Mathanzua
JF-Expert Member
- Jan 4, 2017
- 15,841
- 20,687
Nakumbuka wengi tulipokuwa shuleni, Jeshi la Polisi ilikuwa sehemu ya mwisho kabisa ambayo mtu angependa kujiunga nayo kwa ajira.Wengi tuliona kwamba watu wanaoajiriwa Jeshi la Polisi hawakuwa na uwezo darasani. Kama hii inaukweli sijui, ila nadhani hii inatokana na muonekano wa ujumla wa Jeshi letu.
Sidhani kama ni siri kwamba makazi ya Jeshi letu ni duni sana, ingawa namshuru sana Rais wetu kwa juhudi zake za dhati za kuboresha makazi ya askari wetu.Kimsingi naomba juhudi hizo ziendelee. Jambo hili linadhalilisha sana askari wetu na hatimaye kuwafanya wasijiamini na kukosa ujasiri katika utendaji wao.
Ni kweli pia kwamba Jeshi letu halipati vitendea kazi vya kutosha, ikiwa ni pamoja na uniform.Pia mpaka sasa Jeshi la Polisi linatumia makaratasi kuhifadhi kumbukumbu zake mbali mbali katika vituo vyake. Hali hii ni hatari, kwa kuwa kumbukumbu mbali mbali za watuhumiwa zinaweza kupotezwa makusudi kwa nia mbaya. Hili halina budi kubalika na kutumia mfumo wa ki-electronic.Wizara ya Sheria tayari inatumia mfumo huu.
Zipo taarifa pia kwamba Jeshi halitengewi fedha za kutosha kwa ajili ya mafuta ya magari yake. Hali hii huwafanya viongozi wa maeneo husika kuomba mafuta ya magari kutoka kwa wanaoitwa "Wadau Waelewa," au kutoa hela mifukoni mwao kwa ajili ya kununulia mafuta.Ifahamike kwamba kuomba mafuta kwa mdau yeyote wa Jeshi ni sawa na kuomba rushwa na ni kitendo kinacholidhalilisha Jeshi na anayeomba. Si ajabu kwa hiyo kwamba Jeshi letu linatuhumiwa kwa rushwa, mazingira ya rushwa tunayatengeneza wenyewe. Naomba ikumbukwe kwamba mishahara ya askari wetu sio mikubwa kihivyo, kwa hiyo kumfanya askari atoe sehemu ya mshahara wake kwa shuhuli za kikazi ni kumuelemea isivyo halali, jambo ambalo linaweza kumfanya ashindwe kuhudumia familia yake ipasavyo, na hivyo kukosa ari ya kufanya kazi. Naambiwa viongozi wa Jeshi la Polisi wameridhia hali hiyo,inashangaza sana.
Kiukweli hali hii hufanya kazi ya Jeshi letu kua ngumu,hasa inapobidi kufuatilia matukio na kupeleka watuhumiwa mahakamani. Hii pia hufanya jeshi letu lidharaulike mbele ya macho ya jamii na kufanya kazi ya Jeshi letu kuwa ngumu sana, jambo ambalo viongozi wa Jeshi walipaswa kulitambua.
Hivi kweli tunategemea mamlaka ya Jeshi imkamate anayeitwa "Mdau Muelewa " au ndugu yake aliyechangia mafuta Kituo cha Polisi X, kama amehusika kwenye tukio lolote?
Jambo la kushangaza ni kwamba zipo taariifa za kuaminika kwamba askari wa kawaida wakilalamikia hali ilivyo kwenye Jeshi, viongozi wa juu wanawashuhulikia.
Swali la kujiuliza ni kwamba je, viongozi hawa wanafurahia utoaji duni wa huduma wa Jeshi letu unaotokana na matatizo yaliyopo?
Zipo taarifa pia kwamba askari wanapokwenda kwenye shuhuli za kikazi nje ya vituo vyao vya kazi kwa siku kadhaa, hawalipwi "night duty allowance(NDA)," badala yake wanaambiwa waende halafu wakirudi watadai.Hivi kweli ni mfanyakazi gani anayeweza kujilipa "night duty allowance," hata kama akirudi atadai? Kwa mshahara upi kwanza. Hivi huku si kuwawafanya askari wetu wawe omba omba na kuhalalisha rushwa? Na kwa jinsi hii tuna sababu yeyote ya kuwalaumu askari wetu kwa kula rushwa?
