Kama kweli Mhe. EL alikubali kuwa kafara..basi sasa hivi anasubiri vinguvu vidogo kama Samsom.

Niliyaona hayo maswali na pasco akayakwepa ila kelele hazikuisha.Hembu tujiulize kama Mh E.L nae yupo determined akachukua njia ya kufanya "things right", nini itakuwa matokeo yake ndani na nje ya CCM ?Pi si yeye mwenyewe aliyeambiwa hafai,hata JK alipewa lugha nyepesi kuwa bado hajakomaa.Ila mwalimu Nyerere hakuweka timeframe atakomaa lini, wala vigezo kuwa akikomaa tutamjuaje?Kijana akampisha Mkapa kwa manung`uniko km leo tumuonavyo Zitto ,huku udini ukiongeza mashinikizo.Baadaye akaja na huu kelele zikisema kuwa keshakomaa na mengine mengi sana.

Sasa tupo hapa tulipo hata yale madini tuliyoambiwa tusubiri hadi tupate uwezo yamechimbwa na kuthibiika kuwa hatuna uwezo na hii ni kwa vile hatukuwa na vipimo kutuonyesha kama tumekomaa.Mheshimiwa EL kama atakuja tutegemee kauli kama alitubu kwa Joshua, na ahadi za vijana,na pia hayo masalia pia yatakuwa na kelele zao nyingi.

Nini maoni yako kama atatangaza nia.Akubalia achia kitu ambacho andhani kuwa ni haki yake kuweka ktk malengo na kupenda kuyafikia na kubaki akijilaumu kwa maisha yake yote?Arudi katika drawing board na kujipanga upya?au aamue kuwapa watanzania zawadi kwa kuivunja CCM kabisa na kubaki kama mzee mwenye furaha kwa alichowapa watanzania?Je kama watu wanaamini ni fisadi je atakuwa salama CDM au hata CCm yenye mtu nje ya mtandao akichukua nchi?

Kwa kuwa watanzania wanataka mabadiliko yenye kumaanisha chama mbadala ikiwa atatangaza nia, maana amekuwa akijaribu kufanya PR kampeni nyingi tu akidhani watu hawaelewi anachokifanya, basi huo ndio mwisho wa EL na itakuwa CCM imeanguka mwanguko mkuu.

Kama mkuu Kwitega alivyotanabaisha kuhusu hili swali lako nami naongeza kwamba atajiunga na walewale aliowaharibia kwama 2005 na watafurahi sana.
 
Mkuu,fuatilia tu ile thread ya kuhusu professa Muhongo aliyoyasema kuhusu Tanesco na mikataba kwa ujumla!

Utapatwa na hasira vibaya mno!Hawa watu wanastahili kuwa kizimbani kujibu mashtaka!Halafu kuna watu wana balls za hata kumtamka humu ndani?

Eti kisa alijitoa kafara,kafara kwa nani na Taifa linalipa kwasababu yao na pesa walizopata ndo wanatumia kujijenga binafsi ili kupata madaraka zaidi?Kama ni kafara halafu anataka urais,basi kafara itakuwa ni watanzania!

Na Zitto naye?Yani kwakweli inasikitisha sana!

Ile thread ya Professor Muhongo nimeisoma vizuri tu na inajitosheleza.

Professor anataka kufanya usafi na wale wote wenye hisa kwenye hizo kampuni watakuwa wanahangaika kwa sasa, tatizo ni usalama wake tu maana mizengwe ni mingi sana penye ugonjwa wa UFISADI.

Pia ninayo copy ya report ya Mwakyembe na nimeipitia ambayo nayo inajisholeza hivyo kutoa mwanga wa kuhusu huyu mheshimiwa.

Halafu fuatilia yale mahojiano ya EL na ITV kama sikosei, ambayo alifanya baada ya kujiuzulu utagundua mambo mengi tu.

Kwahio hitimisho linakuwa kwamba hana "credibility" kuweza kushika ofisi ya magogoni kwani hataweza kutoa maamuzi sahihi kuhusu mwelekeo wa taifa kwa ujumla maana washauri atakuwa nao lakini pengine hatawasikiliza au atawasikiliza na baadae kupindisha ushauri.
 
kinyang`anyiro cha kinachoendelea cha kupata wajumbe wa nec wa CCM tayari kinarudisha tena CCM katika suicidal point.Huku samson akijitahidi recovery kupata nguvu za kutosha just kuimaliza CCM.

