GENTAMYCINE
JF-Expert Member
- Jul 13, 2013
- 56,073
- 107,570
Za Jumapili waheshimiwa Wapendwa na natumai nyote mmekuwa na siku murua kabisa huku mkitafakari ni jinsi gani mtainza wiki mpya ya Kesho huku wengine mkiwa mmeishiwa kabisa Hela na wengine kuchunwa kisawasawa na wengine mkiwaza ni jinsi gani sasa mtakuwa mnawakwepa wale mliowakopa ili tu msheherekee vizuri Siku Kuu iliyokwishamalizika ya Eid. ( Msijali nimechomekea tu muanze kutabasamu kwanza kabla ya baadae kuja kulia kwa ninachowaletea hapa chini )
Wapendwa tokea siku ya Ijumaa tarehe 8 hadi jana Jumamosi tarehe 9 niliamua kuungana na Wenzangu kadhaa ambao kiukweli tumekuwa tukikerwa sana na hizi ajali zinazozidi kutokea hapa nchini kwetu Tanzania kufanya UTAFITI mdogo ambao tulihusisha Vituo vikuu vinne vya Mabasi ya Mikoani cha Dar es Salaam, Arusha, Mbeya na Mwanza na nawashukuru sana wale wote waliotudhamini kwa suala zima la usafiri wa Ndege maalum ya kukodi kuruka katika hiyo mikoa tajwa na pia kwa malazi kwani ninaamini haya majibu tuliyoyapata yanaweza yakaasisi tatizo zima ambalo litatusaidia kujua nini cha kufanya ili kujiokoa au kumaliza tatizo.
Katika UTAFITI wetu huu mdogo tuliweza kuwahoji sana Madereva wa haya Mabasi na swali tulilowauliza lilikuwa ni KWANINI SIKU HIZI KUNA AJALI NYINGI NA AMBAZO NI ZA KIZEMBE SANA HAPA NCHINI TANZANIA TOFAUTI NA MIAKA YA NYUMA?
Wapendwa yafuatayo ni majibu ya 90% ya hao Madereva tuliobahatika kuwahoji baada ya kukutana nao katika hiyo Mikoa ambayo naomba niyawakilishe kwenu bila kuongeza au kupunguza chochote:
Ni hayo tu Wapendwa na sijui nyie kama Wataalam, Wasomi na Wajuvi wa mambo mbalimbali hizo sababu zao hapo juu mmezipokeaje na labda nini kifanyike.
Karibuni na muwe na Jumapili njema na tulivu ila binafsi nadhani itabidi tu sasa niwe tu nasafiri kwa miguu hadi Vijijini kwetu Kyaka Nkunde na Ikupilipa Nkoba kwani " NIMEOGOPA " sana na najuta hata kwanini nilienda kufanya huu UTAFITI kwani umenifanya sasa nikisikia tu Rafiki yangu au Ndugu yangu yoyote anasafiri basi " nalia " kidogo kisha ndiyo namtakia safari njema!
Wapendwa tokea siku ya Ijumaa tarehe 8 hadi jana Jumamosi tarehe 9 niliamua kuungana na Wenzangu kadhaa ambao kiukweli tumekuwa tukikerwa sana na hizi ajali zinazozidi kutokea hapa nchini kwetu Tanzania kufanya UTAFITI mdogo ambao tulihusisha Vituo vikuu vinne vya Mabasi ya Mikoani cha Dar es Salaam, Arusha, Mbeya na Mwanza na nawashukuru sana wale wote waliotudhamini kwa suala zima la usafiri wa Ndege maalum ya kukodi kuruka katika hiyo mikoa tajwa na pia kwa malazi kwani ninaamini haya majibu tuliyoyapata yanaweza yakaasisi tatizo zima ambalo litatusaidia kujua nini cha kufanya ili kujiokoa au kumaliza tatizo.
Katika UTAFITI wetu huu mdogo tuliweza kuwahoji sana Madereva wa haya Mabasi na swali tulilowauliza lilikuwa ni KWANINI SIKU HIZI KUNA AJALI NYINGI NA AMBAZO NI ZA KIZEMBE SANA HAPA NCHINI TANZANIA TOFAUTI NA MIAKA YA NYUMA?
Wapendwa yafuatayo ni majibu ya 90% ya hao Madereva tuliobahatika kuwahoji baada ya kukutana nao katika hiyo Mikoa ambayo naomba niyawakilishe kwenu bila kuongeza au kupunguza chochote:
- Wakubwa ( wakimaanisha sisi Watafiti ) sisi Madereva tunasikitika mno pale ambapo kila inapotokea tu ajali lawama zenu zote mnatuletea sisi wakati ukweli ni kwamba WAMILIKI wetu wanayafanyia mno mambo ya KISHIRIKINA haya Mabasi yao na ukikataa kile kinachofanyika basi unaambiwa ukabidhi funguo hivyo sisi hukubaliana na matakwa yao ilimradi familia zetu zisilale njaa.
