Zak Malang
JF-Expert Member
- Dec 30, 2008
- 5,404
- 233
Hebu tujaribu kufanya hypothesis kidogo. Hypothesis huruhusiwa iwapo kunatokea mtiririko wa matukio ambayo misingi yake inafanana.
Iwapo Lewis Makame mwenyekiti wa NEC angekuwa amejaliawa ujasiri, uadilifu na nguvu na kuwa mkweli na akamtangaza Dr Slaa kuwa ndiye mshindi wa urais katika uchaguzi uliyopita, uhakika ni kwamba JK na genge lake wangemnyanganya Dr Slaa ushindi, kwa staili ya Gbagbo.
Mimi nadhani hapo hakuna mjadala:
Kwani Tanzania ni nchi ya Kiafrika ambayo kamwe haimo katika nchi zile zenye kufanya chaguzi za haki.
Tumeona jinsi CCM walivyonyanganya ushindi katika majimbo kadha ya Ubunge, tena bila hata ya aibu!
Tumeona chaguzi za umeya zinavyohujumiwa kavu kavu!
Tumeona jinsi Tido alivyohujumiwa eti tu kwa kuonekana kutenda haki kwa vyama vya upinzani!
Sasa katika hali ya namna hii, CCM kweli ingekubali Dr Slaa kuapishwa?