Kama ilivyokuwa kwa Living With Michael Jackson Royal Tour ya Rais Samia yaweza kuwa na lengo baya kwa Tanzania

CreativityCode

Senior Member
Aug 8, 2020
158
653
Kwa mliofuatilia uandaaji na hatimaye kuoneshwa kwa makala maarufu ya Living With Michael Jackson mtakubaliana nami namna mwandishi mashuhuri Martin Bashiri alivyomrubuni, Mfalme wa Pop Duniani, Hayati Michael Jackson, kushiriki kwenye uandaaji wa makala kwa kumhakikishia kuwa makala hiyo ingelimtangaza vema na kubadili mtazamo wa dunia kuhusiana na kashfa alizokuwa akishutumiwa mwanamziki huyo. Hata hivyo badala ya kumsafisha Michael Jackson makala ya Living with Michael Jackson ilizidi kumchafua na kuibua tuhuma nyingi zaidi.

Kwa ufupi Martin Bashiri alikuwa na nia ovu dhidi ya Michael Jackson.

Nimefikiria sana ushiriki wa Rais Samia kwenye makala hii na kuwa na maswali mengi kichwani ikiwa ni kweli waandaaji wake wana nia njema na ya dhati kabisa ya kuitangaza vema nchi yetu na hatimaye kuvutia watalii na uwekezaji nchini. Kabla ya kushiriki ilitakiwa tufanye tathmini ya kina ikiwa ni pamoja na kuweka wazi wafadhili wa mradi huu na lengo lao hasa.

Nimeishi na raia wa nchi za magharibi kwa muda mrefu, pia nimetazama movie na makala nyingi sana zinazoihusisha Africa kwa movie nzima ama sehemu ndogo sijawahi kuona wamerekodi sehemu za kuvutia. Kwao ni umasikini na vita pekee ndiyo kipaombele. Katika vyote ni movie ya Black Panther pekee iliyoionesha Africa kuwa ni sehemu iliyoendelea zaidi japokuwa kwa kutumia fiction.

Ikiwa ni kweli wana nia njema na nchi yetu basi Rais Samia atakuwa amefanya jambo jema sana mbali na hapo tusubiri kuoneshwa umasikini, maradhi na ujinga wa nchi yetu ukitangazwa duniani kote.

Mara ingine nitakuja na ushauri mzuri wa namna bora ya kutangaza utalii na uwekezaji wa nchi yetu bila wala kutumia nguvu nyingi.

Nawatakia siku njema.
 
Wakati mwingine Mimi najiuliza huu ni muda mwafaka wa kutangaza utalii ukizingatia watalii wengi hawasafiri kutokana na Corona?

Je utalii ndiyo kipau mbele Cha taifa?.
Simuamini kabisa Kagame,na mama kapata wazo hili kwa Kagame.
huyu jamaa anaweza kutumiwa kwa Nia ovu na hawa mabeberu.
Mwendazake alimsoma akajitenga naye.
Na hawa wazungu ukiona wanakupenda ujue walishaona weakness yako wanatafuta pa kuingilia.
 
Kwa mliofuatilia uandaaji na hatimaye kuoneshwa kwa makala maarufu ya Living With Michael Jackson mtakubaliana nami namna mwandishi mashuhuri Martin Bashiri alivyomrubuni, Mfalme wa Pop Duniani, Hayati Michael Jackson, kushiriki kwenye uandaaji wa makala kwa kumhakikishia kuwa makala hiyo ingelimtangaza vema na kubadili mtazamo wa dunia kuhusiana na kashfa alizokuwa akishutumiwa mwanamziki huyo. Hata hivyo badala ya kumsafisha Michael Jackson makala ya Living with Michael Jackson ilizidi kumchafua na kuibua tuhuma nyingi zaidi.

Kwa ufupi Martin Bashiri alikuwa na nia ovu dhidi ya Michael Jackson.

Nimefikiria sana ushiriki wa Rais Samia kwenye makala hii na kuwa na maswali mengi kichwani ikiwa ni kweli waandaaji wake wana nia njema na ya dhati kabisa ya kuitangaza vema nchi yetu na hatimaye kuvutia watalii na uwekezaji nchini. Kabla ya kushiriki ilitakiwa tufanye tathmini ya kina ikiwa ni pamoja na kuweka wazi wafadhili wa mradi huu na lengo lao hasa.

Nimeishi na raia wa nchi za magharibi kwa muda mrefu, pia nimetazama movie na makala nyingi sana zinazoihusisha Africa kwa movie nzima ama sehemu ndogo sijawahi kuona wamerekodi sehemu za kuvutia. Kwao ni umasikini na vita pekee ndiyo kipaombele. Katika vyote ni movie ya Black Panther pekee iliyoionesha Africa kuwa ni sehemu iliyoendelea zaidi japokuwa kwa kutumia fiction.