Vibaraka wa makambi tofauti wakijiweka aktk stance tofauti za kummaliza atakayechaguliwa kuiwakilisha CCM ktk uchaguzi mkuu kipindi kikifika.

Mazingira yote yanampa CDM muda wa kufanya mambo ya msingi,na yenye ku perfect technics zake.Time inavyokwenda kuna wana CCM wataanza iona deadlock live na hivyo kuona ni bora Kuambatana na CDM kuliko kumtunza ng`ombe mwenye kansa ya maziwa.
 
Its about the time samson kuamua kama wafilist wanampa heshima ama anavunja nguzo zote na kuwapa watanzania zawadi ya kufa na wafilist wote na pango wajifichalo.

Kama hakuna njia nyingine ya mhe kutoa kafara basi ni bora akatoa shemu ya nguvu zake kuwa mchangoa katk mapinduzi ya ukombozi Angalau aivunje CCM na watanzania wamkubuke kwa hilo.

Watampa heshima kwa hilo .
 
Ile thread ya Professor Muhongo nimeisoma vizuri tu na inajitosheleza.

Professor anataka kufanya usafi na wale wote wenye hisa kwenye hizo kampuni watakuwa wanahangaika kwa sasa, tatizo ni usalama wake tu maana mizengwe ni mingi sana penye ugonjwa wa UFISADI.

Pia ninayo copy ya report ya Mwakyembe na nimeipitia ambayo nayo inajisholeza hivyo kutoa mwanga wa kuhusu huyu mheshimiwa.

Halafu fuatilia yale mahojiano ya EL na ITV kama sikosei, ambayo alifanya baada ya kujiuzulu utagundua mambo mengi tu.

Kwahio hitimisho linakuwa kwamba hana "credibility" kuweza kushika ofisi ya magogoni kwani hataweza kutoa maamuzi sahihi kuhusu mwelekeo wa taifa kwa ujumla maana washauri atakuwa nao lakini pengine hatawasikiliza au atawasikiliza na baadae kupindisha ushauri.

Na hili ndo tatizo mkuu,cjui km mhongo atabaki salama!coz kazi aliyoianzisha ni kubwa,na hili genge la mafisadi...
 
Na hili ndo tatizo mkuu,cjui km mhongo atabaki salama!coz kazi aliyoianzisha ni kubwa,na hili genge la mafisadi...

kama hana njaa kali, na ana uzalendo anaweza pima na kuona bora legacy ya kuitendea vyema nchi yako kuliko kubaki katik hiki kipindi kilichobaki kwa laana.
 
kauli ya Dr.Slaa kuhsu CCM kushindwa waengua wanaotuhumiwa kwa ufisadi kuna maanisha CCM inakufa,inaonyesha wazi suala la ufisadi bado lina nguvu na mtuhumiwa ufisadi yoyote nahitaji sacrifice kubwa ya kusafisha jina.

CCM nayo haina nia ya dhati ya kusafisha nyumba yake au lah kuamua moja.KUWAKUBALI WATUHUMIWA NA KUIHAKIKISHIA jamii kuwa wapo nao au hata kuwaengu katk chama.CCM wapo wazi kabisa kuwa hawawezi waengue aila hawapo tena tayari msafisha miwngine.Mwishowe waliochafuka wataingia katk cycle ya kutokubalika .Kuweza lobby na kukishinda chama ni kama kupambana ili afe kwa njia nyingine na kwa pamoja na chama.Kwa ujumla chama kimejiweka pabaya sana, na ikizingatiwa walishafanya amkosa amkubwa sana kiasi cha kufanya wakose shukrani ya kuwapa wana mtandao, na baadaye kuwa na kundi kubw alinaloona kuw ahakuna muda tena wa kusubiri nafasi.
 
Kwa hotuba ya leo ninathubutu kusema JK hana uzito wa kumsafisha Lowassa.
 
Lowassa ni fisadi nguli, hafai kabisa kabisa kuwa kiongozi wa ngazi yoyote ya kisiasa duniani.
 
