Kama Kikwete anamjua Rais 2015, Kuna haja gani ya kupoteza mabilioni ya Fedha kwenye Uchaguzi?

Albedo

JF-Expert Member
Feb 24, 2008
5,559
1,452
CCM kupitia kwa Umoja wa Vijana wa CCM Babamoyo (UVCCM) Ilitoa tamko ambalo pamoja na Mambe mengi lilikuwa na Kauli mbili nzito zifuatazo

1. Kamwe Rias 2015 Hatotoka Kaskazini.

2. Anayemjua Rais 2015 ni Jakaya kikwete

Kauli hii ya Kibaguzi dhidi ya Watu wa Kanda ya Kaskazini Ilipita bila kutolewa kwa Kauli ya Kupingwa kutoka kwa Viongozi wa CCM hali inayoashiria kwamba Kauli hii ilikuwa na Baraka za Wakubwa wa CCM na Watu wa Kaskazini "Mlie tu". Lakini kilichonishtua kwa kiasi kikubwa ni Kauli kwamba anamyemjua Rais 2015 ni Kiwete.

Sasa najiluliza kama Kikwete anamfahamu Rais 2015 kuna haja kweli ya Kuitisha Uchaguzi wa Kudanganyana na kupoteza Pesa Nyingi.

Je Watu wa Kaskazini Wameikosea ni CCM? Mbona CCM inawatenga hivyo watu wa Kaskazini? Je hii yaweza kuwa Sababu ya Watu wa Kaskazini Kuichukia CCM kwa Sababu imeamua Kuwahakikishia kwamba Hawana haki ya Kukanyaga Magogoni?
 
CCM wabaguzi sana nilimsikia Mukama naye akisema sasa ni zamu ya wapi sijui, wanagawa urais kama mafungu ya nyanya. Nafikiri kuna haja ya viongozi wa CDM kuifufua upya hoja hii na waitangaze kwa nguvu zao zote majukwaani. Watuambie CCM walikuwa na maana gani, tena ikiwezekana Mbowe kama ananisoma kesho aligusie suala hili kama Kikwete anamjua rais ajae kuna haja gani ya uchaguzi.
 
Albedo,
Nitakupa sababu chache tu kwa nini Watanzania wapige kura mwaka 2015.
1/ Uongozi mbovu wa Kikwete, na kwa hiyo hana haki ya kutuchagulia mrithi maana atakayemrithi atakuwa mbaya kama yeye au hata zaidi.
2/ Tanzania lazima ibadilike ama sivyo tunarudishwa kwenye ukoloni mamboleo na sera za viongozi wa sasa wa CCM
3/ Kama wasemavyo wazungu "you can make a difference." Piga kura yako na hakikisha inahesabiwa kisahihi. Hapo tutaona mwanzo wa Tanzania mpya tunayoitaka.
 
Mkuu umenikumbusha kitu. Mimi binafsi sielewi kwa nini Chama kiweke utaratibu kama huo eti kwamba kuna mtu wa ukanda fulani hawezi kuwa Rais wa Tanzania! Mbona hao marais wanaotoka mahali pengine bado hawajaikwamua Tanzania katika matatizo yake sana sana yanazidi. Yaani bado tuendelee kuamini ukanda badala ya uwezo wa mtu? Inashangaza!!
 
ccm wanajua kua kaskazini hawana majimbo..mwanza, arusha kote kule ni cdm... so wao wanaconcentrate kanda ya kusini na kati ndio bado wako popular...bt watake wasitake Rais 2015 atatokea kaskazini... unless wachakachue kura kama walivyofanya mara ya mwisho...
 
Hichi ndicho kinanifanya niunge mkono hoja ya Mangi Marealle na Joshua Nasary. Kwakuwa ccm na viongozi wake wamehamua kubip na sisi tupige' wamehamua kupika na sisi tupakue.
 
Kwenye nchi ya kidemokrasia kama yetu haiwezekani tupangiwe rais atoke wapi. Nimekuwa nikisikia watu wakisema eti rais hawezi kutoka makabila fulani fulani kama wasukuma, wanyakyusa kisa ni makabila makubwa, hizi ni sababu za kijinga kabisa. Sasa imefikia wakati tuamuke kama tulirithi mambo mabaya ya Nyerere tuyaache tuchukue yale yake mazuri. Kama vipi next president awe msukuma tumechoka na watu wa pwani kwa vile tu tukabila twao tudogo.
 
Back
Top Bottom