Kama mfanyakazi akikosa kazi hasaidiwi, kwanini mkulima asaidiwe?

MsemajiUkweli

JF-Expert Member
Jul 5, 2012
13,172
23,975
Hii nchi niya ajabu kweli!

Ibara ya 13(4) ya Katiba ya Tanzania inasema;
‘’Ni marufuku kwa mtu yeyote kubaguliwa na mtu au mamlaka yoyote inayotekeleza madaraka yake chini ya sheria yoyote au katika utekelezaji wa kazi au shughuli yoyote ya Mamlaka ya Nchi’’.

Tunaambiwa nchi hii niya wakulima na wafanyakazi!

Mkulima akikosa mvua anataka asaidiwe na serikali kupewa chakula.

Mfanyakazi akikosa kazi hasaidiwi hata pesa ya nauli kwenda kutafuta kazi.

Huu usawa na kutokubaguliwa tunaoambiwa ndani ya katiba uko wapi?

Kwenye nchi za wenzetu, mfanyakazi akikosa kazi anasaidiwa kwa kupewa pesa za kujikimu huku akitafuta kazi vivyo hivyo kwa wakulima ambao husaidiwa pesa za kujikimu na gharama za mazao yaliyopotea.

Kama mkulima anasaidiwa, basi hata mfanyakazi lazima asaidiwe.

Kama mfanyakazi hawezi kusaidiwa, basi hata mkulima asisaidiwe.

Hili suala lazima liangaliwe kwa upana zaidi ili kuondoa ubaguzi katika jamii.
 
Hii ndio justification ya kutokutoa chakula cha msaada?
Mkulima mmoja mmoja wakikosa kuvuna kutokana na sababu zao mbalimbali hapo serikali kumsaidia haina ulazima, ila wakulima wengi wanapokosa chakula kutokana na ukame uliaothiri wengi basi serikali ina jukumu la ku step in, la sivyo hakuna haja wala logic ya serikali kuzuia wakulima hawa kuuza chakula nje ili kuweka security ya chakula
 
Hii ndio justification ya kutokutoa chakula cha msaada?
Mkulima mmoja mmoja wakikosa kuvuna kutokana na sababu zao mbalimbali hapo serikali kumsaidia haina ulazima, ila wakulima wengi wanapokosa chakula kutokana na ukame uliaothiri wengi basi serikali ina jukumu la ku step in, la sivyo hakuna haja wala logic ya serikali kuzuia wakulima hawa kuuza chakula nje ili kuweka security ya chakula
Kuna maelfu ya wafanyakazi hawana ajira kama ilivyo kwa wakulima. Kwa nini serikali hai step in kuwasaidia?

Kuhusu kuzuiwa kuuza mazao holela. Hata wafanyakazi hawaruhusiwi kutumia fani zao holela. Kwa mfano, daktari au mwalimu hawezi kufungua hospitali au shule bila kupata kibali serikalini ambapo kuna uwezekano akakataliwa au kuruhusiwa.
 
Hii ndio justification ya kutokutoa chakula cha msaada?
Mkulima mmoja mmoja wakikosa kuvuna kutokana na sababu zao mbalimbali hapo serikali kumsaidia haina ulazima, ila wakulima wengi wanapokosa chakula kutokana na ukame uliaothiri wengi basi serikali ina jukumu la ku step in, la sivyo hakuna haja wala logic ya serikali kuzuia wakulima hawa kuuza chakula nje ili kuweka security ya chakula
nina uhakika atakupa majibu ya hovyo mpaka utaishiwa nguvu kujibizana naye.
 
Kuna maelfu ya wafanyakazi hawana ajira kama ilivyo kwa wakulima. Kwa nini serikali hai step in kuwasaidia?

Kuhusu kuzuiwa kuuza mazao holela. Hata wafanyakazi hawaruhusiwi kutumia fani zao holela. Kwa mfano, daktari au mwalimu hawezi kufungua hospitali au shule bila kupata kibali serikalini.
Hao wakulima wanalima na wanategemea hayo mazao kama chakula na kama chanzo cha kipato, hawana kingine kabisa, wakikosa mvua wamekosa kila kitu, huwezi fananisha na mtu aliyekosa kazi ambaye ana option nyingine za kujiajiri au kuishi kwa ndugu yake mwenye uwezo
Kukosa chakula nitofauti na kukosa kazi, chakula ni kati ya kifo na uhai,
 
Najaribu kukuelewa lakn nashindwa kabisaa maana thread yako imekaa kitoto mno, hv serikali inawasaidia wakulima au inawasaidia wananchi waliokubwa na baa la njaa? umesikia kuwa vyakula vya msaada vitagawiwa kwa wakulima?
Pia nikujulishe tu wapo wafanyakazi wengi ambao wanajishughulisha na kilimo pia
 
Hii nchi niya ajabu kweli!

Ibara ya 13(4) ya Katiba ya Tanzania inasema;
‘’Ni marufuku kwa mtu yeyote kubaguliwa na mtu au mamlaka yoyote inayotekeleza madaraka yake chini ya sheria yoyote au katika utekelezaji wa kazi au shughuli yoyote ya Mamlaka ya Nchi’’.

Tunaambiwa nchi hii niya wakulima na wafanyakazi!

Mkulima akikosa mvua anataka asaidiwe na serikali kupewa chakula.

Mfanyakazi akikosa kazi hasaidiwi hata pesa ya nauli kwenda kutafuta kazi.

Huu usawa na kutokubaguliwa tunaoambiwa ndani ya katiba uko wapi?

