Kama Mwigulu na Lugola waliokuwa wanaivaa bendera ya Taifa uzalendo umewashinda hadi kutumbuliwa sishangai ya Kigwangalla na Kabudi kutaka kujiuzulu

johnthebaptist

JF-Expert Member
May 27, 2014
83,792
141,685
Natafakari tu zile mbwembwe za Mh Mwigulu na mwenzie Kangi Lugola kuivaa bendera ya taifa kama kielelezo cha uzalendo uliotukuka.

Kwa bahati nzuri wawili hawa walipitishwa katika kipimo kimoja kuthibitisha uzalendo wao na wote wamefeli na hawaivai tena ile bendera ya taifa wamebakia kuikodolea macho tu ikiwa kwenye mlingoti.

Kwa namna Mwigulu na Lugola walivyofeli pale Wizara ya mambo ya ndani sishangazwi kabisa na kauli za Mawaziri wengine Dr Kigwangala na Prof Kabudi kwamba kuna "nyakati" majaribu yaliwazidi wakaomba kikombe kiwaupuke lakini Mungu akawapa ujasili wakasonga mbele.

Jumamosi njema.

Maendeleo hayana vyama!
 
huu uzi umeandikwa kimbea tu, au una chuki na hao viongozi ? acha watu wapige kazi
pia watanzania tuache tabia ya kumsifia jiwe anapofukuza kazi watu hovyo (siongelei ya lugola na wenzie)


Sent from my iPhone using JamiiForums
 
Walimwengu hamna dogo aisee..wewe leo hii ndo unawasimanga makada wenzio?

I wish JPM ajue kwamba amezungukwa na wanafiki wanaotaka kula tuu. Hata yeye akitoka atabezwa kama watangulizi wake wanavyobezwa! Tena yeye watambeza Zaidi..tena wale waliofaidika na utawala wake...

Na hii ya kutofuata sheria itawatafuna wengi. Tuombe tuishi Maisha marefu tuone wanavyomkana JPM.....Mchana kweupeeee...

Kwa Tanzania ya leo sioni kama kuna mtu aliye sincere na taifa letu. Labda JPM (hii ni topic nyingine). Lakini as a matter of fact wengi wanaopata fursa za uongozi wanataka kula. Nothing more nothing less.

Na wengi wameshajifunza mchezo. Total surrender kwa aliye madarakani. Akiondoka unaanza upya! Tumeyaona na yanajirudia kila siku!

Ukiona leo mtu ana dare kuwakosoa CCM (Nape et al) ni kwamba amefungiwa nje ya geti au ameondolewa ndani ya ukumbi!
 
Kauli ya kabudi ni ya hovyo mwanaume hupaswi kujishusha vile ama kujiona mnyonge.Bado tuna safari ndefu endapo professor mbobezi alinalilia vile wanafunzi wake wajifunze nini? Anapaswa kupumzishwa kwa matokeo duni suluhi huku akidai we did our best, Trillion zetu 490!? Tzs, zimeota mbawa, na hatuna maamlaka kuhoji tena chapter clossed.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kwahiyo zile noah zetu tunapata lini? Jana wakati mnawalamba miguu mabeberu sijasikia mkiongelea hili.
 
Walimwengu hamna dogo aisee..wewe leo hii ndo unawasimanga makada wenzio?

I wish JPM ajue kwamba amezungukwa na wanafiki wanaotaka kula tuu. Hata yeye akitoka atabezwa kama watangulizi wake wanavyobezwa! Tena yeye watambeza Zaidi..tena wale waliofaidika na utawala wake...

Na hii ya kutofuata sheria itawatafuna wengi. Tuombe tuishi Maisha marefu tuone wanavyomkana JPM.....Mchana kweupeeee...

Kwa Tanzania ya leo sioni kama kuna mtu aliye sincere na taifa letu. Labda JPM (hii ni topic nyingine). Lakini as a matter of fact wengi wanaopata fursa za uongozi wanataka kula. Nothing more nothing less.

Na wengi wameshajifunza mchezo. Total surrender kwa aliye madarakani. Akiondoka unaanza upya! Tumeyaona na yanajirudia kila siku!

Ukiona leo mtu ana dare kuwakosoa CCM (Nape et al) ni kwamba amefungiwa nje ya geti au ameondolewa ndani ya ukumbi!
Bwashee kwenye siasa hasa za chama makini kama CCM hakuna kusimangana bali watu wanaelezana ukweli.

Kwenye vyama vidogo vidogo ndio wanasenyengana kama walivyomsengenya Mwambe na Sumaye!
 
Walimwengu hamna dogo aisee..wewe leo hii ndo unawasimanga makada wenzio?

I wish JPM ajue kwamba amezungukwa na wanafiki wanaotaka kula tuu. Hata yeye akitoka atabezwa kama watangulizi wake wanavyobezwa! Tena yeye watambeza Zaidi..tena wale waliofaidika na utawala wake...

Na hii ya kutofuata sheria itawatafuna wengi. Tuombe tuishi Maisha marefu tuone wanavyomkana JPM.....Mchana kweupeeee...

Kwa Tanzania ya leo sioni kama kuna mtu aliye sincere na taifa letu. Labda JPM (hii ni topic nyingine). Lakini as a matter of fact wengi wanaopata fursa za uongozi wanataka kula. Nothing more nothing less.

Na wengi wameshajifunza mchezo. Total surrender kwa aliye madarakani. Akiondoka unaanza upya! Tumeyaona na yanajirudia kila siku!

Ukiona leo mtu ana dare kuwakosoa CCM (Nape et al) ni kwamba amefungiwa nje ya geti au ameondolewa ndani ya ukumbi!
JPM mwenyewe mnafiki.

Anamfukuza kazi Waziri kwa kuingia mikataba bila kufuata bajeti wala idhini ya bunge.

Wakati yeye mwenyewe JPM ni kinara wa kufanya manunuzi makubwa bila kufuata bajeti, tenda wala idhini ya bunge.

Sasa kama si unafiki hicho alichofanya ni nini?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Bwashee kwenye siasa hasa za chama makini kama CCM hakuna kusimangana bali watu wanaelezana ukweli.

Kwenye vyama vidogo vidogo ndio wanasenyengana kama walivyomsengenya Mwambe na Sumaye!

Leo hii Sumaye akirudi CCM atapewa cheo na utakuwa unamtukuza hivo hivo......Slaa mlimsimanga sana..alivyorudi nyumbani akakumbatiwa..leo hii mnamwita mwanadiplomasia nguli..hahahahah

Vijana wa CCM MJIPANGE...Ingieni kwenye siasa mkiwa mmeshiba. Mkienda na njaa kama mlivyo sasa mtapata taabu sana!
 
Leo hii Sumaye akirudi CCM atapewa cheo na utakuwa unamtukuza hivo hivo......Slaa mlimsimanga sana..alivyorudi nyumbani akakumbatiwa..leo hii mnamwita mwanadiplomasia nguli..hahahahah

Vijana wa CCM MJIPANGE...Ingieni kwenye siasa mkiwa mmeshiba. Mkienda na njaa kama mlivyo sasa mtapata taabu sana!
Bwashee CCM hakuna njaa kama hapo Ufipa...... Umemuona Mwita Waitara alivyonawiri baada ya kuachana na " mataputapu" ya hapo kwenu Ufipa?!
 
Back
Top Bottom