Kama ilivyoisha bomoa bomoa, zikafuata ziara za kushutukiza, kinachofuata kufa ni tumbua tumbua

mpk

JF-Expert Member
Sep 26, 2012
3,115
3,862
Nadhani mnakumbuka mkwara wa kubomoa nyumba zote zilizojengwa kinyume cha utaratibu. Majiji yakaja na takwimu ya kuvunja maelfu ya majengo. Tukaambiwa hotel kubwa kubwa zilizojengwa ufukweni zitashushwa kama ubua. Mpaka sasa hatujui zoezi lilikwishaje! Mabangaroo bado yanapendeza ufukweni

Tunakumbuka pia safari za kushutukiza. Bandarini, TRA, Benki kuu, Muhimbili na mawaziri wakishutukiza kila mahali. Wengine walienda na waandishi alfajiri kuwafungia watu milango ya ofisi, kutoa siku 7 au 14, mwezi nk. Leo sikumbuki ziara ya mwisho ya kushutukiza ilifanyika lini na wapi!

Linaloelekea kufa jingine ni tumbua majipu. Nilishasema kwamba serikali hii ilikuwa haitumbui bali ilikuwa inateua watu wapya kwenye nafasi mbali mbali. Ilikuwa lazima umuondoe mtu fulani nafasi fulani ili umteu mtu mwingine. Lakini zoezi hilo ikabidi liingize sifa kidogo! Inabidi yule unayemuondoa utangaze umemtumbua. Kama unabisha hilo nikumbushe nafasi za uteuzi zilipopungua au kuisha ni lini umesikia mtu anatumbuliwa?
 
Anayebisha atwambie nilichouliza hapo juu ulikisikia lini siyo mapovu
 
Si kuna watu wanataka taratibu zifuatwe? Kama jengo linalotakiwa kubomolewa lina kesi mahakamani ulitaka libomolewe ili uje kusema mahakama haziheshimiwi? tutajie majengo yanayotakiwa kubomolewa na hayana kizuizi chochote ila serikali imeshindwa kufanya hivyo, umejipa muda kufatilia mazuio mawili yaliyowekwa na mahakama baada ya Mh. Mbunge wa Ukonga na Kinondoni kufungua kesi za kupinga hatua hizo? Tutajie ni hotel gani iliyotakiwa kubomolewa ns mpaka leo bado.
Kwani ziara za kushtukiza zilikuwa sera ya kudumu mpaka uhoji kwanini haziendelei? ulijipa muda kuhoji kwanini watu walifanya ziara hizo na baada ya ziara hizo uliona nini?
Kwenye kutumbua nani unahisi alionewa kabisa na hakukuwa na sababu yoyote ile ya yeye kusimamishwa kazi, na je kutumbua ilikuwa ni sera ya kudumu mpaka uhoji kwanini imesitishwa? Je ni wapi unahisi panastahili kutumbuliwa ila pameshindikana kwasabu muhusika ni mpya.
 
Back
Top Bottom