Kama ni kweli basi System ndo Tatizo

Lord denning

JF-Expert Member
Jun 3, 2015
13,148
25,814
Ukiwa ni mfuatiliaji wa siasa za dunia utagundua kitu kimoja kuwa kwenye nchi nyingi sana duniani kama sio zote systems zina mchango mkubwa sana kwenye kupatikana viongozi wanaoziongoza nchi izo. Hii ni kuanzia Nchi tajiri hadi Nchi masikini. Nitatoa maelezo vizuri kidogo ili niweze kueleweka vizuri.

Kwenye nchi zote duniani kuna vitengo vyao vya intellejensia ambavyo kazi kubwa ni kusoma siasa na hali za uchumi za nchi husika na za nchi za dunia na hivo vitengo kazi yake kubwa ni kubashiri au hata kupanga kuwa kwa hali ilivo nchini na kwa hali ilivo duniani ni vizuri tukapata kiongozi au tukawa na kiongozi wa aina fulani ili kwanza nchi iweze kutulia na pili nchi iweze kusonga mbele. Hivi vitengo huwa vinastudy hadi sera za nchi fulani na kutoa ushauri kwenye nchi zao kuwa kutokana na nchi fulani kuchukua sera fulani basi nasi tuchukue njia fulani ili tu uchumi wa nchi na hali ya nchi iwe salama.

Ndo mana kama urusi unaona system inambakisha putin ili aweze kutengeneza watu wengi wa aina yake kwa ajili ya kuweza kupambana na hila za marekani kwa mustakabali wa nchi ya urusi, ndo mana hata china system saivi inatengeneza viongozi wenye kaliba ya unyenyekevu na upole kwa sababu china saivi inajijenga kimataifa ili kuwa nchi yenye ushawishi kibiashara duniani mfano waangalie raisi wa china aliyepita na huyu wa sasa xi jiping.

Ndo mana mnaona Iran inabadilisha viongozi kutoka mwenye msimamo mkali aliyeijenga irani kijeshi Mahmoud Ahmadinejad na huyu wa sasa mwenye hulka ya upole Hassan Rouhan kwa sababu tu wameona watulize mgogoro wao na marekani ili waweze kujijenga kiuchumi. Ndo mana kuna hata watu wanasema kuwa J.F Kennedy aliuawa na system yenyewe ya marekani baada ya kuona kuwa kuna mambo alikuwa akienda against nayo kwa mujibu wa mipango yao.

Nimesema haya kutokana na jambo lililo midomoni mwa watanzania wengi kuanzia siku ya jana hadi leo hii nalo ni kutangaza nia na kuchukua fomu kwa nguli wa sheria duniani Jaji Mkuu Mstaafu Augustino Ramadhani. Kuna watu wanasema kuwa huyu ni chaguo la system na wengine wanasema huyu ni chaguo na Kikwete.

Kuna kitu nimekiwaza sana na sidhani kama kweli ni system ndo imeshauri ivo ilikuwa makini kwa kuelewa tatizo letu Tanzania ni nini na tufanyeje ili kutoka hapa na ndo mana nimeamua kuandika hii thread. Kama tuna system makini lazima itajua kwa sasa Tanzania tunaitaji kiongozi wa namna gani. Na kama huyu ni chaguo la mkuu basi mkuu inabidi atafakari sana na washauri wake kama wana mapenzi mazuri na vizazi vyao huko mbeleni.

Hata kama umeshuka leo kutoka nchi jirani ukizunguka mikoa 5 tu na kuwauliza watu 20 kwenye kila mkoa watakwambia tatizo kubwa la Tanzania nchi haiendi, watu wanachukuliana poa, hamna userious kwenyew kazi na kuwahudumia wananchi,watakwambia kuna tatizo la rushwa na upigaji yani kila mtu ni mwizi na anataka apate nafasi aibe, watakwambia kuna matatizo ya afya,elimu,maji, miradi kutokamilika kwa wakati na watu kula fedha za miradi na watakwambia pia kun a utekelezaji wa miradi chini ya kiwango.

Ukitoka hapo ukifanya study ya jamii ya watanzania hata kwa miezi miwili tu, kwa kuanzia kwenye maofisi,kwenye television na mijadala inayofanyikaga kwenye television na hata kwenye vijiwe utagundua kitu kimoja kuwa watanzania ni watu wa porojo na siasa sana. Ni watu wa maneno mengi na kulalamika si maofisini,si vijiweni, si kwenye mitaa na vijiwe na si kwenye kwenye kumbi za starehe.

Utagundua kuwa kuna opportunities nyingi sana Tanzania ila wazawa hawazitumii na wageni kutoka kenya,south africa na zimbabwe wanakuja wanazitumia na kutengeneza mamilioni ya fedha kila siku. Utagundua kuna tatizo kubwa sana kwenye mifumo ya uli[paji kodi na wananchi wengi sana hawalipi kodi, utagundua kuna ukwepaji mkubwa sana wa kodi unaoikosesha serikali mapato mengi sana.

