Chakaza
JF-Expert Member
- Mar 10, 2007
- 39,702
- 71,013
Wadau wa JF,
Mimi ni Mtanzania mpiga kura halali na 2015 nilimsikiliza huyu mweshimiwa nilipompa nafasi ya kusema sera za chama chake na yeye binafsi atazifanyia kazi namna gani.
Alinishawishi kwa mengi sana katika Afya, Elimu, miundombinu, ulinzi wangu, Uhuru wangu kulingana na Katiba, furaha na amani pia heshima ndani na nje ya nchi kama Mtanzania.
Kutokana na ahadi zake, nikampa ajira ya Urais kwa miaka 5 under probation, ili kama atathibitisha ubora nitampa 5 nyingine.
Sasa ni tofauti, sio kwamba hajafanya kitu, la hasha! Amefanya ya kutosha kama mwajiriwa lakini mengi sio kwa mipango kama nchi bali ameamua kutumia kichwa chake (one man show) na kutuvuruga.
Pili ameshindwa kabisa katika mambo muhimu kama Uhuru wa habari na kujieleza, ulinzi wa raia, Elimu, Ajira, heshima ndani na nje, mahusiano nk.
Kwa kushindwa kwake kutimiza wajibu nataka nimfukuze kazi 28 Oktoba, 2020. Je, ni lazima kumuandikia barua ya kusitisha ajira yake au nimpige kimya kimya kwa sanduku la kura?
Je, kama atatumia vibaya madaraka niliyompa 2015 na kutoheshimu maamuzi yangu ya sasa na aka ng'ang'ania hatoki napaswa kufanyaje kama mwajiri?.
Mimi ni Mtanzania mpiga kura halali na 2015 nilimsikiliza huyu mweshimiwa nilipompa nafasi ya kusema sera za chama chake na yeye binafsi atazifanyia kazi namna gani.
Alinishawishi kwa mengi sana katika Afya, Elimu, miundombinu, ulinzi wangu, Uhuru wangu kulingana na Katiba, furaha na amani pia heshima ndani na nje ya nchi kama Mtanzania.
Kutokana na ahadi zake, nikampa ajira ya Urais kwa miaka 5 under probation, ili kama atathibitisha ubora nitampa 5 nyingine.
Sasa ni tofauti, sio kwamba hajafanya kitu, la hasha! Amefanya ya kutosha kama mwajiriwa lakini mengi sio kwa mipango kama nchi bali ameamua kutumia kichwa chake (one man show) na kutuvuruga.
Pili ameshindwa kabisa katika mambo muhimu kama Uhuru wa habari na kujieleza, ulinzi wa raia, Elimu, Ajira, heshima ndani na nje, mahusiano nk.
Kwa kushindwa kwake kutimiza wajibu nataka nimfukuze kazi 28 Oktoba, 2020. Je, ni lazima kumuandikia barua ya kusitisha ajira yake au nimpige kimya kimya kwa sanduku la kura?
Je, kama atatumia vibaya madaraka niliyompa 2015 na kutoheshimu maamuzi yangu ya sasa na aka ng'ang'ania hatoki napaswa kufanyaje kama mwajiri?.