Lowassa ni fisadi nguli, hafai kabisa kabisa kuwa kiongozi wa ngazi yoyote ya kisiasa duniani.

Tatizo ni kwamba akitaka gombea atagombea na atapitishwa na CCM, shida iliyopo ni kwamba magamba hawatathubutu face reality kusolve problem ya hizi kashfa ila watatmia nguvu kulazimisha ushindi kama walivyoanza. kwa hiyo si mbaya tukajadili reality nao waione.
 
Lowassa awatimulia vumbi Sitta, Membe
Send to a friend
Tuesday, 02 October 2012 20:31

lowassa-top-safi.jpg
Waziri Mkuu wa zamani, Edward Lowassa

APANGA MAJESHI YA URAIS 2015, ASEMA MONDULI NDIYO MSULI WAKE WA KISIASA
Waandishi Wetu
KAMBI zinazosigana ndani ya CCM zinaonekana kuchuana vikali katika uchaguzi wa ngazi ya wilaya ya chama hicho tawala, kuelekea Uchaguzi Mkuu wa 2015, huku Waziri Mkuu wa zamani, Edward Lowassa akionekana kupata mafanikio, ikilinganishwa na mahasimu wake, Benard Membe na Samuel Sitta.

Kama ilivyo kwa Lowassa, Sitta ambaye ni Waziri wa Ushirikiano wa Afrika Mashariki na Membe ambaye ni Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, wamekuwa wakitajwa kuwa kwenye harakati za kuusaka urais, hivyo uchaguzi wa ndani wa CCM ni fursa ya kupanga safu za kufanikisha mikakati hiyo.

Lowassa binafsi tayari amepita katika kinyang'anyiro hicho kwa kuchaguliwa kwa kishindo kuwa mjumbe wa Halmashauri Kuu ya Taifa (NEC) ya CCM kupitia Wilaya ya Monduli. Jana mbunge huyo wa Monduli alitoa kauli kali akisema kuwa wapo watu wanaovuruga CCM katika Wilaya ya Monduli na kwamba tayari amewabaini, hivyo kuahidi kwamba watashughulikiwa kisiasa.

''Yako maneno ya ovyoovyo yamekuwa yakipikwa ya kuwaandama viongozi wa CCM Monduli, yanasemwa na wakubwa fulani, yanapikwa na watu fulani wa Monduli, tunawajua. Nataka kuwaambia tumewajua na nawaambia hawatuwezi,'' alitamba Lowassa.

Lowassa alisema ushindi alioupata umedhihirisha kuwa ana misuli ya kisiasa na kwamba wakazi wa Monduli ndiyo msuli huo.

''Kuna mzee rafiki yangu aliniambia kuwa katika kazi za siasa angalia ‘grassroots'. Watu wanakuwa ndiyo msuli wako kisiasa na mimi watu wa Monduli ndiyo msuli wangu,'' alisema.

Aliendelea ''Wananchi wa Monduli mmenithibitishia hilo na nawashukuru sana kutoka kwenye ‘sakafu' ya moyo wangu, jibu la thibitisho hilo kwangu ni utumishi uliotukuka.''

Kwa upande wake, Membe anasubiri kuparurana na vigogo wenzake katika kundi la kifo la ujumbe huo katika uchaguzi wa ngazi ya Taifa, wakati Sitta tayari ni mjumbe wa NEC akiwakilisha wabunge wa CCM katika chombo hicho kikubwa cha uamuzi ndani ya chama hicho.

Matokeo katika maeneo kulikomalizika uchaguzi wa ngazi ya wilaya yanaonyesha kuwa Lowassa amefanikiwa kupanga safu yake vizuri zaidi, ikilinganishwa na wenzake hao.

Membe anaonekana kufuata kwa karibu na Sitta ni kama anashika mkia kwa kuwa na wafuasi wachache waliofanikiwa kuchaguliwa. Hata hivyo, chaguzi katika baadhi ya mikoa bado zinaendelea, huku uchaguzi wa ngazi za mikoa na taifa ukisubiriwa kwa hamu.

Manyara na Arusha
Kundi la Lowassa lilizidi kupata nguvu baada ya mfuasi wake mpya ambaye ni Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Uwezeshaji na Uwekezaji), Dk Mary Nagu kumbwaga Waziri Mkuu Mstaafu, Frederick Sumaye.