Sasa kama tungekuwa na system makini iyo system ingeweza kuyaona haya yote na siku ya mwisho ndo ingeshauri nani wa kumpa hii dola ili arekebishe haya yote. Sishani kwa system makini ingependekeza mtu mpole, mkimya na asiyeweza kukemea kama Jaji Agustino Ramadhani.

Sina mashaka na weredi,uadilifu na hekima za Jaji Ramadhani ila kama kweli yeye ndo chaguo la watu fulani kama wanavojulikana "The System" basi watakuwa wamekosea sana kwa sababu Tanzania kwa ilipofika hapa na dunia inavokimbia bila shaka tunaitaji watu aina ya Prof Muhongo au John Pombe Magufuli. Tutadanganyana sana ila siku ya mwisho huu ndo ukweli na utabaki kuwa ukweli.

Kama nilivoandika kwenye post inayomuhusu Jaji Ramadhani napenda nirudie tena hapa na someni tena ndugu zanguni

  • TANZANIA INAITAJI MTU SERIOUS, MTU MKALI NA MFUATILIAJI WA MAMBO, MTU ASIYE MPOLE NA ANAYEJUA TATIZO KUU LA WATANZANIA NI UVIVU, KUPENDA POROJO, KUENDEKEZA SIASA KILA MAHALI NA KUTOJITUMA. TATIZO LA TANZANIA NI KUKOSA MTU THABITI MWENYE MAONO FULANI JUU YA UCHUMI WA NCHI NA UCHUMI WA DUNIA AMBAPO HAPA SIDHANI KAMA ATAFIT VIZURI. SIDHANI KAMA ATAWEZA KUPAMBANA NA FITNA ZA KINA MEDIA TYCOON AMBAO WAKIKOSA VITU WANAVYOVITAKA WANAANZA KUIYUMBISHA SERIKALI NA WATENDAJI WAKE KAMA WAPENDAVYO.SIDHANI KAMA ATAWEZA KULISIMAMIA BARAZA LAKE LA MAWAZIRI LIWEZE KUDERIVER KWENYE STANDARDS ZA JUU KABISA INAVOTAKIWA.

Asubuhi njema ndugu zanguni
 
Nani alikudanganya Rais mzuri ni anayejua kukemea? Hatuhitaji mpiga kelele mwenye kupenda sifa majukwaani, tunahitaji rais atakayesimamia utawala wa sheria, na kuchukua hatua stahiki kwa wezi, wala rushwa na wazembe, na sio kuwakemea. By the way andiko lako linaonekana ulikotoka
 
Kuna kitu najifunza hapa,Rais wa hulka ya Ramadhan ni msikivu na hupenda kutoa uhuru wa kiutendaji kwa wasaidizi wake. Ninaamini utawala wake kama utakuwa na baraza zuri la mawaziri basi utakuwa ni utawala mmoja wenye mafanikio sana.Anachotakiwa kufanya ni kuwa mkali kwenye suala la uadilifu na uwajibikaji, giving freedom to act to his assistants will make his administration more successful.The only problem I have about his potential presidency is his association with the outgoing President,huyu ataenda kulinda madhambi ya utawala uliopita, angegombea kupitia UKAWA I would take him more seriously.
 
Nani alikudanganya Rais mzuri ni anayejua kukemea? Hatuhitaji mpiga kelele mwenye kupenda sifa majukwaani, tunahitaji rais atakayesimamia utawala wa sheria, na kuchukua hatua stahiki kwa wezi, wala rushwa na wazembe, na sio kuwakemea. By the way andiko lako linaonekana ulikotoka
Duuh umeshanivamia mimi mkuu?? Kwani me nimetokea wapi?
 
Ukiwa ni mfuatiliaji wa siasa za dunia utagundua kitu kimoja kuwa kwenye nchi nyingi sana duniani kama sio zote systems zina mchango mkubwa sana kwenye kupatikana viongozi wanaoziongoza nchi izo. Hii ni kuanzia Nchi tajiri hadi Nchi masikini. Nitatoa maelezo vizuri kidogo ili niweze kueleweka vizuri.

Kwenye nchi zote duniani kuna vitengo vyao vya intellejensia ambavyo kazi kubwa ni kusoma siasa na hali za uchumi za nchi husika na za nchi za dunia na hivo vitengo kazi yake kubwa ni kubashiri au hata kupanga kuwa kwa hali ilivo nchini na kwa hali ilivo duniani ni vizuri tukapata kiongozi au tukawa na kiongozi wa aina fulani ili kwanza nchi iweze kutulia na pili nchi iweze kusonga mbele. Hivi vitengo huwa vinastudy hadi sera za nchi fulani na kutoa ushauri kwenye nchi zao kuwa kutokana na nchi fulani kuchukua sera fulani basi nasi tuchukue njia fulani ili tu uchumi wa nchi na hali ya nchi iwe salama.

