Kama Rais anafikiri ataua upinzani kwa kununua viongozi kamwe hatofanikiwa

Status
Not open for further replies.

Quinine

JF-Expert Member
Jul 26, 2010
21,271
47,271
Enzi za chama kimoja hakukuwa na viongozi wa vyama vya upinzani lakini sio kwamba upinzani haukuwepo. Wakati wa uchaguzi watu walielekezwa kuchagua kati ya picha ya Nyerere na kivuli lakini bado kuna watu walichagua kivuli bila ya kuongozwa na kiongozi yeyote wa upinzani.

Kwangu mimi kununua au kuhonga kiongozi aje upande wako ni stage ya mwisho ya chama kinachoelekea kupoteza dira au chama kinachoelekea kufa, kwamba chama kimeishiwa sera na mbinu za kuwafanya wananchi kujiunga nacho zaidi ya kutumia nguvu ya pesa na kuwahonga vyeo.

Nionavyo mimi njia sahihi ya kuuwa vyama vya upinzani ni kutimiza ahadi ambazo chama au mgombea alizitoa, kuwaletea wananchi maendeleo chanya kiasi kwamba viongozi au wananchi wenyewe wakose sababu ya kubaki upinzani.

Kununua kiongozi wa upinzani, hakuondoi shida ya maji watu wataendelea kudai maji, kununua viongozi wa upinzani hakufanyi elimu iwe bora, hakuongezi ajira wala hakuongezi mlo kwenye familia, kununua viongozi hakujengi viwanda wala hakuboreshi maisha ya Mtanzania.

Upinzani siyo viongozi, kiongozi wa upinzani ni shida unazopata, mateso unayopata, haki unayonyimwa kulingana na unavyostahili kupata, upinzani ni chakula chako unachopata, ni elimu yako uliyopata, kiongozi wa upinzani ni miundombinu yako, ni afya yako uliyonayo, ni upatikanaji wa maji, ni uhuru wa kujieleza ulionao, siku hivyo vitu vikikosekana akili yako yenyewe itakuongoza kumkataa aliyeko madarakani hautasubiri kuambiwa na kiongozi wa upinzani.

Kwahiyo kitendo cha kununua au kuhonga viongozi ili waje upande mmoja hakutafanya watu wakupende au wakipende chama chako, hata kama CCM itafanikiwa kuwanunua viongozi wote wa vyama vya upinzani, najua hakitaweza kuwanunua watanzania wote million 50, bado kitakuja kupambana na wananchi wenyewe na mbaya zaidi wananchi walioachwa watakuwa hawana kiongozi wa kuwaelekeza wafanye nini.
 
Enzi za chama kimoja hakukuwa na viongozi wa vyama vya upinzani lakini sio kwamba upinzani haukuwepo. Wakati wa uchaguzi watu walielekezwa kuchagua kati ya picha ya Nyerere na kivuli lakini bado kuna watu walichagua kivuli bila ya kuongozwa na kiongozi yeyote wa upinzani.

Kwangu mimi kununua au kuhonga kiongozi aje upande wako ni stage ya mwisho ya chama kinachoelekea kupoteza dira au chama kinachoelekea kufa, kwamba chama kimeishiwa sera na mbinu za kuwafanya wananchi kujiunga nacho zaidi ya kutumia nguvu ya pesa na kuwahonga vyeo.

Nionavyo mimi njia sahihi ya kuuwa vyama vya upinzani ni kutimiza ahadi ambazo chama au mgombea alizitoa kiasi kwamba viongozi au wananchi wenyewe wakose sababu ya kubaki upinzani.

Kununua viongozi wa upinzani, hakuondoi shida ya maji watu wataendelea kudai maji, kununua viongozi wa upinzani hakufanyi elimu iwe bora, hakuongezi ajira wala hakuongezi mlo kwenye familia, kununua viongozi hakujengi viwanda wala hakuboreshi maisha ya Mtanzania.

Kwahiyo kitendo cha kununua au kuhonga viongozi ili waje upande mmoja hakutafanya watu wakupende au wakipende chama chako, hata kama CCM itafanikiwa kuwanunua viongozi wote wa vyama vya upinzani, najua hakitaweza kuwanunua watanzania wote million 50, bado kitakuja kupambana na wananchi wenyewe na mbaya zaidi wananchi walioachwa watakuwa hawana kiongozi wa kuwaelekeza wafanye nini.
Ukimtoa Zitto Kabwe nitajie kiongozi wa upinzani ambaye hana kadi ya CCM?!! Kiufupi hao hawanunuliwi bali wanarejea nyumbani!!
 
Bado chadema hamjajua nini hasa tatizo lenu,
mkuu paschal mayala amewachambulia vizuri kabisa ktk thread yake leo, ya kwamba msiwapuuze wahamiaji, but naona bado mnazungukazunguka tuu!
Ama kweli sikio la kufa halisikii dawa.
 
Kununua viongozi wa upinzani kunapunguza uwezo wa taifa kujitathmini. Tusitarajie maendelea kwa style hii ya siku hizi. Kuzuia fikra za watanzania zaidi mil 50, kupitia mfumo huu wa vyama vingi kamwe hakuwezi kuongeza tija katika utendaji wa serikali hii. Kununua viongozi wa upinzani hakuwezi kitengeneza maficho ya kudumu ya UKWELI. "Ukweli ndiyo adui wa kudumu wa udhalimu unaoendelea sasa hivi nchi!
 
jamaa anafanya teuzi ambazo hazitikisi Soko la Hisa maana yake hakuna la maana anafanya lenye kuleta impact kwenye economy. ni siasa za majitaka tu.
Anataka kubaki kwenye vitabu vya historia kama mtawala alitumia kipindi chake chote kudumaza upinzani,aliyetawala kwa chuki na visasi, asiyeambilika na mwenye kuonesha upendeleo wa wazi wazi! Historia itamchora tu! Madhali tumeshamjua kwa rangi yake halisi basi tutaishi naye kwa akili!
 
Huku ni kuishiwa mbinu kisiasa,utanunua wapinzani wangapi na je huku ndio kutatua shida za kijamii ??bila shaka sivyo,hii ni dalili tu ya kushindwa na kuishiwa Sera...utumiaji wa mabavu kuingilia maisha binafsi ya wapinzani kuwadhoofisha(njaa)ili waurudie mfupa aloushindwa fisi.
Nawaambieni ukijumlisha na yale ya madiwani arusha aisee hi awamu ni ya mavuno kwa wenye njaa za utosi
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom