Lunyungu
JF-Expert Member
- Aug 7, 2006
- 8,873
- 1,894
Kwa mara ya 3 mfulizo kwa nyakati tofauti nimefika katika kituo cha Polisi cha Buguruni na Selandar Bridge. Ndugu IGP, napenda ujue kwamba baada ya Rais kuugawa Mkoa wa Dar na kuweka madoiko kibao kwa jina la usalama, nk, which I have no problem with, imepelekea maonevu na rushwa kushamiri. Ukiingia Buguruni unaomba rushwa wazi wazi hata kama hakuna jambo la kukufanya ufikie hatua hiyo. Ni vigumu kusema nani kaomba rushwa lakini ninaweza kutoa baadhi ya watu wanaohusika na vituko na huku uongozi unajua yanayojiri.
Ndugu IGP, nimeshuhudia mtu anahojiwa behind the Counter ya polisi akiwa chini ya Ulinzi lakini anapigwa na polisi zaidi ya mmoja openly kisa anakataa kutaja jina lake akidai awepo Hakimu kama mlinzi wa amani ama ndugu zake ama Mwansheria. I went far na kuhoji kwa nini alikuwa anapigwa akiwa hakati amri ya kuwekwa chini ya Ulinzi lakini majibu yalikuwa ni matusi kwangu hata bila ya kujua wanasema na nani.
Buguruni kuna uhuni mkubwa kiasi kwamba hata kumuona Mkuu wa Kituo ama OC CID na OCD ni big deals. Watu hukamatwa Buguruni na walio wakamata kwa kujenga mazingira ya rushwa huwaacha ndani na kuondoka kwa masaa mengi ndugu zao wakihaha kuwatafuta na wao wanasema wameenda lunch ama kunywa chai. Ukiwapigia simu wanakuita uende huko mkamalizane.
Je, Mwema, haya unayajua? Unajua walala hoi wanavyoteswa na kukamliwa senti zao na wao hutoa pesa kwa kuhofia na kuogopa kukaa ndani?
Ndugu IGP, nimeshuhudia mtu anahojiwa behind the Counter ya polisi akiwa chini ya Ulinzi lakini anapigwa na polisi zaidi ya mmoja openly kisa anakataa kutaja jina lake akidai awepo Hakimu kama mlinzi wa amani ama ndugu zake ama Mwansheria. I went far na kuhoji kwa nini alikuwa anapigwa akiwa hakati amri ya kuwekwa chini ya Ulinzi lakini majibu yalikuwa ni matusi kwangu hata bila ya kujua wanasema na nani.
Buguruni kuna uhuni mkubwa kiasi kwamba hata kumuona Mkuu wa Kituo ama OC CID na OCD ni big deals. Watu hukamatwa Buguruni na walio wakamata kwa kujenga mazingira ya rushwa huwaacha ndani na kuondoka kwa masaa mengi ndugu zao wakihaha kuwatafuta na wao wanasema wameenda lunch ama kunywa chai. Ukiwapigia simu wanakuita uende huko mkamalizane.
Je, Mwema, haya unayajua? Unajua walala hoi wanavyoteswa na kukamliwa senti zao na wao hutoa pesa kwa kuhofia na kuogopa kukaa ndani?