Zanzibar-ASP
JF-Expert Member
- Nov 28, 2013
- 10,115
- 35,129
Kama Rais Samia kile alichokisema kuhusu Lukuvi (kuwa amemtoa kwenye uwaziri na sasa anamleta ikulu kuja kumsaidia kuwasimamia mawaziri, na atampa kazi maalum ambayo watanzania tusubiri kuja kutangaziwa) basi huenda ikawa ni nafasi ya uwaziri mkuu!
Huenda kinachofanyika sasa ni kupima upepo wa kisiasa, kuvuta muda ili mchakato wa kumpata spika mpya ukamilike, bunge liitishwe na labda jina la waziri mkuu mpya likatangazwa.
Sote tunajua kung'olewa kwa Spika Ndugai ulikuwa ni mkakati wa kumdhoofisha Majaliwa kwenye mbio zake za urais kuelekea 2025, na lengo la kutaka kuundwa upya kwa baraza la mawaziri kulilenga kumtoa Majaliwa lakini ili kuboteza maboya tusijui chochote kilichokusudiwa baada ya kuhisi na taarifa kusambaa ikabidi yafanyike marekebisho tu kwenye baraza la mawaziri na kuvuta muda ambapo utekelezaji uliokusudiwa utanyika vizuri.
Ngoja tujipe muda.
Mambo ni mengi sana.
Huenda kinachofanyika sasa ni kupima upepo wa kisiasa, kuvuta muda ili mchakato wa kumpata spika mpya ukamilike, bunge liitishwe na labda jina la waziri mkuu mpya likatangazwa.
Sote tunajua kung'olewa kwa Spika Ndugai ulikuwa ni mkakati wa kumdhoofisha Majaliwa kwenye mbio zake za urais kuelekea 2025, na lengo la kutaka kuundwa upya kwa baraza la mawaziri kulilenga kumtoa Majaliwa lakini ili kuboteza maboya tusijui chochote kilichokusudiwa baada ya kuhisi na taarifa kusambaa ikabidi yafanyike marekebisho tu kwenye baraza la mawaziri na kuvuta muda ambapo utekelezaji uliokusudiwa utanyika vizuri.
Ngoja tujipe muda.
Mambo ni mengi sana.