Ikiwa ni kweli wana nia njema na nchi yetu basi Rais Samia atakuwa amefanya jambo jema sana mbali na hapo tusubiri kuoneshwa umasikini, maradhi na ujinga wa nchi yetu ukitangazwa duniani kote.

Mara ingine nitakuja na ushauri mzuri wa namna bora ya kutangaza utalii na uwekezaji wa nchi yetu bila wala kutumia nguvu nyingi.

Nawatakia siku njema.

Acha kumfananisha MJ na vitu vya kipumbavu
 
Wakati mwingine Mimi najiuliza huu ni muda mwafaka wa kutangaza utalii ukizingatia watalii wengi hawasafiri kutokana na Corona?

Je utalii ndiyo kipau mbele Cha taifa?.
Simuamini kabisa Kagame,na mama kapata wazo hili kwa Kagame.
huyu jamaa anaweza kutumiwa kwa Nia ovu na hawa mabeberu.
Mwendazake alimsoma akajitenga naye.
Na hawa wazungu ukiona wanakupenda ujue walishaona weakness yako wanatafuta pa kuingilia.
Utalii ndiyo chazo cha kwanza cha fedha za kigeni
 
Wako wapiga picha na watrngeneza sinema ya royal tour ambao mpaka sasa wameshuhuda mambo mengi yahusuyo Mh Rais kuanzia msafara na ulinzi wake. Mungu saidia wasiwe ni majasusi walio katika mission maalumu.
 
Daa huyo M Bashir ndio aliemrubuni Diana pia kwa ile interview
Ila ya Mama ngoja tuone
 
Kiongozi tupe mkasa kamili kuhusu hiyo jamaa Mr Bashir

Sent using Jamii Forums mobile app

Martin Bashir alikuwa ni reporter wa BBC zamani
Na tarehe 31/08/1995 alimshawishi Earl Spencer ambae ni kaka yake na Princess Diana ili afanye interview na dada yake

Bashir alimdanganya Spencer kuwa kuna washauri wa Charles na Diana ambao wanapewa hela ili wamchunguze Diana kila mienendo yake
Na akamuonyesha cheque za Bank feki
Spencer kaka wa Diana ikabidi amwambie dada yake kuwa kumbe unafuatiliwa kila unachofanya na wanajua kila kitu
Itabidi ufanye interview na Martin Bashir na ukweli ujulikane

Kumbe ulikuwa ni mtego na Diana alikuwa kajaa haswa kwa mambo aliyokuwa anafanyiwa na Charles (mume wake )

Kwenye interview Diana alifunguka haswa na kuropoka mengi na ilikuwa mahojiano ya kwanza kwa mmoja wa Royal family kuongea hadharani tena kuangaliwa na umati wa 20m kwenye tv

Alikiri kuwa alitembea na wanaume
Akasema kuwa yumo kwenye ndoa ya watu watatu akiwa na maana yeye, Charles na Camilla

Martin Bashir alikuwa na tuhuma nzito sana na alikana kabisa kuwa hakuonyesha documents fake mara kadhaa
Na aliendelea kukana akijua kabisa anadanganya
Kitu cha kushangaza sasa
Hiyo tarehe aliokutana na kaka yake Diana baada ya miaka miwili tarehe hiyo hiyo Diana akafariki akiwa na mshkaji wake Dodi Al Fayed na dereva wao

Ni muda sasa ila nakumbuka sana hilo tukio kwani nilikuwepo siku ya kuuaga mwili wa People’s Princess
 
Martin Bashir alikuwa ni reporter wa BBC zamani
Na tarehe 31/08/1995 alimshawishi Earl Spencer ambae ni kaka yake na Princess Diana ili afanye interview na dada yake

Bashir alimdanganya Spencer kuwa kuna washauri wa Charles na Diana ambao wanapewa hela ili wamchunguze Diana kila mienendo yake
Na akamuonyesha cheque za Bank feki
Spencer kaka wa Diana ikabidi amwambie dada yake kuwa kumbe unafuatiliwa kila unachofanya na wanajua kila kitu
Itabidi ufanye interview na Martin Bashir na ukweli ujulikane

Kumbe ulikuwa ni mtego na Diana alikuwa kajaa haswa kwa mambo aliyokuwa anafanyiwa na Charles (mume wake )

Kwenye interview Diana alifunguka haswa na kuropoka mengi na ilikuwa mahojiano ya kwanza kwa mmoja wa Royal family kuongea hadharani tena kuangaliwa na umati wa 20m kwenye tv