Ndo mana kama urusi unaona system inambakisha putin ili aweze kutengeneza watu wengi wa aina yake kwa ajili ya kuweza kupambana na hila za marekani kwa mustakabali wa nchi ya urusi, ndo mana hata china system saivi inatengeneza viongozi wenye kaliba ya unyenyekevu na upole kwa sababu china saivi inajijenga kimataifa ili kuwa nchi yenye ushawishi kibiashara duniani mfano waangalie raisi wa china aliyepita na huyu wa sasa xi jiping.

Ndo mana mnaona Iran inabadilisha viongozi kutoka mwenye msimamo mkali aliyeijenga irani kijeshi Mahmoud Ahmadinejad na huyu wa sasa mwenye hulka ya upole Hassan Rouhan kwa sababu tu wameona watulize mgogoro wao na marekani ili waweze kujijenga kiuchumi. Ndo mana kuna hata watu wanasema kuwa J.F Kennedy aliuawa na system yenyewe ya marekani baada ya kuona kuwa kuna mambo alikuwa akienda against nayo kwa mujibu wa mipango yao.

Nimesema haya kutokana na jambo lililo midomoni mwa watanzania wengi kuanzia siku ya jana hadi leo hii nalo ni kutangaza nia na kuchukua fomu kwa nguli wa sheria duniani Jaji Mkuu Mstaafu Augustino Ramadhani. Kuna watu wanasema kuwa huyu ni chaguo la system na wengine wanasema huyu ni chaguo na Kikwete.

Kuna kitu nimekiwaza sana na sidhani kama kweli ni system ndo imeshauri ivo ilikuwa makini kwa kuelewa tatizo letu Tanzania ni nini na tufanyeje ili kutoka hapa na ndo mana nimeamua kuandika hii thread. Kama tuna system makini lazima itajua kwa sasa Tanzania tunaitaji kiongozi wa namna gani. Na kama huyu ni chaguo la mkuu basi mkuu inabidi atafakari sana na washauri wake kama wana mapenzi mazuri na vizazi vyao huko mbeleni.

Hata kama umeshuka leo kutoka nchi jirani ukizunguka mikoa 5 tu na kuwauliza watu 20 kwenye kila mkoa watakwambia tatizo kubwa la Tanzania nchi haiendi, watu wanachukuliana poa, hamna userious kwenyew kazi na kuwahudumia wananchi,watakwambia kuna tatizo la rushwa na upigaji yani kila mtu ni mwizi na anataka apate nafasi aibe, watakwambia kuna matatizo ya afya,elimu,maji, miradi kutokamilika kwa wakati na watu kula fedha za miradi na watakwambia pia kun a utekelezaji wa miradi chini ya kiwango.

Ukitoka hapo ukifanya study ya jamii ya watanzania hata kwa miezi miwili tu, kwa kuanzia kwenye maofisi,kwenye television na mijadala inayofanyikaga kwenye television na hata kwenye vijiwe utagundua kitu kimoja kuwa watanzania ni watu wa porojo na siasa sana. Ni watu wa maneno mengi na kulalamika si maofisini,si vijiweni, si kwenye mitaa na vijiwe na si kwenye kwenye kumbi za starehe.

Utagundua kuwa kuna opportunities nyingi sana Tanzania ila wazawa hawazitumii na wageni kutoka kenya,south africa na zimbabwe wanakuja wanazitumia na kutengeneza mamilioni ya fedha kila siku. Utagundua kuna tatizo kubwa sana kwenye mifumo ya uli[paji kodi na wananchi wengi sana hawalipi kodi, utagundua kuna ukwepaji mkubwa sana wa kodi unaoikosesha serikali mapato mengi sana.

Sasa kama tungekuwa na system makini iyo system ingeweza kuyaona haya yote na siku ya mwisho ndo ingeshauri nani wa kumpa hii dola ili arekebishe haya yote. Sishani kwa system makini ingependekeza mtu mpole, mkimya na asiyeweza kukemea kama Jaji Agustino Ramadhani.

Sina mashaka na weredi,uadilifu na hekima za Jaji Ramadhani ila kama kweli yeye ndo chaguo la watu fulani kama wanavojulikana "The System" basi watakuwa wamekosea sana kwa sababu Tanzania kwa ilipofika hapa na dunia inavokimbia bila shaka tunaitaji watu aina ya Prof Muhongo au John Pombe Magufuli. Tutadanganyana sana ila siku ya mwisho huu ndo ukweli na utabaki kuwa ukweli.

