Kama Mkapa amekiri Majambazi ya EPA yapo, Rais wetu Magufuli aanze na hawa hata wajukuu wasitumie pesa hizi

Wana Jf,

Shahidi wa kwanza ambaye alishuhudia wizi mkubwa wa EPA yupi na ametaja kusikitishwa kwake na kitendo hiki. Ili asemehewe inabidi waliohusika na wizi huu wakamatwe kesi ianze upya. Shahidi wa pili no Dr. Balozii Slaa ambaye aliwatuhumu watu kadhaa bunge likawafanyia kazi, pia list of shame nayo ihusishwe ili wote waliochezea Mali za umma wazijejeshe au wafungwe

Kwa ufupi mzee wetu anapenda kuomba msamaa kwa yaliyotokea, lakini akumbuke kuwa ukienda kutubu kanisani unaambiwa urudishe ulichoiba na kuomba samahani. Kama ulizini basi unapigwa faini pale pale, kama uliua unapigwa faini pale pale, lakini matendo ya kuchukua kisicho chako lazima ukirudishe.

BWM anaweza kuja kuwa mtakatifu wa baadaye kama ameanza taratibu za kutubu, lakini pia matusi yake pia ayatubu maana kuita wapinzani ni kokoto, ni marofa haya hayavumiliki maana kuwaita watu wamungu majina mabaya hayaleti utukufu. Japokuwa kabla ya upinzani yeye alipewa support kubwa kuleta maendeleo ya kila sehemu.

Roho 22 zilizopotea pesa za manunuzi ya kitabu hiki wapelekewe wazazi, au familia zilizopotelewa na ndugu zao. Mwisho namtakia kutubu kwema na namwomba asitumike tena kwenye siasa, aache vyuma viumane vyenyewe kwani Muda wa kukutana na mhusika mkuu aliyetuumba unakaribia.
Mkuu tangu lini mwizi amkamate mwizi mwenzie? Tafakari
 
Yaani viongozi wetu wanashiriki kwenye wizi wa fedha za umma wakiwa wamekula kiapo cha kulitumikia taifa halafu wana gut ya kuandika hadi vitabu kutueleza jinzi walivyoibia nchi wakiwa madarakani na huku wakituita malofa tukitaka kuhoji hayo maovi yao. Mimi ndiye najisikia aibu kwa haya yaliyotenhenezewa kitabu.
 
Waziri Mkubwa na Mzito aliemnyeshwa Sumu Kipenzi cha Wanyonge Jana hakupewa Mwaliko wakati alikuwa Mtu muhimu kwenye utawala wa Mzee Mkapa wa miaka yote 10 na aligombea Urais 2005 but hakufurukuta

Huyo huyo Waziri alimkosa kosa Mkwere 2003 kule Znz kwenye Nec
Ni yule anayetoka jimbo moja na Mama Mary Nagu?. Basi ni mtu hatari sana.
 
soma hapa

Mkuu umewahi kuchukua muda wako na kutaka kujiridhisha Nyerere alisema Ujamaa ni mbaya na ulivurunda au kuharibu uchumi?

Umetumia makala ya Mwandishi wa Mwananchi ndugu Elias Msuya ambayo hata yeye nadiriki kusema hakuandika kwa weledi kwa kuweka nukuu, na kuonyesha rejea ya chanzo chanzo cha hizo nukuu ili kuthibitisha yale aliyo yaongea.

Nyerere aliandika TUJISAHIHISHE mapema sana mwanzoni mwa uongozi wake mwaka 1962 hata kabla ya Azimio la Arusha lililokuja kuimarisha sera za ujamaa zinazo tuhumiwa kuuwa au kuvuruga uchumi.
Pili uchumi wa Tanzania uliingia ktk misukosuko mikubwa sana na kudorora miaka mingi takribani zaidi ya miongo miwili(miaka 20) baada ya andiko la tujisahihishe. Na sio baada ya kuyumba uchumi, hivyo sio sahihi kutumia maelezo yaliyo ktk kitabu hicho kuhitimisha Nyerere alikili makosa ya Ujamaa ktk andiko hilo.

Eliasi Msuya ameonekana kuweka maoni yake binafsi ambayo hajayatetea kiataalamu kwa utafiti wenye kuweka vielelezo na viambatanishi.

Inavyoonekana huyo Ndugu Eliasi Msuya hakusoma au alisoma hakuelewa kuhusu andiko la Nyerere la TUJISAHIHISHE, na vilevile wewe umemnukuu vibaya Eliasi Msuya na kuweka hitimisho kwa mambo ambayo hajasema hivyo.

Tuna shida kubwa sana ktk uandishi wetu wa habari hapa Tanzania, kuna wakati tunaweka maoni binafsi na kuhukumu bila kufanya uchunguzi na kuweka mjadala ujadiliwe huku tukiwa na vielelezo sahihi.

Kwa kukusaidia wewe na wengine wengi nakuwekea kiunganisho au 'link' ya kupata andiko husika la NYerere ili usome mwenyewe kisha uje utoe maoni na hitimisho sahihi.
TUJISAHIHISHE-JK_Nyerere_May-1962
TUJISAHIHISHE-Kama ilivyo chapishwa katika Jamhuri Media
 
Kinga ya urasi iondolewe, haiwezekani watu walipigia kelele suala la EPA kumbe wezi wanajulikana na walikuwa na baraka zote toka kwa raisi ambae chama chake CCM ni moja ya majizi yaliyofaidika
 
Umeandika nini, hao kwani amewaua yeye, izo ela za kitabu hujasikia zinaenda wapi?
Hawa wachekeshaji vituko sana, kitabu chenyewe hajakisoma afu anaandika upupu, kuhusu mauaji mwenyewe yalimuumiza na yanamuumiza the way analaumiwa wakati wala hakuwepo, hicho ndo alichokisema.
 