Sumaye naye anatajwa kuwa miongoni mwa ‘wanaoutaka' urais na kuanguka kwake katika uchaguzi wa Hanang, kunatia doa kubwa harakati zake hizo.

Katika uchaguzi uliofanyika jana kwenye Wilaya ya Arusha Mjini, Lowassa ameibuka kidedea kwa wapambe wake kadhaa kuchaguliwa, huku mwenyekiti wa zamani wa CCM wa Wilaya hiyo, Jubilate Kileo akiangushwa na Dk Wilfred Ole Soilel.

Katika kinyang'anyiro cha mjumbe wa Nec, Godrey Mwalusamba alishinda na kuwaangusha vibaya wapinzani wake ambao ni Loota Laiser na Dk Harold Adamson.Kuchaguliwa kwa Dk Ole Soilel anayehusishwa na kambi la Lowassa kuliibua simanzi kwa kambi nyingine ambapo katika hali isiyo ya kawaida, Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Magesa Mulongo na Katibu wa CCM Arusha, Mary Chatanda walionekana kuwa wanyonge muda wote.

Mwanza na Dodoma
Mkoani Mwanza, kambi za Lowassa na Membe zinatajwa kuchuana vikali huku kukiwa na sintofahamu kwamba mgombea wa nafasi ya mweyekiti wa mkoa huo, Anthony Diallo yuko upande upi.

Diallo ambaye alianguka katika uchaguzi wa ubunge Oktoba 2010, anaonekana kurejea kwa nguvu mpya, kwani tayari baadhi ya wale wanaotajwa kuwa wafuasi wake wametwaa nafasi muhimu katika uchaguzi wa wilaya.

Hata hivyo, kada huyo wa siku nyingi wa CCM ambaye anamaliza muda wake wa ujumbe wa NEC akiuwakilisha Mkoa wa Mwanza, anakabiliwa na kibarua kigumu Oktoba 13, mwaka huu, atakapopambana na mweyekiti anayetetea nafasi yake Clement Mabina, Zebedayo Athumani na Joseph Langula Yared.

Kwa sasa kuna taarifa kwamba Diallo anamuunga mkono Membe hivyo ushindi wa wafuasi wake katika Wilaya za Nyamagana, Ukerewe, Misungwi na Sengerema unaweza kuinufaisha kambi hiyo.

Mabina ambaye anatajwa kuwa mshirika wa Lowassa, katika matokeo ya awali, kambi yake inaonekana kutokufanya vizuri.

Ushindi muhimu katika Wilaya ya Nyamagana ulikuwa ni wa nafasi ya Mwenyekiti iliyonyakuliwa na msadizi wa siku nyingi wa Diallo, Raphael Shilatu, ambaye aliwabwaga Mashaka Kaguna aliyetajwa kuwa mfuasi wa Lowassa na Yahya Nyaonge anayetajwa kuwa mfuasi wa Sitta.

Hata hivyo, ushindi huo unatajwa kutiwa doa na mmoja wa wafuasi wa Lowassa ambaye ni mbunge wa zamani wa Nyamagana, Lawrence Masha ambaye alikuwa mjumbe wa NEC.

Wilayani Ukerewe kambi ya Membe inatajwa kushinda kiti cha Uenyekiti kupitia Ally Mabile na katika Wilaya ya Busega kambi ya Sitta inatajwa kutwaa ujumbe wa NEC kupitia kwa mbunge wa zamani wa Busega, Dk Raphael Chegeni.

Mkoani Dodoma matokeo ya uchaguzi wa nafasi mbalimbali yanaonyesha kwamba kambi ya Lowassa imefanya vizuri hasa katika Wilaya za Dodoma Mjini, Bahi, Kondoa, Chemba na Kongwa.

Hata hivyo, ngome ya Waziri Mkuu huyo wa zamani imeangukia pua katika Wilaya ya Chamwino, baada ya wapambe wake kubwagwa na wale wanaotajwa kumuunga mkono Sitta. Katika Wilaya ya Mpwapwa viongozi waliochaguliwa ni wapya na hadi sasa haifahamiki wanaunga mkono kambi gani.