Kama nilivoandika kwenye post inayomuhusu Jaji Ramadhani napenda nirudie tena hapa na someni tena ndugu zanguni

  • TANZANIA INAITAJI MTU SERIOUS, MTU MKALI NA MFUATILIAJI WA MAMBO, MTU ASIYE MPOLE NA ANAYEJUA TATIZO KUU LA WATANZANIA NI UVIVU, KUPENDA POROJO, KUENDEKEZA SIASA KILA MAHALI NA KUTOJITUMA. TATIZO LA TANZANIA NI KUKOSA MTU THABITI MWENYE MAONO FULANI JUU YA UCHUMI WA NCHI NA UCHUMI WA DUNIA AMBAPO HAPA SIDHANI KAMA ATAFIT VIZURI. SIDHANI KAMA ATAWEZA KUPAMBANA NA FITNA ZA KINA MEDIA TYCOON AMBAO WAKIKOSA VITU WANAVYOVITAKA WANAANZA KUIYUMBISHA SERIKALI NA WATENDAJI WAKE KAMA WAPENDAVYO.SIDHANI KAMA ATAWEZA KULISIMAMIA BARAZA LAKE LA MAWAZIRI LIWEZE KUDERIVER KWENYE STANDARDS ZA JUU KABISA INAVOTAKIWA.

Asubuhi njema ndugu zanguni

I love it when a human being uses his/her brain to the fullest. Asante sana Mkuu nafikiri watu wenye intelligency ya aina yako Tanzania ni wachache and i must guess, born along Lake Victoria

System iliyowekwa na Mwalimu ilikuwa system iliyoheshimika sana duniani. By the way im only 33 so dont think im that old, however, i know my country well.
Israel, M16, CIA zilimshindwa mzee mchonge.
Kazi mojawapo ya system ni kuexpand interest ya taifa ndani na nje ya nchi. Marekani "Siaiei"wako kila kona ya nchi ya duniani. Ukisikia mafuta, madini yamvumbuliwa lazima yupo Mmarekani, ukisikia ajali yoyote ya ndege lazima yupo Mmarekani. Wanatafuta nini? ajira kwa raia wao, rasilimali ya nchi na viwanda vyake na kupunguza ukali wa uchumi wa nchi yao.
Kuna wanaosema System haikutaka Hillary Clinton awe rais kwa sababu ya mume wake anachangiwa na waarabu kwenye foundation yake. System haikutaka mdogo wake Kennedy awe Rais kwasababu alijua Ukweli wa kilichomuua Kakake, kwahiyo wakamtungulia mbali. System iliona weusi wanakuwa brain washed na Martin Luther King wanaanza kusababisha nchi isikalike wakamtungulia mbali
Turudi Bongo intellegency iliyowekwa na Mwalimu iliuawa na mwinyi, mkapa akaizika na Kikwete akamalizia 40 arubaini ya marehemu sasa tumebaki na watu wanamfatilia Dr Slaa while he is not the enermy. Enermy namba moja ya Intelligencia ni Rais na balaza lake.
Anyway nimeipenda sana post yako kaka, and pls keep posting more..
 
Suluhisho la matatizo ya pale Magogoni ni ukawa tu,na si vinginevyo! Hebu tuwachane na longolongo za kimahaba!
 
Turudi Bongo intellegency iliyowekwa na Mwalimu iliuawa na mwinyi, mkapa akaizika na Kikwete akamalizia 40 arubaini ya marehemu sasa tumebaki na watu wanamfatilia Dr Slaa while he is not the enermy. Enermy namba moja ya Intelligencia ni Rais na balaza lake.
Anyway nimeipenda sana post yako kaka, and pls keep posting more..[/QUOTE]
Nimeipenda hii conclusion (hitimisho) yako.....lmfao!!!??
 
I love it when a human being uses his/her brain to the fullest. Asante sana Mkuu nafikiri watu wenye intelligency ya aina yako Tanzania ni wachache and i must guess, born along Lake Victoria

