikali inapofanya makosa, lawama wanatupiwa mawaziri ambao wanadaiwa niwa ''Rais Magufuli'' na wanafanya kazi kwa kutumia ''mentality'' ya Rais Magufuli kwa sababu hawakuteuliwa na Rais Samia. Kama angefanya kama alivyofanya kwa Wakuu wa Mikoa, hizi lawama zisingeendelea kuwepo!

Je, Rais Samia aliogopa nini kufanya kama alivyofanya kwa Wakuu wa Mikoa ''wapya''?
Pole kwa msiba wa Meko..
Nchi imetulia sasa baada ya huyu mwendawazimu wenu kufa.
 
Nilishangaa kidogo kusoma Press Release ya Ikulu ambayo ilitangaza majina ya Wakuu wa Mikoa ''wapya'' ambao WAMETEULIWA na Rais Samia. Kilichonishangaza ni lugha iliyotumika lakini ''kiuhalisia'' kilichofanyika ni UHAMISHO TU wa Wakuu wa Mikoa na kuziba nafasi za wale wamestaafu.

Rais Samia alichofanya ni kuhamisha hao Wakuu wa Mikoa kitu ambacho ni kizuri kiutendaji lakini pia ni kibaya kwa matumizi ya fedha na muda. Hawa Wakuu wa Mikoa itabidi walipwe pesa za Uhamisho lakini pia itawachukua muda kuyazoea mazingira kikazi ya sehemu waliyohamishwa.

Sasa kama ameweza kufanya hivi kwa Wakuu wote wa Mikoa, Kwa nini hakufanya hivyo kwa Waziri Mkuu na Mawaziri ili ionekane hii ni serikali yake ya Awamu ya Sita na sio Serikali ya Awamu ya tano yenye Rais wa Sita!

Rais Samia alitakiwa apendekeze Jina la Waziri Mkuu hata kama ni yule yule (Majaliwa) na likapigiwe kura bungeni kama Katiba inavyosema, halafu baadaye aunde baraza lake la Mawaziri hata kama ni wale wale halafu awaapishe kama atakavyofanya kwa Wakuu wa Mikoa.

Kwa sasa kila mara serikali inapofanya makosa, lawama wanatupiwa mawaziri ambao wanadaiwa niwa ''Rais Magufuli'' na wanafanya kazi kwa kutumia ''mentality'' ya Rais Magufuli kwa sababu hawakuteuliwa na Rais Samia. Kama angefanya kama alivyofanya kwa Wakuu wa Mikoa, hizi lawama zisingeendelea kuwepo!

Je, Rais Samia aliogopa nini kufanya kama alivyofanya kwa Wakuu wa Mikoa ''wapya''?

Alishasema anaendeleza waliyokua wameanza na JPM, na kuboresha pale panapohitaji maboresho kwani hukumuelewa?
Alichokifanya ni sawa na kile JPM alichokifanya kwake na PM na wengine November 2020. Kazi kwao waliopewa dhamana kutetea vibarua vyao.... wakizingua watazinguliwa tuu
 
Ninashukuru sana kuwa na watu wanaonifatilia kama wewe! Yaani unajua kila hoja niliyoweka wakati wa kipindi cha ''jiwe''! Yaani mpaka ninashtuka!

Kwangu haya sio maswali critical bali ni maswali ya kawaida sana labda kama uwezo wako ni mdogo ndio maana utaona ni critical!
Kusoma threads zinazoandikwa humu ni kufuatilia mtu? Hujui hii ni public forum? So kila mtu akianzisha thread humu and nikisoma basi namfuatialia huyo mtu? May be uwezo wangu ni mdogo mzee, maana sijui kipimo cha uwezo mdogo wala mkubwa
 
Pole kwa msiba wa Meko..
Nchi imetulia sasa baada ya huyu mwendawazimu wenu kufa.
Asante kwa kunipa pole!
Sina shaka huko mbele ya safari utaimba tena nyimbo zinazofanana zinazosema ''nchi inayumba'' labda kama huzijui siasa za Tanzania!
 
Nilishangaa kidogo kusoma Press Release ya Ikulu ambayo ilitangaza majina ya Wakuu wa Mikoa ''wapya'' ambao WAMETEULIWA na Rais Samia. Kilichonishangaza ni lugha iliyotumika lakini ''kiuhalisia'' kilichofanyika ni UHAMISHO TU wa Wakuu wa Mikoa na kuziba nafasi za wale wamestaafu.