- Wakubwa inapoelekea huko mbele kuna siku tutasema UKWELI wote kwani sisi Madereva hasa wa hapa Ubungo huwa tunabahatika kabisa usiku wa manane kukutana na WAFANYABIASHARA wakubwa tu na VIONGOZI wakubwa wa KISIASA hapa nchini wakija kufanya mambo ya ajabu ya KISHIRIKINA pale katika geti la kuingilia na hasa hasa pale mataa Ubungo kwani kuna muda hawa Watu huja wenyewe na wakijua kuwa tumewagundua basi hutupa PESA nyingi tu za kutufanya tusiseme lolote.
- Wakubwa Mimi binafsi ni Dereva wa Basi la Dar - Mwanza lakini kila nikianza tu safari yangu Bosi wangu hunipa kitu fulani kikiwa katika mfuko na kunielekeza kuwa nikifika tu maeneo ya Morogoro na Singida basi nikirushe na nitamke neno " kula chakula chako " na nimekuwa nikifanya hivi kwa muda kidogo ila Magari ya wenzangu tu ndiyo hupata ajali ila la kwangu hapana na Bosi wangu ananipenda kupita hata Wanafamilia wake.
- Wakubwa huyu hapa ni Dereva wa ruti za Dar - Mbeya hebu muulizeni ni kwanini kila akiwa anatoka Mbeya au Dar kuna akina Mama huwa anakabidhiwa asafiri nao kisha akifika Kituo fulani awashushe na kapewa SHARTI la kutowasemesha chochote wakiwa wamepanda humo.
- Wakubwa sisi Madereva wenyewe hatupendani kwani wengi wetu kutokana na ugumu wa maisha na kuwa na roho mbaya ya wivu huamua tu KUROGANA ili Magari yetu yapate ajali TUFE kabisa au tupate ULEMAVU wa kudumu kisha wakabidhiwe wao Magari kuendesha. Kama huamini fanyeni UKAGUZI wa ghafla hapa mtagundua kuwa kila Dereva hapa AMEVAA HIRIZI au AMEWEKA HIRIZI yake chini ya kiti chake yote hiyo ikiwa ni moja ya KINGA yake. Huyu Mzee hapa kila akisafiri akifika maeneo ya KITONGA lazima tu ataona Watu wanakatisha na JENEZA na nakumbuka kuna siku aliwahi kuwakwepa na Basi lake likapinduka na kuja kuangalia nje akakuta wale Watu hawapo ila tokea nae aende kwao Kigoma siku hizi akikutana tu na hiyo hali yeye hunyoosha tu na kuwagonga kwani wale huwa si Watu kweli bali ni MAJINI.
- Wakubwa kuna Abiria wengine nao hakika ni WASHIRIKINA sana kwani wapo wengine ambao safari zao ni za kutoka au kwenda kwa Waganga Mikoani ambapo wakiwa huko hupewa Dawa na kutakiwa kufanya KAFARA la DAMU hivyo wengi wao huamua kuingia na hizo Dawa " Ndumba " zao katika haya Mabasi ambapo ndani ya muda fulani Basi huanguka na kusababisha ajali mbaya. Kwa mfano kuna ajali moja tuliikuta maeneo ya Mwanga hivyo ikatubidi tusimame na kutoa msaada ambapo kuna baadhi ya Maiti kama tatu hivi wakati tunawabeba tuliwakuta wana yai mfukoni limepakwa rangi nyeusi, mwingine tukamkuta mfuko wake wa Suruali kuna nyoka mdogo na mwingine tukakuta ana hirizi kubwa kabisa.
- Wakubwa labda tu leo tuwapeni SIRI kubwa ambayo hamuijui ambapo mkisikia tu ajali yoyote ya Basi imetokea halafu mkasikia Dereva au Madereva wamepona basi hapo jueni 100% kuwa ni NGUVU YA KISHIRIKINA na Dereva huwa ameshajua kwani haya Mabasi yetu mengi usiku kabla ya Safari kuanza kule mbele ( kwenye Kichwa tu ) huoshwa na ama Maji yaliyooshea Maiti au Damu ya Kondoo na endapo mkisikia tu ajali imetokea halafu Dereva au Madereva wote wamekufa hapo hapo basi jueni kuwa MADEREVA wenzao wamewafanyia kitu mbaya kwani katika hii Kazi kuna fitina nyingi sana.
Ni hayo tu Wapendwa na sijui nyie kama Wataalam, Wasomi na Wajuvi wa mambo mbalimbali hizo sababu zao hapo juu mmezipokeaje na labda nini kifanyike.
Karibuni na muwe na Jumapili njema na tulivu ila binafsi nadhani itabidi tu sasa niwe tu nasafiri kwa miguu hadi Vijijini kwetu Kyaka Nkunde na Ikupilipa Nkoba kwani " NIMEOGOPA " sana na najuta hata kwanini nilienda kufanya huu UTAFITI kwani umenifanya sasa nikisikia tu Rafiki yangu au Ndugu yangu yoyote anasafiri basi " nalia " kidogo kisha ndiyo namtakia safari njema!