kwisha
JF-Expert Member
- Sep 9, 2021
- 1,666
- 4,365
Mimi siyo Mtanzania ni Mkongo, ila nilijikuta nimependa timu hii ya Tanzania kuliko kawaida na aliyenivutia kwenye timu hii ni Makambo. Mwaka 2018 nilitokea kuwa na mapenzi ya dhati na uchezaji wake, nilikuwa naona clip zake nyingi YouTube.
Mpaka nikajikuta ata Yanga pia nimetokea kuipenda sana na kuvutiwa na Yanga mpaka sasa hivi. Kibaya ni kwamba kila wakati timu hii inapofanya vibaya najikutaga nina hasira ya ajabu.
Maana katika watu ambao ni waoga kushindwa mara pili au mara tatu mimi ni wa kwanza. Huwa sipendi kushindwa au kuona kitu changu chochote au ndugu, rafiki ameshindwa jambo moja mara 2 au zaidi.
Ila nilichogundua, hii timu siyo kwamba uwezo wa kufika mbali hawana, wanao ila hawana bahati tu!
Mpaka nikajikuta ata Yanga pia nimetokea kuipenda sana na kuvutiwa na Yanga mpaka sasa hivi. Kibaya ni kwamba kila wakati timu hii inapofanya vibaya najikutaga nina hasira ya ajabu.
Maana katika watu ambao ni waoga kushindwa mara pili au mara tatu mimi ni wa kwanza. Huwa sipendi kushindwa au kuona kitu changu chochote au ndugu, rafiki ameshindwa jambo moja mara 2 au zaidi.
Ila nilichogundua, hii timu siyo kwamba uwezo wa kufika mbali hawana, wanao ila hawana bahati tu!