System iliyowekwa na Mwalimu ilikuwa system iliyoheshimika sana duniani. By the way im only 33 so dont think im that old, however, i know my country well.
Israel, M16, CIA zilimshindwa mzee mchonge.
Kazi mojawapo ya system ni kuexpand interest ya taifa ndani na nje ya nchi. Marekani "Siaiei"wako kila kona ya nchi ya duniani. Ukisikia mafuta, madini yamvumbuliwa lazima yupo Mmarekani, ukisikia ajali yoyote ya ndege lazima yupo Mmarekani. Wanatafuta nini? ajira kwa raia wao, rasilimali ya nchi na viwanda vyake na kupunguza ukali wa uchumi wa nchi yao.
Kuna wanaosema System haikutaka Hillary Clinton awe rais kwa sababu ya mume wake anachangiwa na waarabu kwenye foundation yake. System haikutaka mdogo wake Kennedy awe Rais kwasababu alijua Ukweli wa kilichomuua Kakake, kwahiyo wakamtungulia mbali. System iliona weusi wanakuwa brain washed na Martin Luther King wanaanza kusababisha nchi isikalike wakamtungulia mbali
Turudi Bongo intellegency iliyowekwa na Mwalimu iliuawa na mwinyi, mkapa akaizika na Kikwete akamalizia 40 arubaini ya marehemu sasa tumebaki na watu wanamfatilia Dr Slaa while he is not the enermy. Enermy namba moja ya Intelligencia ni Rais na balaza lake.
Anyway nimeipenda sana post yako kaka, and pls keep posting more..

Asante sana kaka. Ila umenipa sifa sana Mkuu,zipunguze kidogo,naamini vyote ni kwa utukufu wa Mungu. Natokea maeneo ya Ludewa karibu na ziwa nyasa Mkuu. Tutazidi kushirikiana humu kwa kadri kutakavokuwa na uitaji. Kusema kweli dunia ni kama kijiji sasa tunaitaji kujua vitu vingi sana vinavoiendesha dunia ili tuweze kujitambua na kusonga mbele kama taifa. Mungu azidi kutupa uhai.
 
System ya Tanzania haiwezi kutuletea raisi ambaye atasolve matatizo yanayoikumba jamii ya kitanzania. System inatawaliwa na CCM, yaani ccm na usalama wa taifa ni mtu na mdogo wake. Hata ukiangalia kwa jicho la kawaida usalama wa taifa unawajibika kwa nani, raisi au mwenyekiti wa chama cha mapinduzi? maana raisi na na mwenyekiti wa chama cha mapinduzi ccm ni mtu mmoja. Kwa hiyo system itamchagua mtu ambaye atakiridhisha chama cha mapinduzi ndio maana wakampendekeza Jaji Augustino Ramadhani lengo kuu ni kuua au kuharibu makundi ndani ya chama na sio lengo la kuipatia Tanzania raisi bora.
 
Hatamimi nimependa sana analysis ya mtoa mada kwa sasa Taifa linahitaji kiongozi anayeweza kusukuma mambo yaende mipango tunayo mingi sana tatizo mtekelezaji.Tunahitaji kiongozi mwenyemaono atakayeweza kuitoa nchi ilipo kiuchumi na kuipeleka kuwa nchi ya kipato cha kati.pia atakayeweza kupambana na rushwa zinazolitafuna Taifa.hatuhitaji mtu atakayekuwa alama ya taifa tunahitaji mtu atakaye kuwa kiongozi kwanza awe na uwezo binafsi yeye baadae mfumo utamsaidia.
 
Turudi Bongo intellegency iliyowekwa na Mwalimu iliuawa na mwinyi, mkapa akaizika na Kikwete akamalizia 40 arubaini ya marehemu sasa tumebaki na watu wanamfatilia Dr Slaa while he is not the enermy. Enermy namba moja ya Intelligencia ni Rais na balaza lake.
Anyway nimeipenda sana post yako kaka, and pls keep posting more..
Nimeipenda hii conclusion (hitimisho) yako.....lmfao!!!??[/QUOTE]

Rais na Baraza lake ndio watu pekee namba moja wanaoweza kusabbisha uharibifu mkubwa ndani ya nchi kabla upinzani hawajaweza. Hawa jamaa wanaingia mikataba ya Chief Magungo wakati Dr. Slaa hasa akienda mbali ni maandamano ya wamachinga, mengine hayo ni "ear-say" tu
Tumekosa nidhamu kama taifa, tunahitaji mtu mwenye uwezo wa kuturudisha kwenye mstari. Makundi ya CCM sio tatizo la kitaifa hayo matatizo ya kivyama watasuluhisha huko Lumumba.
 
Hatamimi nimependa sana analysis ya mtoa mada kwa sasa Taifa linahitaji kiongozi anayeweza kusukuma mambo yaende mipango tunayo mingi sana tatizo mtekelezaji.Tunahitaji kiongozi mwenyemaono atakayeweza kuitoa nchi ilipo kiuchumi na kuipeleka kuwa nchi ya kipato cha kati.pia atakayeweza kupambana na rushwa zinazolitafuna Taifa.hatuhitaji mtu atakayekuwa alama ya taifa tunahitaji mtu atakaye kuwa kiongozi kwanza awe na uwezo binafsi yeye baadae mfumo utamsaidia.
Ni hatari sana pale system inaposhindwa kuona jambo ambalo mwananchi wa kawaida tu anaweza kulifikiri na kuliona. Systems imara duniani leo zimeshapanga hadi miaka 50 ijayo wawe na sera gani na mikakati gani na watu wa aina gani kwenye uongozi wa nchi zao ili waweze kwenda na dunia. Kwa kweli sitaki kuamini kama wao kwa hapa Tanzania ndo wameshauri na kupanga ivo. Kama kweli basi kazi itakuwepo kubwa sana huko mbeleni.
 
