Ben Zen Tarot
JF-Expert Member
- Dec 13, 2014
- 3,907
- 6,700
Kitendo cha Mungu kumtupa Ibilisi duniani ni kitendo cha uonevu mkubwa sana kwa binadamu.
Ibilisi sio levo za binadamu ni levo ya Mungu maana yake Mungu yeye angekomaa naye Ibilisi hukohuko mbinguni mpaka kieleweke. Kutuletea Ibilisi huku duniani ni kutuonea tu maana hatuna uwezo wowote wa kupambana naye.
Kama Ibilisi aliweza kupigana vita kuu mbinguni akiwa na malaika wake sasa binadamu ataweza kweli kupambana na kiumbe kama hiki?
Kiumbe ambacho kiliweza kupambana na malaika wa Mungu na kikafanikiwa kuwashawishi baadhi ya malaika kwenye vita kuu mbinguni na wakaasi sasa wewe binadamu utaweza kweli kupambana na Ibilisi?
Kama mbinguni tu Ibilisi alisumbua sana ambako ndiyo kuna Mungu na malaika huku duniani tutamuweza kweli?
Kama Ibilisi anauwezo wa kuingilia mipango ya Mungu na kuiharibu kama ule wa bustani ya Edeni na Mungu hamfanyi chochote anaishia tu kuwapa adhabu zisizo na maana yoyote Adam na Hawa. Hiki kiumbe sisi binadamu tutakiweza kweli?
Ilifikia hatua Mungu mwenyewe aliamua kumtoa kafara mwanaye wa pekee( Yesu) ili aweze kupambana na Ibilisi ila mission ikabuma. Sisi binadamu tutaweza kweli kupambana na Ibilisi?
Hivi unajua kama Ibilisi anaongea na Mungu moja kwa moja? Maana yake Mungu na Ibilisi huwa wanaonana. Unajua mazungumzo ya Mungu na Ibilisi kuhusu Ayubu? Sasa sisi binadamu tutaweza kweli kupambana na Ibilisi anayeweza kuongea na Mungu moja kwa moja?
Hivi Mungu aliwaza nini mpaka akaamua kututupia Ibilisi duniani?
Hapa binadamu tumeonewa sana.
Jukumu la kupambana na Ibilisi ni jukumu la Mungu mwenyewe na sio la binadamu hivyo Mungu amtoe Ibilisi duniani na akaishi naye mbinguni sisi huku hatumuwezi.
Ndio maana imekuwa ni kawaida tu kumkuta mtu ni mfia dini haswa ila ni mzinifu,muongo,muuaji,mchawi,tapeli,mwizi, mnafiki n.k.
Nani kakudanganya kuna binadamu anaweza kupambana na Ibilisi?
Ibilisi sio levo za binadamu ni levo ya Mungu maana yake Mungu yeye angekomaa naye Ibilisi hukohuko mbinguni mpaka kieleweke. Kutuletea Ibilisi huku duniani ni kutuonea tu maana hatuna uwezo wowote wa kupambana naye.
Kama Ibilisi aliweza kupigana vita kuu mbinguni akiwa na malaika wake sasa binadamu ataweza kweli kupambana na kiumbe kama hiki?
Kiumbe ambacho kiliweza kupambana na malaika wa Mungu na kikafanikiwa kuwashawishi baadhi ya malaika kwenye vita kuu mbinguni na wakaasi sasa wewe binadamu utaweza kweli kupambana na Ibilisi?
Kama mbinguni tu Ibilisi alisumbua sana ambako ndiyo kuna Mungu na malaika huku duniani tutamuweza kweli?
Kama Ibilisi anauwezo wa kuingilia mipango ya Mungu na kuiharibu kama ule wa bustani ya Edeni na Mungu hamfanyi chochote anaishia tu kuwapa adhabu zisizo na maana yoyote Adam na Hawa. Hiki kiumbe sisi binadamu tutakiweza kweli?
Ilifikia hatua Mungu mwenyewe aliamua kumtoa kafara mwanaye wa pekee( Yesu) ili aweze kupambana na Ibilisi ila mission ikabuma. Sisi binadamu tutaweza kweli kupambana na Ibilisi?
Hivi unajua kama Ibilisi anaongea na Mungu moja kwa moja? Maana yake Mungu na Ibilisi huwa wanaonana. Unajua mazungumzo ya Mungu na Ibilisi kuhusu Ayubu? Sasa sisi binadamu tutaweza kweli kupambana na Ibilisi anayeweza kuongea na Mungu moja kwa moja?
Hivi Mungu aliwaza nini mpaka akaamua kututupia Ibilisi duniani?
Hapa binadamu tumeonewa sana.
Jukumu la kupambana na Ibilisi ni jukumu la Mungu mwenyewe na sio la binadamu hivyo Mungu amtoe Ibilisi duniani na akaishi naye mbinguni sisi huku hatumuwezi.
Ndio maana imekuwa ni kawaida tu kumkuta mtu ni mfia dini haswa ila ni mzinifu,muongo,muuaji,mchawi,tapeli,mwizi, mnafiki n.k.
Nani kakudanganya kuna binadamu anaweza kupambana na Ibilisi?