Erythrocyte
JF-Expert Member
- Nov 6, 2012
- 117,618
- 218,040
Wakuu natanguliza salamu , baada ya salamu najikita kwenye mada bila kuremba , kwa mtu yeyote anayedhani anaweza kuua Chadema kwa njia yeyote anayoitumia , iwe biashara ya binadamu , iwe kwa kutumia MA DC , MA RC ama labda kwa kutumia polisi au watu wasiojulikana basi afya yake ya akili itazamwe upya
Baada ya kwenda Lusaka nchini Zambia kwa usafiri wa anga na kuhudhuria onyesho la Music la Koffie Olomide Mopao ( ikumbukwe kwamba mimi ni Kijana Tajiri na mpenzi wa kutupwa wa music wa kikongo , ambao kwa sasa si rahisi kuupata nchini Tanzania baada ya mapromota wote kufirisika kutokana na matatizo makubwa ya uchumi ) nikaamua kufanya ziara maalum kwa kutumia gari ili kukagua uhai wa Chadema , Nimepita Nyanda za Juu kusini , kwa maana ya mikoa ya Rukwa , Songwe , Mbeya na wilaya zake zote , Iringa , Njombe na kumalizia mkoa wa Ruvuma , ama kwa hakika ukiwa na akili timamu huwezi hata kuthubutu kufikiria kuua chadema achilia mbali kutamka hadharani.
Mizizi iliyojikita nayo Chadema kwenye eneo hili si tu kwamba si rahisi kuing'oa bali haiwezekani kamwe ! Chadema inaongoza mitaa , kata na halmashauri kadhaa na jambo kubwa zaidi ni namna wananchi wanavyoheshimu uongozi wa chadema kwenye maeneo yao
Taarifa nilizokusanya zinaonyesha kwamba ile mbinu ya kizamani ya kuhonga vibaba vya unga ili kushawishi wananchi kuunga mkono ccm kwenye ukanda huu imegonga mwamba kutokana na uwezo wa wananchi wa eneo hilo kujitosheleza karibu kwa kila kitu hivyo kuwa na uwezo wao wa kiuchumi
Nguzo kuu ya Chadema ni utulivu wa viongozi wake unaotokana na weredi na usomi wao , kama unataka kupoteza muda wako endelea na mawazo mgando ya kudhani unaweza kuua chadema
Baada ya kwenda Lusaka nchini Zambia kwa usafiri wa anga na kuhudhuria onyesho la Music la Koffie Olomide Mopao ( ikumbukwe kwamba mimi ni Kijana Tajiri na mpenzi wa kutupwa wa music wa kikongo , ambao kwa sasa si rahisi kuupata nchini Tanzania baada ya mapromota wote kufirisika kutokana na matatizo makubwa ya uchumi ) nikaamua kufanya ziara maalum kwa kutumia gari ili kukagua uhai wa Chadema , Nimepita Nyanda za Juu kusini , kwa maana ya mikoa ya Rukwa , Songwe , Mbeya na wilaya zake zote , Iringa , Njombe na kumalizia mkoa wa Ruvuma , ama kwa hakika ukiwa na akili timamu huwezi hata kuthubutu kufikiria kuua chadema achilia mbali kutamka hadharani.
Mizizi iliyojikita nayo Chadema kwenye eneo hili si tu kwamba si rahisi kuing'oa bali haiwezekani kamwe ! Chadema inaongoza mitaa , kata na halmashauri kadhaa na jambo kubwa zaidi ni namna wananchi wanavyoheshimu uongozi wa chadema kwenye maeneo yao
Taarifa nilizokusanya zinaonyesha kwamba ile mbinu ya kizamani ya kuhonga vibaba vya unga ili kushawishi wananchi kuunga mkono ccm kwenye ukanda huu imegonga mwamba kutokana na uwezo wa wananchi wa eneo hilo kujitosheleza karibu kwa kila kitu hivyo kuwa na uwezo wao wa kiuchumi
Nguzo kuu ya Chadema ni utulivu wa viongozi wake unaotokana na weredi na usomi wao , kama unataka kupoteza muda wako endelea na mawazo mgando ya kudhani unaweza kuua chadema