System ya Tanzania haiwezi kutuletea raisi ambaye atasolve matatizo yanayoikumba jamii ya kitanzania. System inatawaliwa na CCM, yaani ccm na usalama wa taifa ni mtu na mdogo wake. Hata ukiangalia kwa jicho la kawaida usalama wa taifa unawajibika kwa nani, raisi au mwenyekiti wa chama cha mapinduzi? maana raisi na na mwenyekiti wa chama cha mapinduzi ccm ni mtu mmoja. Kwa hiyo system itamchagua mtu ambaye atakiridhisha chama cha mapinduzi ndio maana wakampendekeza Jaji Augustino Ramadhani lengo kuu ni kuua au kuharibu makundi ndani ya chama na sio lengo la kuipatia Tanzania raisi bora.
Kazi kubwa ya systems ni kufanya kazi kwa maslahi mapana ya nchi ama wengine wanaita ni kuprotect national interest. Kwenye kufanya haya wanaweza fanya jambo lolote lile ila dhumuni kuu linakuwaga kwa ajili ya national interest. Kama wakifanya jambo kwa maslahi ya chama au taasisi ilo ni kosa ila kama wakifanya jambo kwenye taasisi au chama kwa maslahi mapana ya nchi ilo sio kosa. Ninapojiuliza mimi ni how comes wamekuja na hii option wakati wao ni watu wanaoisoma nchi kila kukicha na kujua kila kitu kuhusu hii nchi? Najiuliza why waje na uchaguzi huu wakati wanalipwa kusoma na kufuatilia siasa za dunia na wanajua wapi dunia inaenda alafu wanakuja na ushauri huu wa huyu mtu ambaye kweli sio mbaya ila kwa maslahi mapana ya nchi huko mbeleni haonekani kufit???
 
Hii ndio jf ya Zamani , sio kupiga kelele sijui ukawa sijui mi team membe , team lowassa , tatizo kubwa kwa sasa Tanzania ni system haifanyi kazi ipasavyo, kuna uwezekano mkubwa system imeharibiwa ili viongozi waendelee kufanya mambo yao , kuna wazalendo wengi sana kwenye system ya nchi hii, ila wanakandamizwa na viongozi wa vyombo Vya usalama kulinda maslahi yao ya kisiasa huu ndio ukweli. Pinda, membe, makamba,chikawe,Dr mahiga,Dr kitine wote ni zao la hii system . miaka 50 iliyopita kweli tumekosea , sasa miaka 50 ijayo kwa kweli tujipange , system hapa ndio inatakiwa ufanye kazi, ni lazima tuwape pongezi kwenye upande wa ulinzi unapoona Kenya wanapambana na alshabab wanashindwa na sisi tupo na amani ujue Jamaa wapo kazini lakini dunia ya Leo ni tofauti tunahitaji system inayoweza kutupa rais ambaye atatusaidia kama nchi sio rais aliyeonga viongozi wa system wenyewe mnawajua au rais mpole tunahitaji mtu atakayeijenga system ili vitu vingine vifanye kazi sio kuiua ili yeye na familia yake watajirike na Rafiki zake inauma sana aiseee , system ndio inakabidhi nchi kwa mtu vyama Vya upinzani kuchukua nchi ni mpaka hawa Jamaa wakabidhi nchi , ndio maana wakiona wanayemtaka hapiti wanachakachua , mtaimba ukawa mpaka mwaka 2050 kama Jamaa hawa wapi nchi hamtapewa , hapa ndio panatakiwa marekebisho , kuna thread humu pasco kaelezea umuhimu wa marando kwa chadema , tunahitaji system kuna ambayo itajua gas kiasi gani inazalishwa , itasaidia tpdc kupata tenda kuuza gesi nje , itafanikisha uchumi usonge mbele sio kutoa watu kucha na kudhoofisha system ili muibe , narudia wazalendo wapo wengi kwenye system ila inabidi wapewe nafasi na system kwa kweli waweke uzalendo tupate rais mzuri
 
