Kama kazi tunastaafu kwa nini mapenzi tusistaafu?

Equation x

JF-Expert Member
Sep 3, 2017
28,810
39,018
Mapenzi ni kitu kingine, huwezi kufananisha na kitu chochote kile;
Kwa wale waliofanikiwa kupendwa ni vigumu kuamini kuwa, kuna wengine mapenzi yamewagharimu maisha yao yote au yamepoteza dira ya maisha ya watu wengine.

Wapo ambao mapenzi yamewachapa mpaka kupoteza mwelekeo na hawatamani tena kusikia hilo neno mapenzi. Mpaka wengine wanafikia kusema wamestaafu kwenye mapenzi.

Na ukitaka kujua waliochapwa na mapenzi, wengi wana sifa hizi:-
  • Kuvaa viatu vilivyoisha soli upande mmoja
  • Kuvaa shati lililochanika kwenye kola,mikono n.k
  • Kuvaa nguo zilizopauka
  • Kuwa mchafu mchafu
  • Kuvaa mkanda uliobabuka
  • Kuvaa viatu ambavyo havijapigwa kiwi
  • Kuvaa vazi lisilokuwa na mvuto
  • Wanakuwa na hasira kali muda wote
  • Akitembea anashtukashtuka
  • n.k
 

Similar Discussions

0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom