Ubumuntu
JF-Expert Member
- Oct 21, 2010
- 14,316
- 10,782
Salaam wana JF! Naelewa mijadala juu ya huyo mmeru imeshakua mingi sana humu na nchini,hadi inachosha. Lakini naomba mimi nijikite katika upande mwingine wa shilingi. Huyu mzee anasemekana ana nguvu kubwa sana ndani ya C.C.M. kiasi cha kuwa tishio kwa wapinzani wake (chanzo:walamba miguu yake). Hiyo nguvu ndiyo inapelekea hao wapambe wake waamini hakuna mwana C.C.M. mwenye kuweza kumzuia mzee huyu katika mbio za kuwania urais mwaka 2015. Vyema. Kama kweli anayo hiyo nguvu,basi afanye yafuatayo: 1. Ashawishi wabunge kupitia C.CM. wakubali mapendekezo ya marekebisho ya sheria ya marekebisho ya katiba ya mwaka 2011;marekebisho yaliyopendekezwa na watanzania wenye nia njema na nchi yao. Nasema hivyo kwa sababu maneno mtaani ni kwamba wabunge wa C.CM. wanataka kupinga mapendekezo hayo,kwavile itakua sawa na wao kula matapishi yao! 2. Awashawishi wabunge wa C.C.M. kuwawajibisha (kupitia bunge) viongozi wa wizara ya afya (waziri,naibu na katibu mkuu)na waziri mkuu,kwani viongozi hao wameshindwa kushughulikia ipaswavyo mgomo wa madaktari. Ambamo kuna vijana wenye ajira humo (mzee huyo amekua akijinadi kama mwenye kujali ajira kwa vijana). 3. Na mwisho awashawishi wabunge wa C.C.M. kupiga kura ya kutokua na imani na rais wa JMT. Kwani kiongozi huyo amedhihirika kudanganya umma (kwa mujibu wa wabunge wa C.C.M.) kwa kusema hajaidhinisha ongezeko la posho mpya na malipo yake kwa wabunge. Kwani haiwezekani waziri mkuu na spika waseme hadharani kwamba rais ameshaidhinisha,halafu rais akiwa nje ya nchi atoe tamko la kupinga kauli hizo. Hiyo ni dalili ya kuwadhalilisha wabunge wa C.C.M. ambao ndani yake kuna mawaziri wa serikali yake (ina maana amedhalilisha na serikali yake pia). Mzee Lowassa dhihirisha nguvu zako sasa ndani ya C.C.M. Kwani anguko la rais wa JMT litakufanya upate fursa ya kuwania urais mapema kabla ya 2015. Na kwa nguvu ambazo inasemwa unazo,utaingia magogoni kama unasukuma mlevi. Mzee I DARE YOU. Otherwise, you are nothing,but an opportunistic and hypocrite kind of a greedy politician.