Dar, Zanzibar na Moro
Visiwani Zanzibar, Lowassa aliendelea kupeta kutokana na ushindi wa aliyewahi kuwa Mwenyekiti wa Umoja wa Vijana (UVCCM), Hamad Yussuf Masauni, ambaye alishinda nafasi ya ujumbe wa NEC na kumbwaga aliyekuwa Naibu Waziri wa Habari Utamaduni na Michezo, Mahamoud Thabiti Kombo.
Akitangaza matokeo ya uchaguzi huo Katibu wa Wilaya ya Mjini, Fatma Juma Shomari alisema kwamba kati ya wagombea 19 waliokuwa wakiwania nafasi sita za NEC, Masauni aliibuka mshindi wa pili akitanguliwa na Naibu Katibu Mkuu wa CCM Zanzibar, Vuai Ali Vuai.
Aliyeshinda nafasi ya uenyekiti ni Juma Faki Chumu na wajumbe wengine wa NEC ni Buruhani Saadati Haji, Asha Abdalla Juma, Talib Ali Tali Sufiani Khamis Ramadhani na Omar Jastus Morris.
Hata hivyo, katika Mkoa wa Dar es Salaam, kambi ya Lowassa ilipata pigo kutokaana na kubwagwa kwa Naibu Waziri wa Kazi na Ajira, Dk Makongoro Mahanga aliyekuwa akiwania nafasi ya ujumbe wa NEC kupitia Wilaya ya Ilala.

Kadhalika mkoani Morogoro, kambi hiyo pia ilipata pigo kutokana na Naibu Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo, Amos Makala kubwagwa na Suleiman Ahmed Sadiq katika uwakilishi wa NEC Wilaya ya Mvomero.

Taarifa kutoka mkoani Tabora zinasema katika wilya zote za mkoa huo, kambi ya Lowassa imeshinda kwa kishindo isipokuwa Wilaya ya Urambo ambayo kambi ya Sitta inadaiwa kuibuka kidedea.


Wasomi wanena
Baadhi ya wasomi nchini, wametofautiana kimtazamo kuhusu chaguzi ndani ya CCM huku wengine wakisema chama hicho kimeshindwa kuwadhibiti vigogo wanaotajwa kuwania nafasi ya urais ambao wamefanikiwa kuwaingiza wafuasi wao kwenye nafasi mbalimbali za uongozi.

Mhadhiri wa Chuo cha Kumbukumbu cha Mwalimu Nyerere, Sabun Parit alisema hatma ya chama hicho kuelekea Uchaguzi Mkuu ujao ni nzuri kutokana na kufanikiwa kuendesha uchaguzi wake kwa utulivu.

"Mara nyingi tumezoea kuona makundi yakiibuka wakati wa uchaguzi, lakini safari hii hali ni shwari, hatujasikia makundi wala malalamiko na hii ni ishara kwamba hiki chama kimekomaa na hakiwezi kutetereka," alisema mhadhiri huyo.

Mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM), Dk Kitilya Mkumbo ambaye pia ni Mjumbe wa Kamati Kuu ya Chadema alisema jana kuwa CCM imeshindwa kuwadhibiti vigogo hao ndani ya chama hicho na hivyo wameanza vizuri katika maandalizi ili kupitishwa na chama hicho kugombea kiti ya urais.

"Kwa kweli CCM wamejimaliza na wameonekana kuwa hawana jipya, wale waliotaka kuwavua magamba ndiyo haohao wamepitishwa kwenye uchaguzi pamoja na wafuasi wao kuwasaidia katika Uchaguzi Mkuu," alisema Dk Mkumbo.

Naye Mhadhiri wa UDSM, Dk Benson Bana alisema CCM imeonyesha kwamba hakuna kiongozi yeyote mwenye hatimiliki ya chama hicho.

"Kwa namna mambo yalivyoonyeshwa kwenye uchaguzi huo, mtu yeyote anaweza kuingia na kuondoka kwenye chama hicho," alisema.

Naye Kisena Mabuba ambaye pia ni Mhadhiri katika Chuo cha Mwalimu Nyerere alisema uchaguzi huo umefuta makundi ndani ya CCM.

