GENTAMYCINE
JF-Expert Member
- Jul 13, 2013
- 56,544
- 108,872
Nimeshtushwa, nimeogopa na nimekosa raha hadi hivi sasa kwani kwa muda sasa nimekuwa nikisia katika pitapita zangu huku na kule kwamba Siku hizi Watanzania wamekuja na ' Ubunifu ' wa Kipekee kabisa ambao unaweza ukamfanya Mtu akiwa anaenda Kupima VVU / UKIMWI na Mwenza wake basi ' Vipimo ' visisome kuwa tayari analipiga vyema Gitaa la Dally Kimoko ( yaani ameshaathirika )
Inasemakana kwamba Mtu akiyafanya haya ndani ya Saa 24 hata kama ameshaathirika na Dally Kimoko / UKIMWI basi zile ' Mashine ' za Kupima kama zitapima basi zitaishia tu kuona Dagaa na Matembele aliyokula au Ugali wa Kiporo kama si Ubwabwa ila ' Virusi ' vyenyewe havitaonekana ng'o.
Wanasema kwamba........
Tafadhalini Serikali kupitia Wizara husika ya Afya na Madaktari mliopo hapa Jamvini JamiiForums tusaidieni katika hili kwani Binafsi hofu imeshatanda Moyoni mwangu hasa ikizingatiwa kuwa wengi wetu tumepita Kwingi na huko Kote ' Kofia Ngumu ' namaanisha ' Helmet ya Kibaiolojia ' ilikuwa haitumiki na kila tuliokuwa tunapima nao majibu yao yalikuwa ni ' Negative ' sasa hatujui ' Negative ' hivyo ni ya Kipimo tu au Mhusika Moyoni mwake alikuwa anajua kabisa kuwa tayari ni ' Positive ' na kwamba anatuua Sisi wengine?
Na endapo haya yanayosemwa huku Mitaani na niliyoyataja hapa ni kweli basi nadhani wengi Wetu huu ni muda sahihi tu wa Kuanza Kuandika Majina ya ' Warithi ' Wetu wa Mali ( Kama pia Mali zenyewe tunazo ) na tutoea tu mapema Maelekezo ya ni wapi tukifa kama siyo Kufariki tukazikwe kama ni hapa hapa Mjini kama alivyofanyiwa Ephraim Kibonde au tupelekwe nasi Vijijini Kwetu kama ambavyo alifanyiwa Ruge Mutahaba.
Nina hofu kubwa na hii Kitu hadi nimekosa hata hamu ya Kula. Madaktari wa hapa JF nitoeni Hofu GENTAMYCINE haraka.
Nawasilisha.
Inasemakana kwamba Mtu akiyafanya haya ndani ya Saa 24 hata kama ameshaathirika na Dally Kimoko / UKIMWI basi zile ' Mashine ' za Kupima kama zitapima basi zitaishia tu kuona Dagaa na Matembele aliyokula au Ugali wa Kiporo kama si Ubwabwa ila ' Virusi ' vyenyewe havitaonekana ng'o.
Wanasema kwamba........
- Kama Muathirika akila kwa KitiMoto akienda Kupima hatojulikana kama anao.
- Kama Muathirika akinywa Bia ya Safari tu au Gongo ile ya Mvuke wa Kinyesi ( Kali ) akipima hatojulikana kama anao.
- Kama Muathirika akinywa Maziwa ya Mtindi akipima hatojulikana kama anao
- Kama Muathirika akinywa Vidonge vya Pumu aina ya Salbutamol basi akipima ataonekana hana.
- Kama Muathirika akinywa Chai ya Mdalasini akipima hatojulikana kama anao.
- Kama Muathirika akijishindilia vyema Mtori akipima hatojulikana kama anao.
- Kama Muathirika akila sana Kumbikumbi / Senene akipima ataambiwa hana.
Tafadhalini Serikali kupitia Wizara husika ya Afya na Madaktari mliopo hapa Jamvini JamiiForums tusaidieni katika hili kwani Binafsi hofu imeshatanda Moyoni mwangu hasa ikizingatiwa kuwa wengi wetu tumepita Kwingi na huko Kote ' Kofia Ngumu ' namaanisha ' Helmet ya Kibaiolojia ' ilikuwa haitumiki na kila tuliokuwa tunapima nao majibu yao yalikuwa ni ' Negative ' sasa hatujui ' Negative ' hivyo ni ya Kipimo tu au Mhusika Moyoni mwake alikuwa anajua kabisa kuwa tayari ni ' Positive ' na kwamba anatuua Sisi wengine?
Na endapo haya yanayosemwa huku Mitaani na niliyoyataja hapa ni kweli basi nadhani wengi Wetu huu ni muda sahihi tu wa Kuanza Kuandika Majina ya ' Warithi ' Wetu wa Mali ( Kama pia Mali zenyewe tunazo ) na tutoea tu mapema Maelekezo ya ni wapi tukifa kama siyo Kufariki tukazikwe kama ni hapa hapa Mjini kama alivyofanyiwa Ephraim Kibonde au tupelekwe nasi Vijijini Kwetu kama ambavyo alifanyiwa Ruge Mutahaba.
Nina hofu kubwa na hii Kitu hadi nimekosa hata hamu ya Kula. Madaktari wa hapa JF nitoeni Hofu GENTAMYCINE haraka.
Nawasilisha.