Kama ni kweli marehemu Mabina alimuua mtu kwa risasi mbona picha yake haikuonekana???

Laiser James

Member
Dec 5, 2013
77
8
Siku ya Jumapili tar 15 Nguvu ya Umma Jijini Mwanza ktk kata ya Kisesa,ilijichukulia sheria mkononi kwa kumuua aliewahi kuwa Mwenyekiti wa Ccm Mkoa wa Mwanza na Diwani wao Marehemu Mabina.

Hii ilitokea baada ya kile kinachodaiwa kuwa ni ugomvi wa kugombea eneo la mlima kati ya marehemu Mabina na wananchi hao waliomchagua kuwa kiongozi wao.

Ni takriban siku 3 sasa tangia kutokea kwa tukio hili la "aibu"na kusikitisha km sio Kuuzunisha.
Kinachonishangaza ni kitendo cha picha za marehemu Mabina kuwekwa na kusambazwa ktk mitandao ya kijamii zikimuonyesha akiwa chini huku kichwani akionekana kakatwa kwa vitu vyenye makali na mawe yakiwa pembeni mwa mwili wake,lakini pia picha zingine zikimuonyesha akiwa Mochwari ila hakuna hata picha moja iliowekwa ktk magazeti au mitandao ya kijamii km ilivyofanywa kwa marehemu Mabina ikimuonyesha huyo anaedaiwa kuuawa kwa risasi.

Je ni kweli kuna mtu kauawa na Marehemu Mabina kabla ya yeye nae kuuliwa na wananchi wenye hasira? Na km yupo nini sababu ya picha zake kutoonyeshwa?
 
yupo aliyeuawa na PDG MABINA , BALI WALETA PICHA wameona picha za mabina ndiyo za maana , zile za yule masikini hazina mvuto !
 
Kuonyesha picha ya maiti kwani deal? Hata walivyofanya hiyo ya mabina ?
 
Back
Top Bottom