Kwenye nchi za wenzetu, mfanyakazi akikosa kazi anasaidiwa kwa kupewa pesa za kujikimu huku akitafuta kazi vivyo hivyo kwa wakulima ambao husaidiwa pesa za kujikimu na gharama za mazao yaliyopotea.

Kama mkulima anasaidiwa, basi hata mfanyakazi lazima asaidiwe.

Kama mfanyakazi hawezi kusaidiwa, basi hata mkulima asisaidiwe.

Hili suala lazima liangaliwe kwa upana zaidi ili kuondoa ubaguzi katika jamii.
Kwa taarifa yako, Mkulima ni mfanyakazi pia.. Alafu unakuwaje mfanyakazi wakati huna kazi?
 
Sababu ya kusaidia mkulima ziko mbili
1.Bila chakula nchi itazimia.Mkulima ndie analisha nchi .Ni mtu wa muhimu mno kwenye nchi


2.Ni kwa ajili ya usalama wa nchi.Vita nyingi huanzia vijijini maporini.Hao watu wakikosa chakula ni rahisi kurubuniwa na gaidi lolote likawapa chakula kwa makubaliano ya kuanzisha vita.Somalia,kongo,waasi wa Uganda wa LORD resistance army.Afghanstan ETC kote huko vita zilianzia maeneo ya wenye njaa vijijini waliokuwa hawana vyakula.Soma historia zote za vita nyingi zilianzia maeneo yenye njaa ya vijijini.
 
Ndugu, hapo sijakuelewa, mkulima ni nani na mfanyakazi ni nani?
Mfanyakazi ni yeyote yule anayejishughulisha kutafuta kipato chake ama anajitolea kufanya jambo fulani ambalo halikiuki sheria na miongozo tuliyo jiwekea kama taifa.

Hivyo hata mkulima ni mfanyakazi pia
 
Kuna maelfu ya wafanyakazi hawana ajira kama ilivyo kwa wakulima. Kwa nini serikali hai step in kuwasaidia?

Kuhusu kuzuiwa kuuza mazao holela. Hata wafanyakazi hawaruhusiwi kutumia fani zao holela. Kwa mfano, daktari au mwalimu hawezi kufungua hospitali au shule bila kupata kibali serikalini ambapo kuna uwezekano akakataliwa au kuruhusiwa.
Haaaa hakuna mfanyakazi asiye na kazi ila anaweza kukosa ajira, basi wakati unaendelea kutafuta ajira usiache kufanya kazi kusadifu jina lako la mfanyakazi
 
unataka huo usawa?Hoji na haya:
*kwann wakulima wanapata ruzuku kwny pembejeo?kwann serikali iwasaidie wao peke yao?Basi na watu wasio wakulima waangaliwe namna ya kupata ruzuku kwny shughuli zao.
*kwann mwanafunzi A apate mkopo na mwanafunzi B asipate mkopo wakati wote wamepata sifa ya kujiunga na vyuo vikuu.
*kwann serikali itoe ajira kwa watu wachache na si wahitimu wote
*kwann uwanja wa ndege ujengwe chato?
*kwann akina mama wajawazito na wazee watibiwe bure?kodi si tunakatwa wote,kwann wao?
note;nimeuliza hayo kwa nature ya uzi wako
 
Kazi kubwa ya serikali yoyote duniani ni kudhibiti njaa kwenye sekta zote iwe kwa wafanyakazi ,wakulima au wafanyabiashara.Njaa huwa kitu hatari kwa usalama wa nchi.Mapinduzi kwenye nchi nyingi yalianzishwa na makundi hayo matatu yakiwa na njaa.Mfano Wafanyakazi wenye njaa ndio waliongoza mapinduzi nchi za kikomunisti,Tanzania mkoloni aling`olewa na wafanyakazi waliokuwa na njaa wakiongozwa na vyama vya wafanyakazi vya akina kawawa nk.Marekani wakulima ndio waliongoza mapinduzi baada ya kuwa na hali ngumu.

Midororo ya kibiashara husababisha nchi nyingi kupinduliwa hasa za amerika ya kusini na AFrika magharibi

Kwa hiyo kudhibiti njaa maeneo yote ni kazi ya kwanza ya serikali.

Mtu ukiulizwa kazi ya serikali ni nini? Ni kudhibiti njaa sekta zote.
 
Mfanyakazi ni yeyote yule anayejishughulisha kutafuta kipato chake ama anajitolea kufanya jambo fulani ambalo halikiuki sheria na miongozo tuliyo jiwekea kama taifa.

Hivyo hata mkulima ni mfanyakazi pia
Sasa kwann katiba inasema nchi ya wakulima na wafanyakazi? Je katiba imekosewa? Acha mbwembwe swali si umelielewa?
 
unataka huo usawa?Hoji na haya:
*kwann wakulima wanapata ruzuku kwny pembejeo?kwann serikali iwasaidie wao peke yao?Basi na watu wasio wakulima waangaliwe namna ya kupata ruzuku kwny shughuli zao.
*kwann mwanafunzi A apate mkopo na mwanafunzi B asipate mkopo wakati wote wamepata sifa ya kujiunga na vyuo vikuu.
*kwann serikali itoe ajira kwa watu wachache na si wahitimu wote
*kwann uwanja wa ndege ujengwe chato?
*kwann akina mama wajawazito na wazee watibiwe bure?kodi si tunakatwa wote,kwann wao?
note;nimeuliza hayo kwa nature ya uzi wako
Kuhusu wanafunzi sababu zilishatolewa
 
Back
Top Bottom