Kama Mbowe alijuwa wameshindwa Mbona hakusema?

Kigarama

JF-Expert Member
Apr 23, 2007
2,492
1,230
Kwenye gazeti la Rai Mwema kuna taarifa kwamba Mbowe na Slaa walipata matokeo ya kushindwa kwenye uchaguzi wa Igunga saa tano usiku wa Tarehe 2/10/2011. Ninachojiuliza ni kwa nini si yeye wala Slaa aliyekuwa tayari kuwaambia wafuasi wa CHADEMA kwamba wameshindwa? Vurugu zilizotokea kwa sababu wafuasi hao waliamini kwamba kura zao zimechakachuliwa si zingezuiliwa?

Najua kuna hali imeanza kujijenga kwenye siasa za Bongo kwamba uzalendo ni kuonyesha CCM inakosea kwenye kila jambo!

TUTANGULIZE KWANZA TANZANIA KULIKO USHABIKI WA VYAMA VYETU!!
 
Kwenye gazeti la Rai Mwema kuna taarifa kwamba Mbowe na Slaa walipata matokeo ya kushindwa kwenye uchaguzi wa Igunga saa tano usiku wa Tarehe 2/10/2011. Ninachojiuliza ni kwa nini si yeye wala Slaa aliyekuwa tayari kuwaambia wafuasi wa CHADEMA kwamba wameshindwa? Vurugu zilizotokea kwa sababu wafuasi hao waliamini kwamba kura zao zimechakachuliwa si zingezuiliwa?

Najua kuna hali imeanza kujijenga kwenye siasa za Bongo kwamba uzalendo ni kuonyesha CCM inakosea kwenye kila jambo!

TUTANGULIZE KWANZA TANZANIA KULIKO USHABIKI WA VYAMA VYETU!!

Sio yeye Zitto Kabwe mwenyewe alikiri cdm imeshindwa igunga nakusema hawafikirii kwenda mahakamani. Hapo ndipo utajua wakati mwingine cdm huwa wanakosea sana kuhamasisha vitu ambavyo vingeweza kuzuilika. Kwa hili la igunga maji yalizidi unga wakubali tu
 
kwani nani ana majukumu ya kutangaza matokeo ya uchaguzi?kila mtu ana wajibu wake.ungekua ni uchaguzi ndani ya chadema wangetangaza lakini kumbuka ule uchaguzi ulisimamiwa na NEC.mia
 
"Violence is the last refuge of the incompetent." --Salvor Hardin
 
Nape alipata matokeo mapema na kuyamwaga hapa JF, mbona aliojiwa asubuhi tbc akayakataa? Mbowe, slaa watangaze matokeo kwani wao ndo nec?

Mimi sizungumzii kutangaza matokeo kwa niaba ya tume, ninachokisema ni kwamba hali ya wafuasi wale ilionyesha kwamba wanaamini kwamba matokeo yao yamechakachuliwa. ilikuwa ni wajibu wa viongozi wao ama kuwatuliza kwamba wangojee matokeo na kuwajenga kisaikolojia kwamba ingawa kuna uwezekano wa kushinda lakini upo pia uwezekano wa kushindwa.
 
"Violence is the last refuge of the incompetent." --Salvor Hardin

SO IN YOUR GREASED, WARPED MIND WHO IS VIOLENT IN THIS REGARD? Kinachoongelewa ni akina Mbowe kujua mapema kuwa CDM haijashinda, suala la violence linatoka wapi? Jamani si lazima kutoa comment kwenye kila thread, hiki ni kipimo cha akili tu.
 
SO IN YOUR GREASED, WARPED MIND WHO IS VIOLENT IN THIS REGARD? Kinachoongelewa ni akina Mbowe kujua mapema kuwa CDM haijashinda, suala la violence linatoka wapi? Jamani si lazima kutoa comment kwenye kila thread, hiki ni kipimo cha akili tu.
Tatizo letu ushabiki wa vyama vyetu umetujaa hadi kwenye kope za akili zetu!! Sasa hapa hatuchelewi kuitwa magamba.
 
Back
Top Bottom