Kama ni wewe mwanaume mwenzangu hili tatizo ungelitatuaje?

Brown Kwacha

JF-Expert Member
Jul 31, 2017
299
405
Hata wanawake mnaruhusiwa kuchangia.

Ok ipo wakuu soma yote pls.
Nilikuwa mbali na nyumbani nikakutana na binti fulani nikampenda nikamtongoza baada ya muda akanikubalia tukaanza kudate.

Alinisimulia maisha yake yaliyopita moja akadai ujauzito wake wa miezi mitano ulimharibikia. Nilimpa pole nami nikamsimulia yangu, tukaendelea kudate.

I live alone, alikuwa anafanya kazi karibu na ninapoishi hivyo jioni kabla ya kurudi kwao lazima apite kwangu kisha aondoke. Baada ya muda nikaanza kula tunda life likaendelea, tukala tunda kavu.

Siku moja akaniambia anataka akafanye vipimo nikamwambia ok. Majibu kurudi anamimba. Akaniuliza vipi (nikiwa mkweli) nilimshauri tutoe tukakubaliana bila kinyongo. Mahusiano yalizidi kuendelea bila tatizo. Tukashauriana atumie vidonge.

Akawa anatumia na kila siku nikawa namkumbusha. After three weeks tena akaniambia anataka akachukue vipimo akaenda majibu kurudi anaujauzito. Hapa aliniwahi akasema akiendelea kutoa atahatarisha maisha yake. Lakini nikamuuliza si ulikuwa unatumia pills?? Akasema haelewi.

Ok, nikasema kama kweli yametokea haya na tulitumia mbinu zote kuzuia nitakubaliana na kila kiti usitoe. Ishu ikawa kwa wazazi wake atasemaje?? Akaniambia wazazi wakijua nimepata mimba ya mgeni sitakuwa na cha kuongea hivyo nitaficha hadi watakapogundua.

Tukawa tunaendelea na mapenzi yetu. Kufupisha stori.

-Huyu binti anamdogo wake lakini mimi toka siku ya kwanza nilihisi ni mwanae. Tumegombana saana kwenye hili. Alinitumia hadi vyeti vyake vya kuzaliwa akidai ni mdogo wake. Ila nafsi haikukubali hadi kesho. Namna ya kuthibitisha sina.

-Juzi amenilalamikia nimekuwa kimya saana lakini sio kweli nikimwambia njoo nyumbani hataki toka december, hivyo anaona simpendi tena.

- lingine baada ya kukwaruzana na familia aliamua kuishi nyumba ya babu yao mbali na nyumbani lakini bado anaishi na yule anayemuita mdogo wake.

-Lililonitisha zaidi ni nimemshauri juzi njoo tuishi pamoja kwa kipindi hiki ujauzito mdogo kisha tuta-sort baadhi ya mambo. Tukakubaliana atanipa feedback jana ila jana anadai hawezi kuhama maana anaishi na mdogo wake.

-kuna siku alikuja nyumbani nikaomba mchezo akaninyima akiamini haniamini kama sijatembea na mwanamke mwingine. Nilimjibu vibaya(Nilimwambia inamaana huwezi kuniamini? Mbona mimi niliamini ujauzito ni wangu) alilia saana)

-Nimekuwa najaribu kutumia busara ya kila aina nisimwache aone ananyanyasika au namwachia mzigo wa kulea lakini naona naelekea kushindwa.

1. Toka mwanzo nilimwambia kama una mtoto na ulinificha siwezi kukubaliana na lolote. Huu wasiwasi nimeueleza hapo juu.

2. Analalamika simpendi tena ilihali natumia mbinu zote aje aishi nami maana anaonekana yupo lonely napo hataki. Sasa mimi nifanye nini? Na week siku sio nyingi aliniblock nikatumia simu card nyingine kumtafuta...nikamwambia wewe mbinafsi saana. Unaniblock ili uifurahishe nafsi yako while kid ndiye anaenda kuumia. Nimechoka kuandika.
 
Either hana mimba, au kama anayo siyo yako.
Hata mimi nimekuwa nikihisi hili la kutokuwa na mimba.

Lakini nimeona kadi...or she made some fake copies? What for? Nimejiuliza saana.

Hilo la mimba kutokuwa yangu.
Nitalifuatilia japo..tatizo siwezi kufanya uchunguzi ni ngumu? Unanishauri nifanyeje! Jana nilifikiria kumpotezea kama anamimba yangu akajijue mwenyewe ila roho inanisuta mtoto.
 
Una uhakika ana mimba?!
Kwamba labda ananichezea vimichezo.

-Nililifikiria hili ila alinionyesha kadi. Kumbuka pia toka aseme anaujauzito hajawahi kulala kwangu akawa ananikwepa na kutumia pointi ya wazazi wake wakijua anamimba na mgeni atafanywa vibaya akaanza kukwepa nyumbani.
 
Wewe unapenda kunywa maziwa ila hutaki kufuga ng'ombe

kuna kitu tunaita barua t0mb@
unapeleka kisha anakuwa free kuja kwako hii inasaidia sana wasiooa
Sijaelewa mkuu! Naomba unifafanulie kama unataka nikuelewe.
 
Hata mimi nimekuwa nikihisi hili la kutokuwa na mimba.

Lakini nimeona kadi...or she made some fake copies? What for? Nimejiuliza saana.

Hilo la mimba kutokuwa yangu.
Nitalifuatilia japo..tatizo siwezi kufanya uchunguzi ni ngumu? Unanishauri nifanyeje! Jana nilifikiria kumpotezea kama anamimba yangu akajijue mwenyewe ila roho inanisuta mtoto.

Sina uhakika kama nina ushauri sahihi.
 
Inawezekana anakuchezea kamchezo tuu hana mimba!
Muombe mkapime pamoja
Nitafanya hili ni ushauri mzuri.

Je nikikuta mimba ni yangu na akaendelea kunifanyia hivi vituko nichukue hatua gani? Nimpotezee hadi atakaponitafuta!
 
Nasikitika sana sisi vijana wa siku hizi tunavyoanza mahusiano bila malengo ya kuoa alafu tunakuja kubadili gia angani eti ndo tunataka kuoa.

Mkuu hayo yametokana na wewe mwenyewe kuwa na mipango mibovu tokea mwanzo,unsjua fika uko bado na hayo majukumu alafu unachukua demu mkuu.

وما أصابكم من مصيبة فبما كسبت أيديكم ويعفو عن كثير

[ ASH-SHUURA - 30 ]
Na misiba inayo kusibuni ni kwa sababu ya vitendo vya mikono yenu. Naye anasamehe mengi.

Lakini hasa inakuwaje mtu anamlea binti mkuubwaa(demu) alafu anaogopa kumlea katoto kachanga tu?

Ok mkuu hilo jambo sio jema,kama kweli una nia ya dhati ya kuondokana na misuko suko basi fanya maamuzi ya kiume,nenda kaongee nae kikubwa ikiwezekana tuma watu wenye heshima waende kwao kutangaza posa na mipango ya ndoa ifanyike.

Wanawake msikubali kuzalishwa kabla ya kuolewa mnajipotezea point bure kabisa.mwanaume anakuambia hataki mimba na hajakuoa hufikirii ana lengo gani huyo?
 
7 Reactions
Reply
Back
Top Bottom