"Tofauti na matarajio ya wengi kuwa CCM ingemeguka, mimi ninachokiona hapa kundi lililobaki na nguvu ni lile la mwenyekiti mwenyewe. Kundi moja limefutwa kabisa na mengine yameshindwa kupata nguvu za kutosha," alisema Mabuba.

Alitaja mbinu zilizotumika kufuta makundi hayo kuwa ni hatua ya kubadili katiba na kuwaweka pembeni marais wastaafu pamoja na uteuzi wa makatibu wa chama ngazi ya mikoa na wilaya ambao walifanya makundi kupoteza nguvu.

Habari hii imeandikwa na Moses Mashalla (Arusha), Habel Chidawali (Dodoma), Frederick Katulanda (Mwanza) na Joseph Zablon, Raymond Kaminyoge na George Njogopa.
Source:Mwananchi

Waiting for the next episode...before we come back to hot issue ya kumsafisha huyu mheshimiwa.
 
Sumaye kaamsha hisia nyingine.Kama anayo nia ya kuondoka na akitangaza vizuri kuondoka kwake atakuwa kamaimaliza CCM,kwani wengi wanaoona kuwa hawana chao tena watafuatia kwa kasi ya jabu .Kasi watakayoondokea watu itawapa mashaka wengine na baadaya kuwapa moyo wa kuondoka na ili wawahi number.Ni vyema kafanya mapema kabla dealine ya CDM haijaisha.

Akifanya hayo maamuzi itakuwa salama kwake mbele ya chama cha kigaidi kama ccm otheriwise hakuna histori ya viongozi wenye mashaka wanaodunu ktk hii nchi.Ila kwenda upinzani akutamlinda na chochote cha kuangamiza.Akigeuka takuwa chumvi.
 
kuna mweny tathmini ya alichoachieve EL ktk chaguzi za CCM?Na kwa kiasi gani kaweza itawala CCM,ili tujuwe anaenda vipi kuiua CCM na kufika ktk ballot akiwa hana chama huku harufu ya uhafu wa CCM ikimfuata hadi walipo wapiga kura.
 
JK akiri kuwa wanaweza fika ktk uchaguzi mkuu wakiwa wamechoka sana kama wataendelea kuharibiana.NI wazi anasupport hii nortion kuwa uchaguzi mkuu. CCM watafika ama Mgombea wao kuwa Mzigo, ama chama kuwa mzigo, ama wote kuwa mzigo kwa pamoja na si vinginevyo.
 
JK bana - Nyoka wote wana ndimi mbili!...

Haha.....usishange ndugu hii ni Africa.Watu hawapo serious kwa kila kitu.Mtu anatumia vitu asivyovijua kama mfano.Halafu mbaya kile kinachodhoofisha mfano wake ndicho kachagua. "Ulimi".

wenzetu wanatupiga bao kwa vile walishazoea kucheza "best examples na si just an Example", sasa sisi wa habari za sunrgura mjanja, tuna mifano rahisi tuu,na mtu akiuliza ni rahisi kumzimisha kwa neno "whatever lakini si umeelewa".JK akifany amzaha mkutano utamgeukia vibaya,wengine wapo serious ktk mipango yao leo pale.
 
JK mwenyekiti wa chama kinachojiita chama dume, leo anatoa mipasho anajipa challengi nyingine ambayo ni impossible kama si suicidal.Anakiri kuwa watafika ktk uchaguzi wakiwa dhaifu, anonyesha jinsi Kivuli cha CDM "the Honey Badger" kinavyowatisha,anasema wazi kuwa ccm ina novices na mengine mengi sana niliyowahi yadokeza kwa kuweka thread kabisakuhusu CCM.

NI wazi mambo yanelekea kuiva na nyota ya 2015 itang`aa kwa watanzania.There is no stop time hipo tena CCM kuangali ataifa kwa ujumla,sasa hivi ni urais na kujinasibu na kambia fulani ili watu waje pata fadhila kama za wale waliopiga bingo kwa kuwa karibu za Rizwani wakati mzee alipotawazwa kuwa presidaa.Watu watauwa busy kuwekeza,na hii itaanzia kwa viongozi , wafanyakazi wa umma na wa taasisi binafsi .Kila mtu atakuwa busy sana kujiweka kwa mgombea potential.
 
Back
Top Bottom