Waliomuibia Dk Chami waendeleza ubabe
Saturday, 15 October 2011 07:56
Daniel Mjema, Moshi
KUNDI la wahalifu linalodaiwa kuvunja nyumba ya Waziri wa Viwanda, Biashara na Masoko, Dk Cyrill Chami na kuiba vitu mbalimbali usiku wa kuamkia juzi, limetishia kuendeleza uhalifu katika familia ya waziri huyo.
*
Licha ya Kamanda wa Polisi Mkoa Kilimanjaro, Absolom Mwakyoma kutuma kikosi cha polisi wa pikipiki, iteligensia na upelelezi juzi ili kuwasaka wahalifu hao, kundi hilo lilirudi tena katika nyumba hiyo usiku wa kuamkia jana.
*
Habari za uhakika zilizopatikana jana, zilisema tukio la wezi hao kuingia nyumbani kwa Dk Chami ambaye pia ni Mbunge wa Moshi Vijijini (CCM), lilitokea Kijiji cha Manushi, Kibosho usiku wa kuamkia juzi.
*
Kamanda Mwakyoma alipotafutwa jana, alikataa kuzungumza lolote kwa hoja kwamba hakuwa mahali pazuri pa kufanya hivyo, lakini Dk Chami alisema hakuwapo wakati tukio hilo likitokea.
Kwa mujibu wa Dk Chami katika kundi hilo, yupo mhalifu sugu maarufu Askofu na kwamba ametishia kumuua mama yake mzazi, Agness Chami kama njia ya kulipiza kisasi.
*
Ametishia kumchinja mama yangu kwa sababu alimtaja Askofu baada ya polisi kufika kijijini hapo, amedhamiria, hata usiku wa kuamkia leo (jana) 'Askofu' na kundi lake walikuja tena nyumbani,alifafanua Dk Chami.
*
Waziri Chami alisema kutokana na vitisho hivyo, jana aliwasiliana na Kamanda Mwakyoma ambaye alimshauri amhamishe mama yake na kumpeleka eneo lenye usalama wakati polisi wakimsaka mhalifu huyo.
*
Akizungumzia tukio hilo, Dk Chami alisema siku hiyo usiku, wezi walivunja milango miwili ya nyumba yake na kuiba vitu mbalimbali vya elektroniki.
*
Unajua walipanga wavamie ile nyumba wakati mimi nipo kwa sababu wanajua nimekuja kwa ziara ya jimboni, lakini bahati nzuri mimi sikuwa nimelala humo, nafikiri tungekuwa tunazungumza mengine,alisema.
*
Waziri Chami alisema baada ya kuvunja milango hiyo miwili, waliingia ndani na kuiba televisheni moja, mashine ya DVD, seti ya muziki na begi kubwa la nguo ambalo walidhani kuna fedha au bastola.
*
*Tatizo ninaloliona hapa ni kwamba huyu 'Askofu' siku zote hatajwi kwenye vyombo vya dola kwa sababu anaogopwa sana na hili limempa nguvu ya kufanya hayo anayoyafanya bila uwoga wa kukamatwa,alisema.
*
Chami alisema anaamini polisi wataendelea kutekeleza wajibu wao wa kulinda raia na mali zao. Alisema tishio la kuuawa kwa mama yake limeripotiwa polisi.
source:Gazeti mwananchi
Saturday, 15 October 2011 07:56
Daniel Mjema, Moshi
KUNDI la wahalifu linalodaiwa kuvunja nyumba ya Waziri wa Viwanda, Biashara na Masoko, Dk Cyrill Chami na kuiba vitu mbalimbali usiku wa kuamkia juzi, limetishia kuendeleza uhalifu katika familia ya waziri huyo.
*
Licha ya Kamanda wa Polisi Mkoa Kilimanjaro, Absolom Mwakyoma kutuma kikosi cha polisi wa pikipiki, iteligensia na upelelezi juzi ili kuwasaka wahalifu hao, kundi hilo lilirudi tena katika nyumba hiyo usiku wa kuamkia jana.
*
Habari za uhakika zilizopatikana jana, zilisema tukio la wezi hao kuingia nyumbani kwa Dk Chami ambaye pia ni Mbunge wa Moshi Vijijini (CCM), lilitokea Kijiji cha Manushi, Kibosho usiku wa kuamkia juzi.
*
Kamanda Mwakyoma alipotafutwa jana, alikataa kuzungumza lolote kwa hoja kwamba hakuwa mahali pazuri pa kufanya hivyo, lakini Dk Chami alisema hakuwapo wakati tukio hilo likitokea.
Kwa mujibu wa Dk Chami katika kundi hilo, yupo mhalifu sugu maarufu Askofu na kwamba ametishia kumuua mama yake mzazi, Agness Chami kama njia ya kulipiza kisasi.
*
Ametishia kumchinja mama yangu kwa sababu alimtaja Askofu baada ya polisi kufika kijijini hapo, amedhamiria, hata usiku wa kuamkia leo (jana) 'Askofu' na kundi lake walikuja tena nyumbani,alifafanua Dk Chami.
*
Waziri Chami alisema kutokana na vitisho hivyo, jana aliwasiliana na Kamanda Mwakyoma ambaye alimshauri amhamishe mama yake na kumpeleka eneo lenye usalama wakati polisi wakimsaka mhalifu huyo.
*
Akizungumzia tukio hilo, Dk Chami alisema siku hiyo usiku, wezi walivunja milango miwili ya nyumba yake na kuiba vitu mbalimbali vya elektroniki.
*
Unajua walipanga wavamie ile nyumba wakati mimi nipo kwa sababu wanajua nimekuja kwa ziara ya jimboni, lakini bahati nzuri mimi sikuwa nimelala humo, nafikiri tungekuwa tunazungumza mengine,alisema.
*
Waziri Chami alisema baada ya kuvunja milango hiyo miwili, waliingia ndani na kuiba televisheni moja, mashine ya DVD, seti ya muziki na begi kubwa la nguo ambalo walidhani kuna fedha au bastola.
*
*Tatizo ninaloliona hapa ni kwamba huyu 'Askofu' siku zote hatajwi kwenye vyombo vya dola kwa sababu anaogopwa sana na hili limempa nguvu ya kufanya hayo anayoyafanya bila uwoga wa kukamatwa,alisema.
*
Chami alisema anaamini polisi wataendelea kutekeleza wajibu wao wa kulinda raia na mali zao. Alisema tishio la kuuawa kwa mama yake limeripotiwa polisi.
source:Gazeti mwananchi