GAGL
JF-Expert Member
- Aug 5, 2010
- 390
- 392
Mwanzoni mwa mwaka huu kama si mwishoni mwaka jana, kipindi cha orijino komedi kinachorushwa kupitia TBC, kilirusha uchakavu na utelekezwaji wa makumbusho ya mzalendo wa kweli hayati Edward Moringe Sokoine. Kwa kweli palionesha hali mbaya sana pale.
Leo nimepita pale nimeona kuna ujenzi unaendelea na bila shaka itakuwa ni sehemu ya uboreshaji wa makumbusho hayo. Kwa mara nyingine serikali inatimiza wajibu wake baada ya kusimangwa tena na vijana wanaoendesha maisha yao kwa kutumia vipaji na si elimu.
Serikali imejaa wasomi na wataalamu wa kada mbalimbali ila wameshindwa kuona hata jambo hili lililo na impact kubwa katika historia ya nchi yetu hadi waliposimangwa na orijino komedi!
Hivi hii serikali ni lini itatimiza wajibu wake kwa hiari? Hongereni sana orijino komedi.
Leo nimepita pale nimeona kuna ujenzi unaendelea na bila shaka itakuwa ni sehemu ya uboreshaji wa makumbusho hayo. Kwa mara nyingine serikali inatimiza wajibu wake baada ya kusimangwa tena na vijana wanaoendesha maisha yao kwa kutumia vipaji na si elimu.
Serikali imejaa wasomi na wataalamu wa kada mbalimbali ila wameshindwa kuona hata jambo hili lililo na impact kubwa katika historia ya nchi yetu hadi waliposimangwa na orijino komedi!
Hivi hii serikali ni lini itatimiza wajibu wake kwa hiari? Hongereni sana orijino komedi.