TL. Marandu
JF-Expert Member
- Jul 12, 2015
- 3,625
- 5,807
Kutokana na Ukweli ambao Kila Mmoja anajua, Kwamba Uchaguzi wa Zanzibar Matokeo yalifutwa (sio uchaguzi kufutwa) Kisha CCM kwa Kumtumia Jecha wakajitahidi sana Kuwalazimisha CUF washiriki "Uchaguzi" wa Marudio ili wapate uhalali. Wakalazimisha hata Kuweka Majina ya Wagomea wa CUF kwenye Balot papers. Anyway, Iliposhindikana wakaingia uchaguzi na Vyama vikaragosi, ati wakapata Ushindi wa 90% sawa na Kujitekenya mwenyewe na kucheka!
Cha kushangaza, Ni Mtu asemaye Ni msema kweli na Ni Mpenzi wa Mungu, Kwa kebehi ya Kutisha anaagiuza Jecha stooge aliyevuruga Demokrasia Zanzibar apewe tuzo? Je Nani mwenye akili Timamu anadhani Mh. Magufuli atajali hata Kidogo Kuagiza Uchaguzi wa 2020 Uvurugwe Kila Ngazi na Kuwapa Tuzo waliouvuruga?
Wapinzani Iwapo watajiingiza Kwenye Uchaguzi wa 2020 Kama hali ilivyo watakuwa wamemhalalishia Magufuli Matokeo atakayoyapata yeye na Chama chake. Pia Wakisusa Kushiriki Uchaguzi, CCM watatumia vyama Vikaragosi Kugombea nao na Kisha kuwapa Majimbo Matano Matano Waliovuruga wanapewa Tuzo Mchezo Unaisha.
Mimi Nafikiri Kuna Madictator Wanaofanya Watakavyo Barani Afrika Kwa sababu Tunakuwa na Upole wa Ujinga na Tunajipenda sana na Kujawa hofu, Na Pale Tunapokasirishwa na Kupambana tunapambana na watu wrong, raia wenzetu, Polisi, Wanajeshi etc. Lakini Kama Afrika Wakiwahakikishia Madictator wasipoacha Udictator hawapo salama, Madictator Watajirekebisha na Kufuata sheria na Katiba, au Wakikomaza shingo Waishe wote!
Ni kweli Kama alivyokuwa Qadaffi, Ni Vizuri Kuleta Madawati, Ni Vizuri Kupambana na Rushwa, Ni Vizuri Kujali huduma za Afya Ni Vizuri Kuboresha Elimu na Maisha ya Waalimu. Na Asante yetu Ni mishahara tuwapayo, na Tutawaenzi, Lakini Rais Yeyote anayedhani Kwa Kuzingatia kufanya hayo ati Tumlipe kwa Currency ya UHURU wetu, AMANI yetu, SAUTI zetu, KATIBA yetu? Huyo Anawazimu, Hatufai na Ni adui, Ni sawa na Mtu anayekununulia Chupa ya Bia na Jioni anataka Umrusu aje Kwa Mkeo! Tukimkubalia Basi Tuwaombe kwaza Radhi, Wajerumani, Waingereza, Wareno, Wabelgiji, Wafaransa na Wakoloni wengine Tuliopigana nao Afrika sio kwa Kutaka Asprin, Au Dawati au Barabara Bali UHURU!
Cha kushangaza, Ni Mtu asemaye Ni msema kweli na Ni Mpenzi wa Mungu, Kwa kebehi ya Kutisha anaagiuza Jecha stooge aliyevuruga Demokrasia Zanzibar apewe tuzo? Je Nani mwenye akili Timamu anadhani Mh. Magufuli atajali hata Kidogo Kuagiza Uchaguzi wa 2020 Uvurugwe Kila Ngazi na Kuwapa Tuzo waliouvuruga?
Wapinzani Iwapo watajiingiza Kwenye Uchaguzi wa 2020 Kama hali ilivyo watakuwa wamemhalalishia Magufuli Matokeo atakayoyapata yeye na Chama chake. Pia Wakisusa Kushiriki Uchaguzi, CCM watatumia vyama Vikaragosi Kugombea nao na Kisha kuwapa Majimbo Matano Matano Waliovuruga wanapewa Tuzo Mchezo Unaisha.
Mimi Nafikiri Kuna Madictator Wanaofanya Watakavyo Barani Afrika Kwa sababu Tunakuwa na Upole wa Ujinga na Tunajipenda sana na Kujawa hofu, Na Pale Tunapokasirishwa na Kupambana tunapambana na watu wrong, raia wenzetu, Polisi, Wanajeshi etc. Lakini Kama Afrika Wakiwahakikishia Madictator wasipoacha Udictator hawapo salama, Madictator Watajirekebisha na Kufuata sheria na Katiba, au Wakikomaza shingo Waishe wote!
Ni kweli Kama alivyokuwa Qadaffi, Ni Vizuri Kuleta Madawati, Ni Vizuri Kupambana na Rushwa, Ni Vizuri Kujali huduma za Afya Ni Vizuri Kuboresha Elimu na Maisha ya Waalimu. Na Asante yetu Ni mishahara tuwapayo, na Tutawaenzi, Lakini Rais Yeyote anayedhani Kwa Kuzingatia kufanya hayo ati Tumlipe kwa Currency ya UHURU wetu, AMANI yetu, SAUTI zetu, KATIBA yetu? Huyo Anawazimu, Hatufai na Ni adui, Ni sawa na Mtu anayekununulia Chupa ya Bia na Jioni anataka Umrusu aje Kwa Mkeo! Tukimkubalia Basi Tuwaombe kwaza Radhi, Wajerumani, Waingereza, Wareno, Wabelgiji, Wafaransa na Wakoloni wengine Tuliopigana nao Afrika sio kwa Kutaka Asprin, Au Dawati au Barabara Bali UHURU!