Hii ndio jf ya Zamani , sio kupiga kelele sijui ukawa sijui mi team membe , team lowassa , tatizo kubwa kwa sasa Tanzania ni system haifanyi kazi ipasavyo, kuna uwezekano mkubwa system imeharibiwa ili viongozi waendelee kufanya mambo yao , kuna wazalendo wengi sana kwenye system ya nchi hii, ila wanakandamizwa na viongozi wa vyombo Vya usalama kulinda maslahi yao ya kisiasa huu ndio ukweli. Pinda, membe, makamba,chikawe,Dr mahiga,Dr kitine wote ni zao la hii system . miaka 50 iliyopita kweli tumekosea , sasa miaka 50 ijayo kwa kweli tujipange , system hapa ndio inatakiwa ufanye kazi, ni lazima tuwape pongezi kwenye upande wa ulinzi unapoona Kenya wanapambana na alshabab wanashindwa na sisi tupo na amani ujue Jamaa wapo kazini lakini dunia ya Leo ni tofauti tunahitaji system inayoweza kutupa rais ambaye atatusaidia kama nchi sio rais aliyeonga viongozi wa system wenyewe mnawajua au rais mpole tunahitaji mtu atakayeijenga system ili vitu vingine vifanye kazi sio kuiua ili yeye na familia yake watajirike na Rafiki zake inauma sana aiseee , system ndio inakabidhi nchi kwa mtu vyama Vya upinzani kuchukua nchi ni mpaka hawa Jamaa wakabidhi nchi , ndio maana wakiona wanayemtaka hapiti wanachakachua , mtaimba ukawa mpaka mwaka 2050 kama Jamaa hawa wapi nchi hamtapewa , hapa ndio panatakiwa marekebisho , kuna thread humu pasco kaelezea umuhimu wa marando kwa chadema , tunahitaji system kuna ambayo itajua gas kiasi gani inazalishwa , itasaidia tpdc kupata tenda kuuza gesi nje , itafanikisha uchumi usonge mbele sio kutoa watu kucha na kudhoofisha system ili muibe , narudia wazalendo wapo wengi kwenye system ila inabidi wapewe nafasi na system kwa kweli waweke uzalendo tupate rais mzuri
Ni kweli kabisa mkuu hii inaitwa Home of Great Thinkers na siku zote great thinkers ndo wanafanyaga vitu vya namna hii na sio kujadili team fulani au team fulani. Ni hatari sana kwa nchi na taifa pale kwenye forum inayoheshimika watu wanaweka ushabiki usio na maana. Kuna nchi zinajijenga vizuri sana kisystem na sasa wanaanza kuona matunda yake mf. Rwanda. Tanzania lazima tuamke,tukumbuke ni wapi tulikosea na tuanze kupajenga upya na sehemu kubwa ya kuijenga kwa kweli ni kwenye system. Nchi yoyote bila kuwa na system imara inayofanya kazi kwa weredi lazima iyumbe na pale kwenye system imara huna hata mashaka ya kumpa nchi kichaa kwa sababu pamoja na ukichaa wake system inakuwa imeshaweka misingi imara na nchi itaenda.
 
Huu mfumo wa chama tawala kuwa ndo intelligence network ya nchi ndo umezisambaratisha nchi nyingi za kijamaa kiuchumi. Pamoja na kuwa tunafuata sasa mfumo was uchumi was soko (ubepari) structures zetu bado ni za kijamaa. Bado viongozi wengi wanakitumia chama kama ngao ya kuwalinda wakati wanapo plunder huko serikalini. Huu mfumo, ukijumlisha na mediocre leaders yaani ni kama kuweka pamoja petroli na moto. Wenye kufuatilia mambo yanavyoenda ndani ya nchi hii watakuwa wanajua kuwa in fact CCM ndo intelligence yetu. Kwa hiyo mess tunayoiona ccm (matapeli kujimilikisha nchi kwa kulindwa na chama au intelligence). Wizi na ufisadi mkubwa umeanzia huko kwenye chama. Kwa kuwa chama ndo intelligence na viongozi wanatokea huko hakuna wa kumsaidia mWingine. Mfumo wa chama kushika hatamu usipovunjwa nchi hii hatutoki na kitakachofuata ni kuanguka kama wajamaa wote walivyoanguka.

Na chama kushika hatamu kwa kudhibiti intelligence haitaweza kuvunjwa bila kukitoa chama kilichopo madarakani. Kwa kifupi tuko kwenye vicious cycle na kuivunja hiyo tunahitaji muujiza. Muujiza wenyewe ni kuwa atokee kiongozi was upinzani atakayekuwa so strong and unwavering kuweza kuzivunja networks za mifumo ya kijamaa. Hii haitakuwa kitu rahisi. Tulipo ni kwenye auto pilot ya self destruction ambayo ndio fate ya mifumo yote ya kijamaa. No hope.
 
