Kama ilivyokuwa kwa Mtikila kufungua kesi ya Mgombea Binafsi, Tundu Lissu kufungua kesi kuhoji ni kwanini matokeo ya Urais hayapingwi Mahakamani!

Tila-lila2

JF-Expert Member
Oct 20, 2019
653
1,058
Tayari mpango mzuri na wenye maana kubwa sana katika Taifa letu unaendelea kuandaliwa. Uchaguzi wa Mwaka 2020 utakapokamilika tu na iwapo CCM watakuwa wameshinda kuna kesi itafunguliwa kwa umakini wa hali ya juu kuhusu kwa nini matokeo ya Urais hayapingwi Mahakamani.

Kinachozuiwa nchini mwetu ni kwa kutofungua kesi ya kupinga matokeo ya Urais lakini kuhusu kufungua kesi ya kuhoji kuwa ni "Kwa nini Matokeo ya Urais hayapingwi Mahakamani" hakujazuiwa kufunguliwa kesi.

Tundu Lissu tayari amekuwa katika maandalizi ya kufungua kesi ya hivyo mara tu Uchaguzi utakapokamilika. Iwapo Mahakama Kuu ya Tanzania itakataa kesi ya hivyo kusajiliwa kwao tayari maandalizi ya kuisajili Mahakama ya Afrika Mashariki au ya Afrika nayo yanaendelea. Ushahidi wa mambo yanayotendeka ili kujenga hoja katika kesi hiyo unaendelea kukusanywa.

Inavyoonesha kesi hiyo haitafunguliwa tu iwapo itatokea Upinzani wameshinda kwani watachofanya ni kubadilisha Sheria ya Uchaguzi na kuruhusu matokeo ya URais kupingwa Mahakama Kuu.

Kwa hili CCM tupo tayari kwa kiasi gani kulipokea.
 
Mnahangaika sana yaani mahakama ya africa mashariki iingilie mambo ya kikatiba ya uchaguzi ndani ya nchi huru?
Huyo tundu lisu hachoki na kesi, hizo pesa za kesi atatoa wapi huku anaomba michango ya ubunge?.
 
Mnahangaika sana yaani mahakama ya africa mashariki iingilie mambo ya kikatiba ya uchaguzi ndani ya nchi huru?
Huyo tundu lisu hachoki na kesi, hizo pesa za kesi atatoa wapi huku anaomba michango ya ubunge?.
Mnajihami kupita kiasi hadi hueleweki. Issue ni Mahakama au fedha - eleza vizuri!
 
Yuko Ubeligiji amekimbia kesi za uchochezi, sasa hiyo kesi ataifungua vipi? Bado Polisi wanamhitaji aje atoe ushahidi juu ya tukio lililompata.
 
Mnajihami kupita kiasi hadi hueleweki. Issue ni Mahakama au fedha - eleza vizuri!

Kwanza ni mahakama haina uwezo wa kuingilia uchaguzi na sheria zake, kwani sheria zinatungwa na bunge la tanzania na si mahakama hiyo,
la pili hizo pesa angezifanyia kazi za maendeleo kuliko kuzipoteza

Kuna wananchi wanahitaji maji huko kwao angefanya hilo hata kuchimba kisima kimoja ingemsaidia sana.
 
Kwanza ni mahakama haina uwezo wa kuingilia uchaguzi na sheria zake, kwani sheria zinatungwa na bunge la tanzania na si mahakama hiyo,
la pili hizo pesa angezifanyia kazi za maendeleo kuliko kuzipoteza,
Kuna wananchi wanahitaji maji huko kwao angefanya hilo hata kuchimba kisima kimoja ingemsaidia sana.

Ndugu, dunia hii imeendelea sana- sijui kama umewahi kusika case inayohusu breaches of Fundamental rights and Freedoms. kama hujawahi, , nenda kawasome hawa watu- The Yusuf, Kadi, Ayadi and Hassan cases ... link nimekuwekea hapa na ujionee hata UN security council iligalagazwa na EU court kwa point hiyo hiyo ya breaches of securitu council. Kwa hiyo kesi ikipelekwa mahakani Tanzania kwa kipengele hicho tu cha breach if fundamentak rughts and freedok bila kipinga matokea, watawala kivumbi kitawatoka- hebu Soma hapa: European Court Rules on UN and EU Terrorist Suspect Blacklists | ASIL .

kwa ufupi, mahakama zetu hata kama ni mahakama ccm , zitajiuliza kama zina wajibu wa kulinda au kutetea respect fundamental rights au breaches zake- ikiwepo right to free and fair election, right to participate in an election na mengineyo.