Rais Samia alichofanya ni kuhamisha hao Wakuu wa Mikoa kitu ambacho ni kizuri kiutendaji lakini pia ni kibaya kwa matumizi ya fedha na muda. Hawa Wakuu wa Mikoa itabidi walipwe pesa za Uhamisho lakini pia itawachukua muda kuyazoea mazingira kikazi ya sehemu waliyohamishwa.

Sasa kama ameweza kufanya hivi kwa Wakuu wote wa Mikoa, Kwa nini hakufanya hivyo kwa Waziri Mkuu na Mawaziri ili ionekane hii ni serikali yake ya Awamu ya Sita na sio Serikali ya Awamu ya tano yenye Rais wa Sita!

Rais Samia alitakiwa apendekeze Jina la Waziri Mkuu hata kama ni yule yule (Majaliwa) na likapigiwe kura bungeni kama Katiba inavyosema, halafu baadaye aunde baraza lake la Mawaziri hata kama ni wale wale halafu awaapishe kama atakavyofanya kwa Wakuu wa Mikoa.

Kwa sasa kila mara serikali inapofanya makosa, lawama wanatupiwa mawaziri ambao wanadaiwa niwa ''Rais Magufuli'' na wanafanya kazi kwa kutumia ''mentality'' ya Rais Magufuli kwa sababu hawakuteuliwa na Rais Samia. Kama angefanya kama alivyofanya kwa Wakuu wa Mikoa, hizi lawama zisingeendelea kuwepo!

Je, Rais Samia aliogopa nini kufanya kama alivyofanya kwa Wakuu wa Mikoa ''wapya''?

Kwenye hili suala la rais kufariki akiwa madarakani, nimegundua katiba yetu ni dhaifu sana. Yaani kumetokea tafsiri za kubahatisha vibaya sana, haifahamiki ni awamu ya ngapi, rais aunde vipi serikali yake nk. Nyingi vya tafsiri hazikuwa za kunyooka bali ubabaishaji mkubwa.
 
Je, Rais Samia aliogopa nini kufanya kama alivyofanya kwa Wakuu wa Mikoa ''wapya''?
Alisema anawapa muda watendaji wote aliowakuta ili aone ufanisi wao kwanza kabla ya kufanya mabadiliko.

Amefanya kwa wakuu wa mikoa, now who are next? Labda wanaofuata ni hao hao mawaziri sasa.
 
Nilishangaa kidogo kusoma Press Release ya Ikulu ambayo ilitangaza majina ya Wakuu wa Mikoa ''wapya'' ambao WAMETEULIWA na Rais Samia. Kilichonishangaza ni lugha iliyotumika lakini ''kiuhalisia'' kilichofanyika ni UHAMISHO TU wa Wakuu wa Mikoa na kuziba nafasi za wale wamestaafu.

Rais Samia alichofanya ni kuhamisha hao Wakuu wa Mikoa kitu ambacho ni kizuri kiutendaji lakini pia ni kibaya kwa matumizi ya fedha na muda. Hawa Wakuu wa Mikoa itabidi walipwe pesa za Uhamisho lakini pia itawachukua muda kuyazoea mazingira kikazi ya sehemu waliyohamishwa.

Sasa kama ameweza kufanya hivi kwa Wakuu wote wa Mikoa, Kwa nini hakufanya hivyo kwa Waziri Mkuu na Mawaziri ili ionekane hii ni serikali yake ya Awamu ya Sita na sio Serikali ya Awamu ya tano yenye Rais wa Sita!

Rais Samia alitakiwa apendekeze Jina la Waziri Mkuu hata kama ni yule yule (Majaliwa) na likapigiwe kura bungeni kama Katiba inavyosema, halafu baadaye aunde baraza lake la Mawaziri hata kama ni wale wale halafu awaapishe kama atakavyofanya kwa Wakuu wa Mikoa.

Kwa sasa kila mara serikali inapofanya makosa, lawama wanatupiwa mawaziri ambao wanadaiwa niwa ''Rais Magufuli'' na wanafanya kazi kwa kutumia ''mentality'' ya Rais Magufuli kwa sababu hawakuteuliwa na Rais Samia. Kama angefanya kama alivyofanya kwa Wakuu wa Mikoa, hizi lawama zisingeendelea kuwepo!

Je, Rais Samia aliogopa nini kufanya kama alivyofanya kwa Wakuu wa Mikoa ''wapya''?
Kwa hiyo Waziri Mkuu KIAPO cha Utiifu kwa Rais aliapa kwa Magufuli na Sio kwa Samia kisheria hii ikoje?
 
Back
Top Bottom