Kama ni Demokrasia ya JF.. Piga kura yako: Wengi wape

Mzee Mwanakijiji

Platinum Member
Mar 10, 2006
33,462
39,928
Bila ya shaka mmeanza kuona pembeni kuna sanduku la Kura. Swali la Msingi ni kuwa Kuendelea na habari binafsi za ngono za viongozi ambazo hazihusishi uvunjaji wa sheria au kuingilia utendaji wao wa kazi hapa JF. Chukua msimamo na kura za wengi basi ndio wapewe na uamuzi wao uheshimiwe. Kwa vile JF ni eneo la demokrasia ambapo panastahili kuwa na heshima yake basi tuamue suala hili kwa kupiga kura na uamuzi wowote wa walio wengi uheshimiwe.

M. M
 
piga kura na songa mbele... we hujaona hilo bandiko hapo pembeni... ? au ukiwa Underground ndiyo huoni?
 
Bila ya shaka mmeanza kuona pembeni kuna sanduku la Kura. Swali la Msingi ni kuwa Kuendelea na habari binafsi za ngono za viongozi ambazo hazihusishi uvunjaji wa sheria au kuingilia utendaji wao wa kazi hapa JF. Chukua msimamo na kura za wengi basi ndio wapewe na uamuzi wao uheshimiwe. Kwa vile JF ni eneo la demokrasia ambapo panastahili kuwa na heshima yake basi tuamue suala hili kwa kupiga kura na uamuzi wowote wa walio wengi uheshimiwe.

M. M

naomba nifafanuliwe ju ya huu usemi usemao ngono za viongozi ambazo hazihusishi uvunjaji wa sheria au kuingilia utendaji wao wa kazi.

Je kuna mifano ya ngono zinazo vunja sheria ?

Vile vile,Kuna ngono zinazoingilia utendaji wa kazi?
 
Kura zitaendelea kupigwa hadi lini? Kuna kikomo cha muda au idadi ya wapiga kura?
 
Mwkjj,
Hiyo ni nyingine ktk nyingi q'nable & losing position unachukua bila kutumia fikra 'sahihi' zako kama kweli unazo!! Kula itapigwa vipi na kuwa fair, ilihali inajulikana kwamba kuna lukuki la memberz hapa ambao wana id's zaidi ya moja? Kura hizi zitapigwa kwa muda gani? Ni asilimia gani minimum ya members wanaotakiwa kupiga kura, ili matokeo hayo yawe halali?

Na maswali mengi mengine!!! Wewe ama kweli umeanza kuleta vioja na hiyo janja yako ya "kwapa kunuka bila kidonda." Unadhani kwamba umekomaa, lakini "sisi" vyongo viona mbali, hasa mie nimeona fatal weaknesses kwa upande wako ktk siku hizi chache zilizopita... Moja wapo ni upofu wako wa makusudi/wakujitakia wa kutokuona kwamba ngono ni hoja halali ktk midani za kisiasa!! Si tu kwamba ni halali bali kwa wale wanaokuwa na maadili ni winning tool popote pale dunia.

Sina muda, mambo ya ED friday night... Lakini whatever itakavyokuwa matokeo ya kura hii hayatakuwa halali, yatakuwa yapo tainted, na badala ya kuboresha kama myopic minded wanavyodhani itakuwa a total opposite!!!! Watu hapa inabidi tu wawe civil, watu wajifunze to agree to disagree... Mstari lazima uchorwe, na tofauti ziwe za dhahiri badala ya viini macho.

UPINZANI Tanzania unashindwa mara nyingi kwasababu wananchi hawaoni tofauti kati yake na CCM. Hii ni kimaadili ya kiserikali na yale ya kijamii. Mbowe fuska, Kikwete fuska, wote wawili pia mafisadi, wewe unafikiri mwisho wa siku nani atachaguliwa? Lazima tofauti ziwepo, wanaohitajika ni watu safi!!! Hata kwa mungu ngono ni dhambi kubwa kushinda kura rushwa au ufisadi wa kusaini mkataba mbovu!!! Ebo, where is the ambiguity? I go nuts kwamba watu hawaelewi kitu simple kama hii.

Ufuska wa viongozi ni halali kuzungumziwa ktk hii political battle kama mabadiliko ya kweli yanategemewa!!!!! Cheerz, weekend njema everybody. American Gangster, now playin' in the theatre near you!! Adios, muchas gracias.
 
Mwkjj,
Hiyo ni nyingine ktk nyingi q'nable & losing position unachukua bila kutumia fikra 'sahihi' zako kama kweli unazo!!.

mhh yaani siamini hii lugha ni kwa mtu anayejiita mstaarabu hapa kwenye forum. Wewe nawe uko flawed too ingawa unajisifia day after day hapa.

