Kama katika uongozi wa miaka mitano ya Bunge Magufuli alichoona cha maana kwa Ndugai ni kuundwa Kamati ya Madini tu, basi Ndugai hafai kuwa Spika

Synthesizer

JF-Expert Member
Feb 15, 2010
11,023
18,566
NImeshangaa sana. NImeona upungufu mkubwa kwa upande wa Magufuli, kwamba katika sababu ambazo angependa Ndugai arudi kuwa Spika baada ya uchaguzi, ya maana kuliko zote ni hiyo ya kuunda kamati ya madini.

Kwangu ina maana Magufuli kimsingi anakiri kwamba hakuna cha maana alichofanya Ndugai katika uongozi wake wa Bunge wa miaka mitano. Na sababu kubwa ya kusema hivi ni kwamba Spika kuunda kamati ya madini kama alivyofanya Ndugai ni utaratibu wa kawaida katika kazi za Spika, hakuna cha ziada alichofanya hapo zaidi ya kufanya kazi zake za uspika.

Kwa hiyo alichofanya Magufuli ni sawa na mteja kwenda hotelini, na kuletewa chakula alichoagiza na mhudumu wa hoteli, na mteja kuwaambia watu kwamba huyu mhudumu aendlee kuwa mhudumu hapa hotelini kwa kuwa nilipoagiza chakula aliniletea.

Hivi kweli hapo ndipo Magufuli alipotafuta sifa zote ambazo angeweza kumsifia Ndugai, na kuona hiyo ndiyo ya maana kuliko zote ya kumpigia debe? Kwangu mimi basi kuna tatizo eidha kwa Magufuli au kwa Ndugai.

Labda tuyaache hayo. IKiwa Magufuli anataka Ndugai arudi kuwa Spika, hilo linamuweka wapi Tulia Ackson katika Bunge lijalo ikiwa CCM watakuwa katika nafasi ya wingi wa kumchagua Spika? Pia kuna mambo kadhaa. Labda Magufuli ameona kuwa Tulia hawezi kumshinda Sugu kule Mbeya, au labda Tulia itabidi aridhike kuendelea kuwa Naibu Spika, au pia Tulia anaandaliwa nafasi ya uwaziri. Inawezekana pia kwamba Tulia hayupo katika hesabu za uteuzi wa Magufuli kwa sasa!

1596789462010.png
 
Kusema Ok sawa unaelewa maana yake wewe
Dogo aise chalii yangu inakuwaje? Heshima kwako. Nimeicheki iyo avatar picha yako nikaipenda sana. Rumplelstiltskin ni kitabu cha story nzuri sana za uingereza zamani kale kajitu kalikuwa kanashona viatu balaa. Zingine ni Cinderella, snow white and seven dwarfs, rapunzel
 
Ndugai anapambana sana aweke rekodi ya kushika uspika kwa at least miaka 10 akitokea unaibu spika miaka5 tofauti na watangulizi wake S. Sitta na Anna Makinda ambao waligawana miaka mitano mitano

Wakati huo huo bibi wa Mbeya kajipanga vilivyo kuukwaa uspika

Iwe iwavyo siasa za 2020-2025 tutashuhudia kila aina ya sarakasi
 
Ndugai Ni spika wa ovyo kuliko wote walio tangulia kushika uspika...
Aliunda Kamati ya Madini MKuu, kwa sababu hiyo Magufuli anaona sio wa hovyo.

Sasa naona jinsi gani kumsifia sifia Magufuli inasaidia sana watu! Kwa muda mrefu Ndugai alikuwa anaongoza Bunge utafikiri yeye ndio msemaji wa Magufuli!
 
Magufuli anapenda Spika Ndugai kwa sababu zilizo wazi.
Kwanza serikali ya Magufuli imepitisha miswaada mingi bungeni karibu yote bila shida.
Pili amewadhibiti wapinzani bila huruma.
Tatu hoja binafsi za kuifedhesha serikali ya Magufuli hazikusogea hatua ya kujadiriwa bungeni.
Nne Spika Ndugai aliunga kwa dhati serikali katika juhudi za ujenzi na ununuzi wa miradi mikubwa (Mega project)
Ulitaka apante Spika wa kumkwamisha?
 
Ndugai anapambana sana aweke rekodi ya kushika uspika kwa at least miaka 10 akitokea unaibu spika miaka5 tofauti na watangulizi wake S. Sitta na Anna Makinda ambao waligawana miaka mitano mitano

Allahu y'a alla'm..... tuwe na mazoea ya kusema Inshallah
 
Yaani mtoa mada utakuwa choko mkubwa sana wewe hilo kwa taarifa yako ni moja tu maana alizungumzia madini hapo angesema aongelee kila kitu wangekesha
 
Magufuli anapenda Spika Ndugai kwa sababu zilizo wazi.
Kwanza serikali ya Magufuli imepitisha miswaada mingi bungeni karibu yote bila shida.
Pili amewadhibiti wapinzani bila huruma.
Tatu hoja binafsi za kuifedhesha serikali ya Magufuli hazikusogea hatua ya kujadiriwa bungeni.
Nne Spika Ndugai aliunga kwa dhati serikali katika juhudi za ujenzi na ununuzi wa miradi mikubwa (Mega project)
Ulitaka apande Spika wa kumkwamisha?
Na ni wazi hawezi kusema wamchague tena kuwa Spika kwa ajili ya hizo sababu!
 
5 Reactions
Reply
Back
Top Bottom