Ndo hivyo mkuu tayari taarifa zao zinarushwaHatubishi bali tunaona ni Maajabu makubwa sana kama siyo mno kwa Leo hii Simba kuomba kuwa na Urafiki mwema na Swala au akina Nyumbu.
Cha kuzimuKwani TBC inapatikana kwenye King'amuzi gani?
Mkurugenzi Mtendaji wa TBC Dkt. Ayoub Rioba amesema chombo hicho cha habari hakibagui chama chochote cha siasa katika kurusha matangazo.
Dkt. Rioba amesema kuwa chombo hicho cha umma hakibagui chama bali wanatimiza wajibu wa kuwahabarisha wananchi kama inavyopaswa na sio kukaa kwenye mrengo mmoja wa chama kimoja.
Dkt.Rioba pia amesema baadhi ya vyama vilifikia hatua kukataa kushiriki kwenye vipindi endapo wanaalikwa ndani ya chombo hicho cha umma.
Aidha, amesema ikitokea vyama vya siasa vinaenda kuomba muda wa kipindi au matangazo chombo hicho cha umma kinatoa fursa na nafasi kwa vyama vyote nchini na anavikaribisha vyama vyote kwenye chombo hicho cha umma hususani kuelekea kipindi hiki cha uchaguzi Mkuu bila ubaguzi wowote.
Habari Star TV Tanzania
Kuna Mtu Mmoja aliwahi Kuniambia Mzukulu kuwa kuna tofauti kubwa sana kati ya Kuongea na Kutenda au Uhalisia na Ukweli wa Jambo husika.
Shirika lenyewe tu linatambulika kama TBCCM! Halafu litapata wapi sifa ya kurusha matangazo bila ya ubaguzi wa kisiasa na kiitikadi? Watangazaji wake wote ni Ccm na wamekaa standby kusubiria uteuzi wa Ukuu wa Wilaya na U DED kitoka kwa Mwenyekiti wa chama!
TBC ilijitahidi kuwa neutral enzi zile Mkurugenzi Mtendaji akiwa ni muasisi wake Mh.Tido Mhando. Baada kusababisha mvurugano kwenye ule uchaguzi mkuu wa 2010, tunakumbuka kilichoikuta TBC na huyo Tido mwenyewe miezi michache baadaye.
NgawethuHawezi kutumbuliwa kwa kusema alichosema. Asingeweza kusema kuwa wao kama combo cha umma wanapendelea Chama au mtu. Kusema alichosema ni ushahidi kuwa anajua taasisi anayoiongoza inatazamwa visivyo katika sehemu ya jamii. Vitendo vyake ndio vitathibitisha kama hawamtendei haki au la, sio maneno yake. Na anajua hilo. Na viongozi wake wanajua hilo.
Amanda...
Ngoja tumpe benefit of doubt, nimemuoana leo akiwa Star TV kwenye kipindi cha jicho letu ndani ya habari akiwa kwenye mjadala na nguli Dotto Bulendu. Natagemea nione mabadiliko kuanzia sasa kama ni kweli alichokisema.
Na Wewe unamwamini kabisa tena 100% huyo DG wa TBC juu ya alichokisema Ndugu? Yaani TBC waturushie Maudhui ya Madongo ya Wapinzani?