Kula itapigwa vipi na kuwa fair, ilihali inajulikana kwamba kuna lukuki la memberz hapa ambao wana id's zaidi ya moja?. Kura hizi zitapigwa kwa muda gani? ni asilimia gani minimum ya members wanaotakiwa kupiga kura, ili matokeo hayo yawe halali? Na maswali mengi mengine!!!.

kupiga kura haihitaji uwe member, unapiga tu hiyo kura wewe hayo ya watu kuwa na ID zaidi moja yatahusika vipi?

Wewe ama kweli umeanza kuleta vioja na hiyo janja yako ya "kwapa kunuka bila kidonda." Unadhani kwamba umekomaa, lakini "sisi" vyongo viona mbali, hasa mie nimeona fatal weaknesses kwa upande wako ktk siku hizi chache zilizopita..............

kujipatia misifa tu ya bure. watu makini husifiwa na sio kujisifu kuwa wao ni makini.... geeeeez!

Moja wapo ni upofu wako wa makusudi/wakujitakia wa kutokuona kwamba ngono ni hoja halali ktk midani za kisiasa!!. Si tu kwamba ni halali bali kwa wale wanaokuwa na maadili ni winning tool popote pale dunia.

kumekuwa na thread zaidi ya tatu za ngono hapa kwenye siasa na wala hujaonekana ukichangia. Ulilia kaa mtoto kuwa thread ya Mbowe irudishwe na iriporudi hujachangia chochote zaidi ya kujisifia all the time kuwa wewe unajua kuliko mkjjj. Kama Mkjj ndio standard yako ya mafanikio mbona umechemsha.

Stand up like a man ufanye unachotaka na kupenda sio kulialia all the time...... unatia huruma sasa!

Sina muda, mambo ya ED friday night.....lakini whatever itakavyokuwa matokeo ya kura hii hayatakuwa halali, yatakuwa yapo tainted, na badala ya kuboresha kama myopic minded wanavyodhani itakuwa a total opposite!!!!.

unamtisha nani sasa kuwa huna muda, naona ushakuwa kama Mchambuzi the quiter moran maasai. Unaquit na kuanza kulia to hovyo. stop whining damn it!

Watu hapa inabidi tu wawe civil, watu wajifunze to agree to disagree........mstari lazima uchorwe, na tofauti ziwe za dhahiri badala ya viini macho.

mbona unachukua higher point sana as if wewe ndio una elimu au ujuzi dhani everybody else hapa. Kila mtu anaplay part kama memba wa forum. mkjj kapresent hilo la kura na wewe unaweza kuleta la kwako. Come on too much whining sasa!

UPINZANI Tanzania unashindwa mara nyingi kwasababu wananchi hawaoni tofauti kati yake na CCM. Hii ni kimaadili ya kiserikali na yale ya kijamii.........Mbowe fuska, Kikwete fuska, wote wawili pia mafisadi, wewe unafikiri mwisho wa siku nani atachaguliwa? Lazima tofauti ziwepo, wanaohitajika ni watu safi!!!

haya ni maoni yako na sio consesus ya hitimisho la professional study ambayo sasa inabidi ifuatwe.

Hata kwa mungu ngono ni dhambi kubwa kushinda kura rushwa au ufisadi wa kusaini mkataba mbovu!!! ebo, where is the ambiguity? I go nuts kwamba watu hawaelewi kitu simple kama hii.........

Wewe mwenyewe umekaaa kimya huongelei hayo mambo ya ngono na unataka nani ayaongelee badala yako. mbona una nafasi sawa tu hapa ya kuanzisha thread zako za ngono na ukaziongelea!

ufuska wa viongozi ni halali kuzungumziwa ktk hii political battle kama mabadiliko ya kweli yanategemewa!!!!!.
Cheerz, weekend njema everybody. American Gangster, now playin' in the theater near you!!. Adios, muchas gracias.

Maoni yako yanaweza kutofautiana na ya wengi hapa. Mbona hutaki watu wafanye choice? Unadai demokrasia na ukipewa unaanza kulia ohhh mawazo yako ni bora kuliko ya wengine! gooooosh
 
YNIS, hutaki kilichoulizwa piga kura, porojo nyingi za nini? Mwafrika.. once again you amazes me (I know.. in so many other ways..).
 
MwKike,
Rxn yako ilikuwa xpected........sina haja ya malumbano, nimewakuta hapa JF kwahiyo mnaweza kuendelea na routine yenu!!. Kila laheri ktk kura hizi hopefully something good will come out of it!! Weekend njema, Celtics imeanza msimu kwa kishindo Wizards of Washington were no match.
 