Uhusiano ni Mkapa ndio aliruhusu wizi wa EPA kwa ahadi kwamba chama kitanufaika pesa za kampeni za uchaguzi mkuu uliyomuingiza Kikwete madarakani.

Mkapa kwenye kitabu chake ameandika kwamba anahisi alitumika na kusalitiwa. ( Na Daud Balali?)
miaka yote hii bado anahisi? wapelelezi wetu mahiri wako wapi? au napo kuna ule wimbo pendwa: upelelezi haujakamilika! hakuna sehemu kaongelea kifo cha huyo msaliti? au naye alizikwa baharini kama osama. ajabu mangwea anafia nje, maiti yake inaletwa na kuzikwa nyumbani kwao. balali anazikwa na maji! nchi ya vi-wonder.
 
Ameona kumbe kwenye ft 6 ataingia yeye kama yeye na kuna utawala mwingine huko anahitaji kuweka mambo sawa kabla hajafik huko
 
Kinga ya urasi iondolewe, haiwezekani watu walipigia kelele suala la EPA kumbe wezi wanajulikana na walikuwa na baraka zote toka kwa raisi ambae chama chake CCM ni moja ya majizi yaliyofaidika
Hili ndilo litakuwa suruhisho, waliohusika wafilisiwe kwani nao hawataona noma kwa kuwa mali haikuwa yao ni ya kiwizi wizi
 
Msajili wa vyama kwa nini mpaka sasa hajakifuta hiko chama cha CCM maana rais wa amekiri wametumia hela kwa WIZI kwenye kampeni yao.
 
Hawa wachekeshaji vituko sana, kitabu chenyewe hajakisoma afu anaandika upupu, kuhusu mauaji mwenyewe yalimuumiza na yanamuumiza the way analaumiwa wakati wala hakuwepo, hicho ndo alichokisema.
Una uelewa wowote kuhusu command in chief ni nini? Au umeamuwa tu kujambajamba?

Wale wanaohukumiwa kwenye mahakama za uhalifu wa kimataifa walishika bunduki kuuwa? Omar Bashir alishika bunduki kuuwa waandamanaji?

Puumbavuu kabisa.
 
Hawa wachekeshaji vituko sana, kitabu chenyewe hajakisoma afu anaandika upupu, kuhusu mauaji mwenyewe yalimuumiza na yanamuumiza the way analaumiwa wakati wala hakuwepo, hicho ndo alichokisema.
Hakuna haja ya kukisoma wakati alitakiwa awe amejipeleka mwenyewe mahakamani baada ya kuandika, alafu aombe adhabu yeyote kutoka kwa akimu aliyejitolea kumhukumu. lakini kinga ndizo uwapaviburi, miaka yote alikana ANNBEN, KIWIRA, RAMDA Hotel, RADA ya Chenge, Ndege yake Ilimfunga Basil Mramba, Profesa Mahalu na Pesa za Ubalozi wa Ital hadi kaitwa kutoa ushahidi kumnusuru. dhambi nyingi tu hata akikiri lakini taifa liliumia san hasa alipouza TBL na Nyumba za serikali.
 
TUNASUBIRI KITABU CHA KIKWETE, SIJUI ATASEMA NINI

Akiwa fair akaeleza kila kitu kuanzia mwanzo mpka mwisho kitavutia sana

Jk ana historia ya aina yake kwenye Siasa zetu na akiacha diplomasia akaweka kila kitu hewani kitakuwa gumzo sana
 
Wana Jf,

Shahidi wa kwanza ambaye alishuhudia wizi mkubwa wa EPA yupi na ametaja kusikitishwa kwake na kitendo hiki. Ili asemehewe inabidi waliohusika na wizi huu wakamatwe kesi ianze upya. Shahidi wa pili no Dr. Balozii Slaa ambaye aliwatuhumu watu kadhaa bunge likawafanyia kazi, pia list of shame nayo ihusishwe ili wote waliochezea Mali za umma wazijejeshe au wafungwe

Kwa ufupi mzee wetu anapenda kuomba msamaa kwa yaliyotokea, lakini akumbuke kuwa ukienda kutubu kanisani unaambiwa urudishe ulichoiba na kuomba samahani. Kama ulizini basi unapigwa faini pale pale, kama uliua unapigwa faini pale pale, lakini matendo ya kuchukua kisicho chako lazima ukirudishe.

BWM anaweza kuja kuwa mtakatifu wa baadaye kama ameanza taratibu za kutubu, lakini pia matusi yake pia ayatubu maana kuita wapinzani ni kokoto, ni marofa haya hayavumiliki maana kuwaita watu wamungu majina mabaya hayaleti utukufu. Japokuwa kabla ya upinzani yeye alipewa support kubwa kuleta maendeleo ya kila sehemu.

Roho 22 zilizopotea pesa za manunuzi ya kitabu hiki wapelekewe wazazi, au familia zilizopotelewa na ndugu zao. Mwisho namtakia kutubu kwema na namwomba asitumike tena kwenye siasa, aache vyuma viumane vyenyewe kwani Muda wa kukutana na mhusika mkuu aliyetuumba unakaribia.
Badala ya kuulizia au kutueleza namna gani tunaweza kukipata hicho kitabu na kinauzwaje wewe unaandika pumba tu.
 
Back
Top Bottom