Nadhani ni wakati muafaka sasa wa viongozi wa Jeshi la Polisi kupokea matatizo ya askari wanaowaongoza na kuyapeleka panapohusika,ili yapatiwe ufumbuzi, badala ya kuona kwamba askari hao ni adui. Ni wakati muafaka pia wa Serikali yetu kutatua matatizo yanayolikabili Jeshi letu,ili liwe Jeshi imara,linalotimiza wajibu wake kwa wakati na kujiamini.
Sidhani kama ni siri kwamba makazi ya Jeshi letu ni duni sana, ingawa namshuru sana Rais wetu kwa juhudi zake za dhati za kuboresha makazi ya askari wetu.Kimsingi naomba juhudi hizo ziendelee. Jambo hili linadhalilisha sana askari wetu na hatimaye kuwafanya wasijiamini na kukosa ujasiri katika utendaji wao.
Ni kweli pia kwamba Jeshi letu halipati vitendea kazi vya kutosha, ikiwa ni pamoja na uniform.Pia mpaka sasa Jeshi la Polisi linatumia makaratasi kuhifadhi kumbukumbu zake mbali mbali katika vituo vyake. Hali hii ni hatari, kwa kuwa kumbukumbu mbali mbali za watuhumiwa zinaweza kupotezwa makusudi kwa nia mbaya. Hili halina budi kubalika na kutumia mfumo wa ki-electronic.Wizara ya Sheria tayari inatumia mfumo huu.
Zipo taarifa pia kwamba Jeshi halitengewi fedha za kutosha kwa ajili ya mafuta ya magari yake. Hali hii huwafanya viongozi wa maeneo husika kuomba mafuta ya magari kutoka kwa wanaoitwa "Wadau Waelewa," au kutoa hela mifukoni mwao kwa ajili ya kununulia mafuta.Ifahamike kwamba kuomba mafuta kwa mdau yeyote wa Jeshi ni sawa na kuomba rushwa na ni kitendo kinacholidhalilisha Jeshi na anayeomba. Si ajabu kwa hiyo kwamba Jeshi letu linatuhumiwa kwa rushwa, mazingira ya rushwa tunayatengeneza wenyewe. Naomba ikumbukwe kwamba mishahara ya askari wetu sio mikubwa kihivyo, kwa hiyo kumfanya askari atoe sehemu ya mshahara wake kwa shuhuli za kikazi ni kumuelemea isivyo halali, jambo ambalo linaweza kumfanya ashindwe kuhudumia familia yake ipasavyo, na hivyo kukosa ari ya kufanya kazi. Naambiwa viongozi wa Jeshi la Polisi wameridhia hali hiyo,inashangaza sana.
Kiukweli hali hii hufanya kazi ya Jeshi letu kua ngumu,hasa inapobidi kufuatilia matukio na kupeleka watuhumiwa mahakamani. Hii pia hufanya jeshi letu lidharaulike mbele ya macho ya jamii na kufanya kazi ya Jeshi letu kuwa ngumu sana, jambo ambalo viongozi wa Jeshi walipaswa kulitambua.
Hivi kweli tunategemea mamlaka ya Jeshi imkamate anayeitwa "Mdau Muelewa " au ndugu yake aliyechangia mafuta Kituo cha Polisi X, kama amehusika kwenye tukio lolote?
Jambo la kushangaza ni kwamba zipo taariifa za kuaminika kwamba askari wa kawaida wakilalamikia hali ilivyo kwenye Jeshi, viongozi wa juu wanawashuhulikia.
Swali la kujiuliza ni kwamba je, viongozi hawa wanafurahia utoaji duni wa huduma wa Jeshi letu unaotokana na matatizo yaliyopo?
Zipo taarifa pia kwamba askari wanapokwenda kwenye shuhuli za kikazi nje ya vituo vyao vya kazi kwa siku kadhaa, hawalipwi "night duty allowance(NDA)," badala yake wanaambiwa waende halafu wakirudi watadai.Hivi kweli ni mfanyakazi gani anayeweza kujilipa "night duty allowance," hata kama akirudi atadai? Kwa mshahara upi kwanza. Hivi huku si kuwawafanya askari wetu wawe omba omba na kuhalalisha rushwa? Na kwa jinsi hii tuna sababu yeyote ya kuwalaumu askari wetu kwa kula rushwa?
Nadhani ni wakati muafaka sasa wa viongozi wa Jeshi la Polisi kupokea matatizo ya askari wanaowaongoza na kuyapeleka panapohusika,ili yapatiwe ufumbuzi, badala ya kuona kwamba askari hao ni adui. Ni wakati muafaka pia wa Serikali yetu kutatua matatizo yanayolikabili Jeshi letu,ili liwe Jeshi imara,linalotimiza wajibu wake kwa wakati na kujiamini.