sabuwanka
JF-Expert Member
- Apr 11, 2015
- 690
- 751
Wakuu salamu, nimendika sentensi hiyo hapo juu ambayo ni ushauri ulitolewa kwa mtu anayetaka kupunguza uzito, nimepitia thread moja humu mdau akieleza jinsi vyakula vya wali na ugali vinavyochangia kuongeza uzito hasa kwa wanaofanya kazi za maofisini, maana muda mwingi wanakuwa wamekaa na hata wakifanya mazoezi ya mwili bado hayana uhusiano wa moja kwa moja na kupungua uzito, pamoja na mazoezi ya mwili pia ushauri mwingine ni kupunguza/kuacha chakula Cha usiku kwa kuwa chakula tunachokula usiku hakina kazi kubwa na hivyo hutunzwa Kama mafuta katika sehemu za tumbo, mapaja , kiuno nk.
Kama umetumia mbinu nyingi umekwama kupunguza uzito...hii inaweza kukufaa ikiwa hauna kisukari!
Ikumbukwe kuwa janga la OBESITY ni janga la duniani, ndo maana makampuni yanayocheza na fursa yamekuja na madawa kwa ajili ya suluhisho...ingawa mchango wake sio mkubwa Kama unavyotangazwa
Uzito mkubwa na na kuwa na lehemu nyingi katika damu ni chanzo Cha magonjwa ya moyo, pamoja na kutokuwa na nguvu za kijinsia ......hii nayo imekuwa fursa ya kuja na kila lundo la dawa za nguvu za kiume bila kuangalia chanzo halisi Cha tatizo
Kwa yeyote mwenye mchango /uzoefu/maoni /mawazo kuhusu hii mada karibu
Kama umetumia mbinu nyingi umekwama kupunguza uzito...hii inaweza kukufaa ikiwa hauna kisukari!
Ikumbukwe kuwa janga la OBESITY ni janga la duniani, ndo maana makampuni yanayocheza na fursa yamekuja na madawa kwa ajili ya suluhisho...ingawa mchango wake sio mkubwa Kama unavyotangazwa
Uzito mkubwa na na kuwa na lehemu nyingi katika damu ni chanzo Cha magonjwa ya moyo, pamoja na kutokuwa na nguvu za kijinsia ......hii nayo imekuwa fursa ya kuja na kila lundo la dawa za nguvu za kiume bila kuangalia chanzo halisi Cha tatizo
Kwa yeyote mwenye mchango /uzoefu/maoni /mawazo kuhusu hii mada karibu