Kama kuna uwezekano (kifedha) Kitengo cha CID kiwe taasisi kamili inayojitegemea

Stroke

JF-Expert Member
Feb 17, 2012
34,635
40,790
Kutokana na mfumo wa Jeshi la polisi ulivyo, kitengo Cha CID kipo chini ya jeshi Hilo ambapo mkuu wa kitengo hicho ni mmoja wa wasaidizi wa IGP anayeshughulika na upelelezi wa makosa makubwa ya Kijinai "serious offences/crimes"

Hivyo kiutendaji watumishi katika kitengo hicho wanategemewa kuwa na ujuzi wa ziada katika tasnia ya upelelezi wa makosa ya jinai.

Kwakua kwa hivi karibuni kumetokea na malalamiko ya kubambika na kuchelewa Kwa kesi sio vibaya tukawa na taasisi maalum ambayo inajitegemea itayokuwa na jukumu la kufanya upelelezi wa makosa makubwa ya kijinai yatayofanyika hapa nchini na hata nje ya nchi kama itabidi kuwa hivyo kulingana na mazingira ya kosa litalofanywa nje ya nchi.

Hii itaifanya jeshi la polisi kupunguziwa mzigo mkubwa wa kimajukumu ililonalo Sasa ambalo Naona kama ndio kikwazo Cha baadhi ya kesi kuchukua muda mrefu kukamilika.

Taasisi hii mpya itakuwa na muda na ikiwezeshwa kuwa na wataalam na vifaa itasaidia pakubwa katika kuharakisha upelelezi wa kesi.

Polisi wabakie na jukumu lao mama la Ulinzi wa Raia na Mali zao, pamoja na kuzuia kutendeka Kwa makosa ya jinai, na kuhakikisha kuna utulivu na Sheria zinazingatiwa na Raia.
 
Kutokana na mfumo wa Jeshi la polisi ulivyo, kitengo Cha CID kipo chini ya jeshi Hilo ambapo mkuu wa kitengo hicho ni mmoja wa wasaidizi wa IGP anayeshughulika na upelelezi wa makosa makubwa ya Kijinai "serious offences/crimes"

Hivyo kiutendaji watumishi katika kitengo hicho wanategemewa kuwa na ujuzi wa ziada katika tasnia ya upelelezi wa makosa ya jinai.

Kwakua kwa hivi karibuni kumetokea na malalamiko ya kubambika na kuchelewa Kwa kesi sio vibaya tukawa na taasisi maalum ambayo inajitegemea itayokuwa na jukumu la kufanya upelelezi wa makosa makubwa ya kijinai yatayofanyika hapa nchini na hata nje ya nchi kama itabidi kuwa hivyo kulingana na mazingira ya kosa litalofanywa nje ya nchi.

Hii itaifanya jeshi la polisi kupunguziwa mzigo mkubwa wa kimajukumu ililonalo Sasa ambalo Naona kama ndio kikwazo Cha baadhi ya kesi kuchukua muda mrefu kukamilika.

Taasisi hii mpya itakuwa na muda na ikiwezeshwa kuwa na wataalam na vifaa itasaidia pakubwa katika kuharakisha upelelezi wa kesi.

Polisi wabakie na jukumu lao mama la Ulinzi wa Raia na Mali zao, pamoja na kuzuia kutendeka Kwa makosa ya jinai, na kuhakikisha kuna utulivu na Sheria zinazingatiwa na Raia.
Kwa mfano wa nchi gani duniani !!?? Sana sana jibu ni katiba mpya ,iondoe Tanzania police force iwe Tanzania police services kama ilivyo kenya na baadhi kwingineko duniani ,
 
Kwani Job Description iweje.

May be lakini naona ni ngumu. Ni sawa na useme unga uive peke yake na maji yaive peke yake bila kuvichanganya. Cz CID ni Polisi huyohuyo. Anauwezo wa kukamata, Kuhoji, Kupekua, kupeleleza. Naona sijui umewaza Jambo gani nje ya Boksi
Unajua hata prosecutors zamani walikuwa ni polisi na pia kitengo cha madawa ya kulevya ilikuwa polisi? Kimsingi upelelezi ni fani unayoweza kusomea hata mtu wa kawaida maana kuna upelelezi wa aina nyingi ikiwemo forensic, masuala na mitandao nk.

Kuwa mpelelezi haihitaji uwe na mbinu za kipolisi ndio maana hata polisi wanasomea upelelezi sio kozi ambayo kila polisi anaisoma na sio kitengo ambacho kila polisi anapangiwa na hata ukipangiwa ni lazima utapelekwa kusomea.

Kumbuka hata Mambo ya rushwa zamani ilikuwa chini ya polisi tatizo linakuja polisi kukamata na kuchunguza huwa ni shida sana sasa wakiona wamekusingizia wao huamua kukuzungusha tu wakukomeshe na wakienda mahakamani wanasema uchunguzi haijakamilika.

Ndio maana siku hizi DPP anaamua kufuta kesi sababu unakuta kesi inafunguliwa analaumiwa DPP as if yeye ndio alikamata na ndio anayefanya uchunguzi.

Angalia hata tume ya madawa ya kulevya, zamani ilikuwa kikosi chini ya polisi tu, lakini sasa ni Tume maana no hatari sana kumuachia polisi adeal na masuala ya madawa ya kulevya na huyohuyo akamate.

So mie naona ni sahihi DCI awe Mamlaka inayojitegemea.
 