YNIS, hutaki kilichoulizwa piga kura, porojo nyingi za nini? Mwafrika.. once again you amazes me (I know.. in so many other ways..).

Honestly, mie kura sipigi kwasababu sioni maana yake zaidi ya kuchora mistari miongoni mwa members. Uzuri wako ni kuwa huchukulii criticism personal, MAYBE and maybe sikubaliani na wewe lakini hiyo ni big plus kwa upande wako!!.
Weekend Njema kaka.
 
Uwongo ukubaliwao na wengi katu hautabadili Thamani na umuhimu wa ukweli ukubaliwao na wachache.

kwa hiyo wachache wapewe haki yao ya kujadili, na wengi wapewe haki yao ya kusikiliza/kutokusikiliza/kuchangia/kutokuchangia.

cha muhimu ni kusisitiza hoja na si vioja kama baadhi ya members badala ya kuchangia hoja wakageuza picha ndo hoja zenyewe

kura ya kuua uhuru na demokrasia ni kura batili.

ni sawa na kura ya maoni ya kuulizia jamhuri ya muungano wa Tanzania iendelee kuwepo au isiwepo bila kuonyesha kwamba una lengo la kuunda nyingine iliyo bora zaidi
 
Mi naona kura zinaendelea, ubishi au ubishani havitasaidia! Hapa kwenye JF, napo pameshakuwa kama kambi fulani ya siasa, kwani hatuangalii tena hoja za membaz bali tumeshaanza hata kujipa, kupewa, au kupeana 'virtual' vyeo!!! Na kama kuna mbinu za kujipachika majina lukuki na kupiga kura lukuki ili kushindisha hoja, basi JF nayo itakuwa imekumbwa na ugonjwa ule ule wa UZANDIKI kama wa wanasiasa!
Eneweyz, mi nshapiga kura yangu! Napenda kuwashauri au kuwakumbusha tu ndugu zangu wanaoendelea kupiga kura humu kuwa MAISHA YA KIONGOZI YEYOTE, KWA ASILIMIA KUBWA, SI MAISHA BINAFSI KAMA YA KINA MASULUPWETE! Matendo yake wakati wote, yatachukuliwa kuwa ndio kioo cha uongozi wake na utendaji wake katika utumishi wa umma. Hayatakiwi yawe siri au yakwepe kurunzi la macho ya umma anaoutumikia!
 
Kuendelea na habari binafsi za ngono za viongozi ambazo hazihusishi uvunjaji wa sheria au kuingilia
Zihamishwe kwenda kwenye Udaku
Zipelekwe kwenye Vibweka vya Wakubwa
Ziachwe hapa hapa kwenye siasa
Zifutwe kabisa na zipelekwe kwenye zilizofungwa.


View results

Kwanza katika habari zilizoletwa kuhusiana na ngono za viongozi ni zipi ambazo hazihusishi uvunjaji wa sheria?.

Inabidi tupigie kura kitu ambacho kipo, na si kupigia kura kitu ambacho hakipo.

Iwapo tutakubaliana kwamba UGONI ni kosa kisheria basi poll hiyo hapo juu ni batili,
 
Kwanza katika habari zilizoletwa kuhusiana na ngono za viongozi ni zipi ambazo hazihusishi uvunjaji wa sheria?.

Inabidi tupigie kura kitu ambacho kipo, na si kupigia kura kitu ambacho hakipo.

Iwapo tutakubaliana kwamba UGONI ni kosa kisheria basi poll hiyo hapo juu ni batili,

cha kushangaza ni kwamba, poll haijauliza hicho kitu !(kama ugoni ni batili au la )
 
Napendekeza kura zifungwe siku ya Jumatatu Jioni au Jumanne. Nyie pigeni kura, nani aliwahi kusema kuwa kupiga kura kumewahi kuwaridhisha watu wote? Kama watu wengi wataona hivi basi iwe hivi kama itakuwa vile basi itakuwa vile, kwanini mnahukumu matokeo kana kwamba yamefikia kikomo.
 
...Swali la Msingi ni kuwa Kuendelea na habari binafsi za ngono za viongozi ambazo hazihusishi uvunjaji wa sheria au kuingilia utendaji wao wa kazi ...
M. M

Mzee Mwanakijiji,

Naomba ufafanuzi hapo nilipokolezea... what exactly do you mean? Vilevile kumbuka kuna tofauti kati ya habari binafsi za ngono za viongozi na ufuska? Sasa kama ufuska siyo subset ya ufisadi tutakuwa tunatwanga maji kwenye kinu!
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom