Mwifwa
JF-Expert Member
- Apr 3, 2017
- 46,881
- 122,124
Hakuna jambo jema kama kuwa mzalendo wa kweli katika nchi yako, Askofu Kakobe kaonesha Uzalendo wa kweli na kutambua juhudi za Rais Magufuli katika kufufua Shirika la ndege nchini.
Tunapaswa kuwa wazalendo kama Kakobe ili tuweze kupiga hatua katika maendeleo ya nchi yetu.
Wakati Kakobe akipokea Ndege pamoja na Rais, Wazalendo wengine waliamua kuendelea na mpango wa kuandamana kupongeza juhudi za ufumbuzi wa Kikokotoo uliotolea na Rais siku za hivi karibuni.
Kwa uzalendo wa Kakobe aliouonesha, kama ningekuwa mimi haya maneno yangekuwa miongoni mwa maneno ya hotuba yangu.
Rais Magufuli ni msikivu, muelewa, anapenda kushauriwa hasa katika mambo ya maslahi mapana ya Taifa, hata nilipomshauri atubu, alitubu na akawaomba watanzania wamuombee hadi kapata ujasiri wa kuthubutu kufanya mambo makubwa yaliyoshindikana kama ununuzi wa Ndege, na leo tumeipokea Ndege ya 6 ya Airbus
Hongera Kakobe wewe ni mtanzania halisi kutoka mwisho wa reli(Ujiji-Kigoma)
Tunapaswa kuwa wazalendo kama Kakobe ili tuweze kupiga hatua katika maendeleo ya nchi yetu.
Wakati Kakobe akipokea Ndege pamoja na Rais, Wazalendo wengine waliamua kuendelea na mpango wa kuandamana kupongeza juhudi za ufumbuzi wa Kikokotoo uliotolea na Rais siku za hivi karibuni.
Kwa uzalendo wa Kakobe aliouonesha, kama ningekuwa mimi haya maneno yangekuwa miongoni mwa maneno ya hotuba yangu.
Rais Magufuli ni msikivu, muelewa, anapenda kushauriwa hasa katika mambo ya maslahi mapana ya Taifa, hata nilipomshauri atubu, alitubu na akawaomba watanzania wamuombee hadi kapata ujasiri wa kuthubutu kufanya mambo makubwa yaliyoshindikana kama ununuzi wa Ndege, na leo tumeipokea Ndege ya 6 ya Airbus
Hongera Kakobe wewe ni mtanzania halisi kutoka mwisho wa reli(Ujiji-Kigoma)