EJM_
JF-Expert Member
- Jul 8, 2011
- 3,836
- 2,090
Wakati akihitimisha mjadala wa taarifa ya kamati mbalimbali hasa za Serikali za mitaa, mashirika ya umma na ile ya wakubwa, Mwenyekiti wa kamati ya serikali za mitaa Mh. Zitto Zuberi Kabwe ametoa pendekezo la kupiga kura ya kutokuwa na imani na waziri mkuu kama njia ya kuwawajibisha mawaziri ambao wamekuwa wakipatikana na makosa mbalimbali lakini hawachukuliwi hatua.
Mh. Zitto amesema kwakuwa mamlaka ya kuteua na kuwaondoa mawaziri ni ya rais pekee, na kwakuwa wao kama bunge hawana mamlaka yoyote juu yaom basi wao watumie rungu waalilonalo ambalo ni kumwajibisha waziri mkuu ambapo kwa kufanya hivyo wataanza kwa kukusanya sahihi za wabunge 70 ili kufikisha idadi ya wabunge wanaotosha kuunda hoja ya kupigwa kwa kura hiyo kwa mujibu wa kanuni na zaidi ya asilimia 50 ya kura kumwondoa waziri mkuu.
Kwa mtazamo wangu nadhani kumekuwa na kubebana kwa kiasi kikubwa kwa mawaziri na nashauri kama kweli wabunge wa CCM wana machungu na wanachi wanaowawakilisha, kama kweli wana mapenzi ya kweli kwa nchi hii na chama chao, basi waungane mkono na hili kwa moyo mmoja ili tuweze kuendelea kama nchi.
Mh. Zitto amesema kwakuwa mamlaka ya kuteua na kuwaondoa mawaziri ni ya rais pekee, na kwakuwa wao kama bunge hawana mamlaka yoyote juu yaom basi wao watumie rungu waalilonalo ambalo ni kumwajibisha waziri mkuu ambapo kwa kufanya hivyo wataanza kwa kukusanya sahihi za wabunge 70 ili kufikisha idadi ya wabunge wanaotosha kuunda hoja ya kupigwa kwa kura hiyo kwa mujibu wa kanuni na zaidi ya asilimia 50 ya kura kumwondoa waziri mkuu.
Kwa mtazamo wangu nadhani kumekuwa na kubebana kwa kiasi kikubwa kwa mawaziri na nashauri kama kweli wabunge wa CCM wana machungu na wanachi wanaowawakilisha, kama kweli wana mapenzi ya kweli kwa nchi hii na chama chao, basi waungane mkono na hili kwa moyo mmoja ili tuweze kuendelea kama nchi.