Huu mfumo wa chama tawala kuwa ndo intelligence network ya nchi ndo umezisambaratisha nchi nyingi za kijamaa kiuchumi. Pamoja na kuwa tunafuata sasa mfumo was uchumi was soko (ubepari) structures zetu bado ni za kijamaa. Bado viongozi wengi wanakitumia chama kama ngao ya kuwalinda wakati wanapo plunder huko serikalini. Huu mfumo, ukijumlisha na mediocre leaders yaani ni kama kuweka pamoja petroli na moto. Wenye kufuatilia mambo yanavyoenda ndani ya nchi hii watakuwa wanajua kuwa in fact CCM ndo intelligence yetu. Kwa hiyo mess tunayoiona ccm (matapeli kujimilikisha nchi kwa kulindwa na chama au intelligence). Wizi na ufisadi mkubwa umeanzia huko kwenye chama. Kwa kuwa chama ndo intelligence na viongozi wanatokea huko hakuna wa kumsaidia mWingine. Mfumo wa chama kushika hatamu usipovunjwa nchi hii hatutoki na kitakachofuata ni kuanguka kama wajamaa wote walivyoanguka.

Na chama kushika hatamu kwa kudhibiti intelligence haitaweza kuvunjwa bila kukitoa chama kilichopo madarakani. Kwa kifupi tuko kwenye vicious cycle na kuivunja hiyo tunahitaji muujiza. Muujiza wenyewe ni kuwa atokee kiongozi was upinzani atakayekuwa so strong and unwavering kuweza kuzivunja networks za mifumo ya kijamaa. Hii haitakuwa kitu rahisi. Tulipo ni kwenye auto pilot ya self destruction ambayo ndio fate ya mifumo yote ya kijamaa. No hope.
Asante mkuu wa mchango wako murua. Ila kuwa na structures za kijamaa sio tatizo kubwa sana, mbona nchi kama China pamoja na kubadirika kutoka uchumi wa kikomunist hadi wa kibepari ila system yao inaonekana kuimarika zaidi na kufanya vizuri zaidi hadi China inazidi kupaa kiuchumi kila siku na kule China still kuna one party system?
Ninachokiona Tanzania ni kuwa ni kama kuna sehemu Sytem yetu imelala kama sio kufa na hiyo sehemu ni kwenye huo upande wa kupanga mipango na mikakati madhubuti kuhusu siasa na uchumi na ndo mana nchi yetu imekuwa inayumba sana hasa kwenye kupata viongozi bora wenye maono katika kuifanya nchi iweze kucompete vizuri kwenye dunia hii ya ushindani. Nakubaliana na wewe pia kuwa inawezekana kuna baadhi ya watu wanaififisha kwa maslahi yao binafsi na ninavoona kwa maslahi mapana ya nchi lazima system iamue kujiweka sawa kwa kuwaondoa na kufanya kazi zake vizuri ili iweze kutimiza majukumu yake vizuri.
 
  • Thanks
Reactions: DSN
Naamini wewe kuna kitu unacho cha pekee umereta uchambuzi ambao ni kinga ya ccm na ninawashauri wenye nafasi zao ndani ya ccm wasome huu uzi na usitoke humu mapema kwa faida yao,kiukweli na nawashauri wazunguke mjini na vijijini wapate maoni,huyu jamaa anasifa lkn tanzania ya sasa sio aina ya rais wanaemtaka na pia watu hawamjui kabisa,pia wasje wakajidanganya kufananisha namna mkapa alivyoingia madarakani na hali ya sisa za sasa,kama ni system ndo imempendekeza wajipange vizuri viginevyo watatumia nguvu nyingi kumpeleka ikulu au hata kushindwa kabisa pili ccm watapoteza viti vingi vya wabunge kama hawatampitisha rais ambaye anaweza kuwaombea kura wabunge kitu mbacho bado itakuwa ni changamoto sn kwa ccm,kama mleta uzi kama anavyosema nenda kote ndani ya ccm ua ndani ya majimbo ya upinzani wanakwambia mtu pekee ambaye wanamkubali ni magufuli au kidogo muhongo lkn wengine wote wenye cv nzuri za elimu na utumushi lkn wapole hawakubaliki, angalizo watu wanamtaka mtu ambaye ni mkali wa kupambana na mfumo ulioshindikana na wakimkosa ndani ya ccm watamtafuta kwingine.kikwete na wale wenye nafasi lione hili mapema kabla hamjakosa usingizi maana mkapa alifanikisha mwk 1995 lkn siasa za wakati huo sio sawa na za sasa hiyo system mguvu ya umma itawashinda dunia imabadirika sana
 
Acha wajichanganye wenyewe sisi tukimkosa rais tunaemtaka ndani ya ccm tutamtafuta nje ya ccm ilimradi sifa yake ya kwanza iwe ni ukali wa kusimamia mambo maana hat huyu ramadhani alikua jaji mkuu akashidwa kuzuia rusha iliyoko kwenye idara ya mahakama,je ataweza mfumo mzima?
 

Similar Discussions

12 Reactions
Reply
Back
Top Bottom