Kwa mfano wa nchi gani duniani !!?? Sana sana jibu ni katiba mpya ,iondoe Tanzania police force iwe Tanzania police services kama ilivyo kenya na baadhi kwingineko duniani ,
Mfano, Marekani anayepeleleza jinai ni FBI (Federal Bureau of Investigation) lakini hata nchi nyingi za Ulaya pia anayepeleleza kesi sio polisi. Polisi wanaweza kuhusishwa kwenye upelelezi kama itahitajika Ila huwa sio kazi yao wao watasubiri tu report. Lakini pia kuna makosa ambayo polisi anaweza kupelekeza kama kuvuta bangi, kupigana sijui kutukanana, vibaka Ila ujambazi, madawa ya kulevya, mauaji, organised criimes, rushwa hizo ni federal offense zinazochunguzwa na FBI
 
Baadae Takukuru wawe jeshi lakukamata
Hapana mkuu,

Hiyo kukamata atabakia nayo Polisi, na pia investigation ya petty offences Ila serious crimes inayohitaji muda , utaalam na vifaa viende kwenye taasisi mpya ya CI , hapo hata vijana na wataalam wengine watapata nafasi ya kulitumikia Taifa lao, Ila Kwa sasa kitengo kimemezwa na Jeshi la Polisi ufanisi unakua mdogo na matokeo yake ndio kama haya kesi zinaru dikana mahakamani kikwazo kikiwa kuwa upelelezi haujakamilika.
 
Jamani Jamani;

Hili lizingatiwe kuongeza ufanisi wa utendaji wa Jeshi la Polisi na kupunguza mikasa na malalamiko ya kila mara.

Tuna mifano hai mpaka sasa ambayo inatufanya jambo hili tulitekeleze bila kuchelewa.
 
Kutokana na mfumo wa Jeshi la polisi ulivyo, kitengo Cha CID kipo chini ya jeshi Hilo ambapo mkuu wa kitengo hicho ni mmoja wa wasaidizi wa IGP anayeshughulika na upelelezi wa makosa makubwa ya Kijinai "serious offences/crimes"

Hivyo kiutendaji watumishi katika kitengo hicho wanategemewa kuwa na ujuzi wa ziada katika tasnia ya upelelezi wa makosa ya jinai.

Kwakua kwa hivi karibuni kumetokea na malalamiko ya kubambika na kuchelewa Kwa kesi sio vibaya tukawa na taasisi maalum ambayo inajitegemea itayokuwa na jukumu la kufanya upelelezi wa makosa makubwa ya kijinai yatayofanyika hapa nchini na hata nje ya nchi kama itabidi kuwa hivyo kulingana na mazingira ya kosa litalofanywa nje ya nchi.

Hii itaifanya jeshi la polisi kupunguziwa mzigo mkubwa wa kimajukumu ililonalo Sasa ambalo Naona kama ndio kikwazo Cha baadhi ya kesi kuchukua muda mrefu kukamilika.

Taasisi hii mpya itakuwa na muda na ikiwezeshwa kuwa na wataalam na vifaa itasaidia pakubwa katika kuharakisha upelelezi wa kesi.

Polisi wabakie na jukumu lao mama la Ulinzi wa Raia na Mali zao, pamoja na kuzuia kutendeka Kwa makosa ya jinai, na kuhakikisha kuna utulivu na Sheria zinazingatiwa na Raia.
KATIBA MPYA ndio Suluhisho wa Yote hayo
 
Jamani Jamani;

Hili lizingatiwe kuongeza ufanisi wa utendaji wa Jeshi la Polisi na kupunguza mikasa na malalamiko ya kila mara.

Tuna mifano hai mpaka sasa ambayo inatufanya jambo hili tulitekeleze bila kuchelewa.
Wazo zuri sana.....kama ambavyo ' Fbi' inajitegemea ila ipo chini ya idara ya sheria na haki ya Serikali kuu ya Marekani

Hapa kwetu tutafute namna tutakavyokifanya hichi kitengo wateule wake wasiwe kwa sababu za kisiasa.
 
Wazo zuri sana.....kama ambavyo ' Fbi' inajitegemea ila ipo chini ya idara ya sheria na haki ya Serikali kuu ya Marekani

Hapa kwetu tutafute namna tutakavyokifanya hichi kitengo wateule wake wasiwe kwa sababu za kisiasa.
Wameelemewa wasaidiwe.
 
Rwanda walilitambua hili mapema na wakatenganisha polisi na idara ya upelelezi ili kupunguza mlundikano wa majukumu,malalamiko na ucheleweshaji wa upelelezi..

... hata hapa kwetu Tz nadhani ni wakati sahihi wa kufanya hivyo.
Nakubaliana na wewe.
 
Rwanda walilitambua hili mapema na wakatenganisha polisi na idara ya upelelezi ili kupunguza mlundikano wa majukumu,malalamiko na ucheleweshaji wa upelelezi..

... hata hapa kwetu Tz nadhani ni wakati sahihi wa kufanya hivyo.
Rwanda ni nchi ya kidekteta na polisi wake wanafanya kazi kutokana na matakwa ya wanasiasa waliowekwa na Kagame badala ya weledi.
 
Rwanda ni nchi ya kidekteta na polisi wake wanafanya kazi kutokana na matakwa ya wanasiasa waliowekwa na Kagame badala ya weledi.
Na Rwanda imekua Ni ya 1 kwa kuongoza in terms of rule of law Kati ya nchi 33 za Sub-Saharan Africa.

Na globally kwny rule of law Rwanda Ni ya 42,kwa Nchi nyingine za huku E/Africa Tz Ni ya 100,Kenya ya 106,Uganda ya 125

Source Ni The World Justice Project(WJP) mwaka 2021.
 
11 Reactions
Reply
Back
Top Bottom