Synthesizer
JF-Expert Member
- Feb 15, 2010
- 11,143
- 18,774
Kama watanzania tunategemea wanajeshi wetu, kutia ndani Polisi na Magereza, kujiendesha kwa namna ambayo inaonyesha wao ni vinara wa uaminifu (integrity). Hutarajii hata siku moja kuona kwamba Polisi na Magereza wanatumia udanganyifu katika kazi zao. Pale inapotokea wanafanya kazi kwa udanganyifu basi tutatilia shaka kila linalosemwa na Jeshi la Polisi au Magereza, na hata kukubali dhana ya kwamba kesi nyingi zinazofunguliwa Polisi ni za kubambika.
Katika suala la kesi inayomkabili Mbunge Lema dhidi ya Mkuu wa Mkoa wa Arusha Gumbo, askari wa Jeshi la Polisi wakishirikiana na wale wa Jeshi la Magereza, waliwafukuza waandishi wa habari waliokuwa katika kazi zao rasmi hapo Mahakamani wakidai kwamba walifanya hivyo kwa maagizo ya Mahakama. Waandish wa habari walipoenda kumuuliza Hakimu Rwezile anayesimamia kesi hii, alipinga tamko hilo la Polisi na Magereza akisema kwamba Mahakama haikutoa agizo hilo na alitambua kwamba waandishi wa habari walikuwa na barua za utambulisho kufanya kazi yao Mahakamani.
Kama ni kweli Polisi ma Magereza walitumia udanganyifu katika kuwafukuza waandishi wa habari, basi hiki ni kitendo cha kihuni sana kwa upande wa Polisi na Magereza. Na ina maana Tanzania tuna tatizo kubwa na la kutisha kwamba tuna Polisi na Magereza ambao kwao kusema uongo ni jambo dogo sana. Sasa ikiwa wao ndio walioaminiwa hata katika masuala ya kufungua mashitaka dhidi ya uhalifu na kutoa ushahidi mahakamani, tutaaminije kwamba hawafanyi hivyo kwa njia ya udanganyifu, ikiwa wanaonyesha wamezoe kusema uongo kirahisi tu?
Si jambo dogo, ni jambo linalotakiwa kutolewa maelezo na Wakuu wa Polisi na Magereza na hata Waziri wa Mambo ya Ndani.
Katika suala la kesi inayomkabili Mbunge Lema dhidi ya Mkuu wa Mkoa wa Arusha Gumbo, askari wa Jeshi la Polisi wakishirikiana na wale wa Jeshi la Magereza, waliwafukuza waandishi wa habari waliokuwa katika kazi zao rasmi hapo Mahakamani wakidai kwamba walifanya hivyo kwa maagizo ya Mahakama. Waandish wa habari walipoenda kumuuliza Hakimu Rwezile anayesimamia kesi hii, alipinga tamko hilo la Polisi na Magereza akisema kwamba Mahakama haikutoa agizo hilo na alitambua kwamba waandishi wa habari walikuwa na barua za utambulisho kufanya kazi yao Mahakamani.
Kama ni kweli Polisi ma Magereza walitumia udanganyifu katika kuwafukuza waandishi wa habari, basi hiki ni kitendo cha kihuni sana kwa upande wa Polisi na Magereza. Na ina maana Tanzania tuna tatizo kubwa na la kutisha kwamba tuna Polisi na Magereza ambao kwao kusema uongo ni jambo dogo sana. Sasa ikiwa wao ndio walioaminiwa hata katika masuala ya kufungua mashitaka dhidi ya uhalifu na kutoa ushahidi mahakamani, tutaaminije kwamba hawafanyi hivyo kwa njia ya udanganyifu, ikiwa wanaonyesha wamezoe kusema uongo kirahisi tu?
Si jambo dogo, ni jambo linalotakiwa kutolewa maelezo na Wakuu wa Polisi na Magereza na hata Waziri wa Mambo ya Ndani.