Kama Mkapa amekiri Majambazi ya EPA yapo, Rais wetu Magufuli aanze na hawa hata wajukuu wasitumie pesa hizi

mgt software

JF-Expert Member
Nov 1, 2010
13,767
7,115
Wana Jf,

Shahidi wa kwanza ambaye alishuhudia wizi mkubwa wa EPA yupi na ametaja kusikitishwa kwake na kitendo hiki. Ili asemehewe inabidi waliohusika na wizi huu wakamatwe kesi ianze upya. Shahidi wa pili no Dr. Balozii Slaa ambaye aliwatuhumu watu kadhaa bunge likawafanyia kazi, pia list of shame nayo ihusishwe ili wote waliochezea Mali za umma wazijejeshe au wafungwe

Kwa ufupi mzee wetu anapenda kuomba msamaa kwa yaliyotokea, lakini akumbuke kuwa ukienda kutubu kanisani unaambiwa urudishe ulichoiba na kuomba samahani. Kama ulizini basi unapigwa faini pale pale, kama uliua unapigwa faini pale pale, lakini matendo ya kuchukua kisicho chako lazima ukirudishe.

BWM anaweza kuja kuwa mtakatifu wa baadaye kama ameanza taratibu za kutubu, lakini pia matusi yake pia ayatubu maana kuita wapinzani ni kokoto, ni marofa haya hayavumiliki maana kuwaita watu wamungu majina mabaya hayaleti utukufu. Japokuwa kabla ya upinzani yeye alipewa support kubwa kuleta maendeleo ya kila sehemu.

Roho 22 zilizopotea pesa za manunuzi ya kitabu hiki wapelekewe wazazi, au familia zilizopotelewa na ndugu zao. Mwisho namtakia kutubu kwema na namwomba asitumike tena kwenye siasa, aache vyuma viumane vyenyewe kwani Muda wa kukutana na mhusika mkuu aliyetuumba unakaribia.
 
Ukisikiliza kwa makini na ukazingatia kilichozungumzwa jana na kama sisi wote ni watu makini, basi sidhani kama CCM ilipaswa kuwepo madarakani.. Kulingana na kichozungumzwa ilitakiwa wafuasi wote wa CCM warudishe kadi zao na kuingia barabarani maana imedhihirika kabisa wizi wote mkubwa unaofanywa Tanzania una mikono ya CCM na ni kwa maslahi ya CCM sasa sijui ni nani atazingatia maslahi ya Tanzania na watanzania kama si sisi watanzania wenyewe.
 
Waziri Mkubwa na Mzito aliemnyeshwa Sumu Kipenzi cha Wanyonge Jana hakupewa Mwaliko wakati alikuwa Mtu muhimu kwenye utawala wa Mzee Mkapa wa miaka yote 10 na aligombea Urais 2005 but hakufurukuta

Huyo huyo Waziri alimkosa kosa Mkwere 2003 kule Znz kwenye Nec
 
Kuna siku hata wezi wa Richmond watatajana tu. Mambo mengi mda mchache
Kila rais atataja wizi dhambi alizozifanya, hata yule babu alisema Ujamaa ulikuwa na makosa mengi ukatupeleka kwenye umaskini wa kutupwa, watu walishindwa kujiendeleza kwa kuwa walikuwa na hofu ya kunyanganywa kila kitu na kuitwa wahujumu uchumi, sasa kuna ushindani wa fikra za kimaendeleo.
 
Mungu amsamehe tuanze mapya, ni binadamu afterall. Na aliyemnywesha sumu mwenzake naye atubu, na waliopanga na kumpiga lisu rossi nao watubu.ni mwendo wa toba tu muda wa kuishi umebaki kidogo mno
 
hata yule babu alisema Ujamaa ulikuwa na makosa mengi ukatupeleka kwenye umaskini wa kutupwa
Mkuu haya maelezo umeyatoa ktk kitabu au hotuba ipi ya babu?
Sio upotoshaji huu?

Kumbuka dunia ya leo unapata kila kitu nje ya maktaba ya asili iliyozoeleka.
 
Acha wewe wizi wa EPA una uhusiano gani ni Kitabu? Watanzania sio Wajinga
Uhusiano ni Mkapa ndio aliruhusu wizi wa EPA kwa ahadi kwamba chama kitanufaika pesa za kampeni za uchaguzi mkuu uliyomuingiza Kikwete madarakani.

Mkapa kwenye kitabu chake ameandika kwamba anahisi alitumika na kusalitiwa. ( Na Daud Balali?)
 
Back
Top Bottom