Wengine wanaweza sema kwamba hii case haituhusu, lakini mlolongo wake umehusisha nchi nchi sana.. isomeni na mjue, siku zote ndege mjanja hunaswa na tundu bovu....ipo siku haya mambo yatafunguliwa kesi huko EU au UN, ili mradi kuwepo na legal standae na kuweza kuonyesha tu kwamba hizi breaches ziko against na charter ya UN- peace and security, na ikifika siku hiyo, dunia haitakaa kimya kusema kwamba haya mambo ni ya Tanzania pekee tuwaachie... Haitawezekana kwa sababu peace an security ni suala mtambuka na la dunia nzima... kinachohitajika ni mtu wa kuya- link matukio hayo na kufungua kesi kuonesha kwamba peace and security has been breached na matokea yako yaweza kuwa genocide....

Ni suala la muda tu...siku hiyo sijui kama nchi tutakuwa wapi- labda akina Fatu Bensouda -ICC na timu yake labda bado wanatuchungulia.
 
Tundu Lissu ana kesi ambazo yeye kama mtuhumiwa haonekani mahakamani kufungua kesi mahakamani ni kuonyesha dharau kwa mahakama
 
Tayari mpango mzuri na wenye maana kubwa sana katika Taifa letu unaendelea kuandaliwa. Uchaguzi wa Mwaka 2020 utakapokamilika tu na iwapo CCM watakuwa wameshinda kuna kesi itafunguliwa kwa umakini wa hali ya juu kuhusu kwa nini matokeo ya URais hayapingwi Mahakamani.

Kinachozuiwa nchini mwetu ni kwa kutofungua kesi ya kupinga matokeo ya URais lakini kuhusu kufungua kesi ya kuhoji kuwa ni "Kwa nini Matokeo ya URais hayapingwi Mahakamani" hakujazuiwa kufunguliwa kesi.

Tundu Lissu tayari amekuwa katika maandalizi ya kufungua kesi ya hivyo mara tu Uchaguzi utakapokamilika. Iwapo Mahakama Kuu ya Tanzania itakataa kesi ya hivyo kusajiliwa kwao tayari maandalizi ya kuisajili Mahakama ya Afrika Mashariki au ya Afrika nayo yanaendelea. Ushahidi wa mambo yanayotendeka ili kujenga hoja katika kesi hiyo unaendelea kukusanywa.

Inavyoonesha kesi hiyo haitafunguliwa tu iwapo itatokea Upinzani wameshinda kwani watachofanya ni kubadilisha Sheria ya Uchaguzi na kuruhusu matokeo ya URais kupingwa Mahakama Kuu.

Kwa hili CCM tupo tayari kwa kiasi gani kulipokea.
Mimi nafikiri baada ya jiwe kuondoka itabidi akimbilie nje ya nchi hata kama hawezi kuzungumza lugha zao.
Usimfananishe mtikila na vitu vya hovyo
Sasa kama CCM imeshinda unaenda mahakamani kuhoji nini, mnataka kurukwa akiri siyo?
Walikua wapi? Na hakuna wakulisimamia hilo,tuna wapinzani wa ajabu wanaowaza ruzuku tu.
Tundu Lissu ana kesi ambazo yeye kama mtuhumiwa haonekani mahakamani kufungua kesi mahakamani ni kuonyesha dharau kwa mahakama
 
Mnahangaika sana yaani mahakama ya africa mashariki iingilie mambo ya kikatiba ya uchaguzi ndani ya nchi huru?
Huyo tundu lisu hachoki na kesi, hizo pesa za kesi atatoa wapi huku anaomba michango ya ubunge?.
Ubunge gani mkuu,sio kwamba anawania urais kupitia Chadema?.
 
Hivi mleta mada unajua Tanzania ni monist state na siii dualist state
Uwe unafanya tafiti angalau kidogo

Huko mahakama ya Africa mashariki maamuzi yake yana ibind Tanzania?
 
Matokeo ya Urais Tanzania yakishasomwa tu na Mwenyekiti wa Tume ya uchaguzi basi muda huo huo yanageuka kuwa maandiko matakatifu - hakuna mwenye mamlaka kuhoji popote pale duniani.. labda mbinguni kama ana uwezo huo.

Hata hao wakoloni weupe aka mabeberu hawakuwa na sheria kandamizi kama hii.
 
Back
Top Bottom