Alikiri kuwa alitembea na wanaume
Akasema kuwa yumo kwenye ndoa ya watu watatu akiwa na maana yeye, Charles na Camilla

Martin Bashir alikuwa na tuhuma nzito sana na alikana kabisa kuwa hakuonyesha documents fake mara kadhaa
Na aliendelea kukana akijua kabisa anadanganya
Kitu cha kushangaza sasa
Hiyo tarehe aliokutana na kaka yake Diana baada ya miaka miwili tarehe hiyo hiyo Diana akafariki akiwa na mshkaji wake Dodi Al Fayed na dereva wao

Ni muda sasa ila nakumbuka sana hilo tukio kwani nilikuwepo siku ya kuuaga mwili wa People’s Princess
Nashukulu Sana kiongozi kumbe unayajua mengi Sana kuhusu hii loyal family ya United kingdom.Nakuomba kwa unyenyekevu mkubwa siku ukipata muda dondosha kisa Cha ndoa ya Princess Diana na prince Charles iwe from the biginng hadi mwisho I mean walivokutana,uchumba,ndoa,migogolo ya ndo hadi kifo Cha Princess Diana.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kwa mliofuatilia uandaaji na hatimaye kuoneshwa kwa makala maarufu ya Living With Michael Jackson mtakubaliana nami namna mwandishi mashuhuri Martin Bashiri alivyomrubuni, Mfalme wa Pop Duniani, Hayati Michael Jackson, kushiriki kwenye uandaaji wa makala kwa kumhakikishia kuwa makala hiyo ingelimtangaza vema na kubadili mtazamo wa dunia kuhusiana na kashfa alizokuwa akishutumiwa mwanamziki huyo. Hata hivyo badala ya kumsafisha Michael Jackson makala ya Living with Michael Jackson ilizidi kumchafua na kuibua tuhuma nyingi zaidi.

Kwa ufupi Martin Bashiri alikuwa na nia ovu dhidi ya Michael Jackson.

Nimefikiria sana ushiriki wa Rais Samia kwenye makala hii na kuwa na maswali mengi kichwani ikiwa ni kweli waandaaji wake wana nia njema na ya dhati kabisa ya kuitangaza vema nchi yetu na hatimaye kuvutia watalii na uwekezaji nchini. Kabla ya kushiriki ilitakiwa tufanye tathmini ya kina ikiwa ni pamoja na kuweka wazi wafadhili wa mradi huu na lengo lao hasa.

Nimeishi na raia wa nchi za magharibi kwa muda mrefu, pia nimetazama movie na makala nyingi sana zinazoihusisha Africa kwa movie nzima ama sehemu ndogo sijawahi kuona wamerekodi sehemu za kuvutia. Kwao ni umasikini na vita pekee ndiyo kipaombele. Katika vyote ni movie ya Black Panther pekee iliyoionesha Africa kuwa ni sehemu iliyoendelea zaidi japokuwa kwa kutumia fiction.

Ikiwa ni kweli wana nia njema na nchi yetu basi Rais Samia atakuwa amefanya jambo jema sana mbali na hapo tusubiri kuoneshwa umasikini, maradhi na ujinga wa nchi yetu ukitangazwa duniani kote.

Mara ingine nitakuja na ushauri mzuri wa namna bora ya kutangaza utalii na uwekezaji wa nchi yetu bila wala kutumia nguvu nyingi.

Nawatakia siku njema.
It was by then 'Tanzania ya viwanda' the slogan that suddenly vanished in the thin air welcoming the most trumpeted versive era nicknamed as 'Rebranding Tanzania of Tourism' featuring the head of state spearheading the tune to be sung externally and internally with hitherto uncertainty gain hope as normal civilians perceive it.
 
Nashukulu Sana kiongozi kumbe unayajua mengi Sana kuhusu hii loyal family ya United kingdom.Nakuomba kwa unyenyekevu mkubwa siku ukipata muda dondosha kisa Cha ndoa ya Princess Diana na prince Charles iwe from the biginng hadi mwisho I mean walivokutana,uchumba,ndoa,migogolo ya ndo hadi kifo Cha Princess Diana.

Sent using Jamii Forums mobile app

Tuko pamoja sana
Nina miaka 30 huku kwa hiyo nawajua vizuri kwa kusoma na kufuatilia habari zao kama watu mashuhuri wa nchi hii
Mimi sio mwandishi mzuri ila kuna nyuzi humu ambazo nimechangia sana kuhusu Charles na Di
Hata Malkia na mume wake pia kaongelewa sana na mimi nikiwa mchangiaji

Sijui kuweka link na sikumbuki topic zinaitwaje ila unaweza kuzipata kama utaandika Diana
Asante
 
Back
Top Bottom